Tajiri wa kusini
JF-Expert Member
- Nov 28, 2022
- 1,079
- 2,947
Nilimsomesha CHUO akaniacha na Kwenda kuolewa MKE wapili!
Nilihangaika mpaka nikamlipia ada. Kipindi hicho, mimi nilikuwa nimemaliza diploma, yeye alikuwa anasoma digrii. Katikati ya masomo, baba yake aliyekuwa anamsomesha alifariki, hivyo kama mwanaume, kwa kuwa yeye hakuwa ameanza kufanya kazi, niliamua kupiga bodaboda na nikapata ya mkataba. Nilikuwa nahangaika sana, lakini bado nilikuwa namhudumia.
Mwaka wake wa pili chuoni, nilimhudumia kwa kila kitu, mpaka mama yake alifahamu juhudi zangu na alinipa heshima kubwa. Baada ya kumaliza masomo, nilimtafutia mchongo akawa anajitolea TRA, na hatimaye akapata kazi pale. Mwaka mmoja, tukiwa kwenye maandalizi ya harusi, aliajiriwa rasmi. Kipindi hicho, alikuwa na ujauzito wa miezi saba. Siku moja nilipewa taarifa kuwa amelazwa hospitalini ujauzito umeharibika.
Ukweli, kiumbe kilichotolewa kilikuwa kama mtoto kamili kabisa, lakini hakikudumu dakika mbili kikafariki. Nilifika nikiwa nimechelewa, na ndipo niliulizwa tunamzika wapi mtoto. Niliumia sana kumwangalia mke wangu akiwa amenyong’onyea kitandani, iliniumiza sana kuona hali hiyo.
Nilimhangaikia sana mpaka alipokuwa sawa. Nikamwambia tuendelee na mipango ya ndoa, lakini akanambia tusubiri kwanza. Nilipomuuliza kwa nini, akanijibu kuwa amepoteza mtoto, hivyo hataki kusherehekea. Nilimuelewa, na kuna wakati nilihisi vibaya kumwambia kuhusu ndoa wakati alikuwa amepoteza mtoto. Nilimuomba msamaha na mambo yakaisha.
Baada ya wiki mbili, nasikia mchumba wangu anaolewa. Kuna mwanaume kamvisha pete, nikamuuliza kulikoni. Akanijibu amepata mtu wake hivyo kama ni pesa ya kumsomeshea nimuambie tanilipa. Nilidhani ni utani, lakini hata mama yake aliniambia, "Wewe bado unajitafuta tu, mwanangu ana kazi nzuri, utamrudisha nyuma."
Walifunga ndoa na yule mwanaume, na akawa mke wa pili. Ni mzee mtu mzima, walikutana huko kazini, akiwa na kampuni yake. Inaonekana waliingia kwenye uhusiano baada ya kufanya kazi pamoja kwenye mahesabu. Iliniumiza sana, lakini nilikuja kugundua kuwa hata mimba alitoa kwa sababu mwanaume alimwambia hataki kulea mtoto wa mtu mwingine.
Hapo ndipo nilipompotezea na kuamua kuendelea na maisha yangu. Sikutaka kulipwa chochote, niliendelea na maisha yangu, lakini mpaka sasa bado sijapata nafuu kabisa. Hata hivyo, maisha yanaendelea.
MWISHO
Nilihangaika mpaka nikamlipia ada. Kipindi hicho, mimi nilikuwa nimemaliza diploma, yeye alikuwa anasoma digrii. Katikati ya masomo, baba yake aliyekuwa anamsomesha alifariki, hivyo kama mwanaume, kwa kuwa yeye hakuwa ameanza kufanya kazi, niliamua kupiga bodaboda na nikapata ya mkataba. Nilikuwa nahangaika sana, lakini bado nilikuwa namhudumia.
Mwaka wake wa pili chuoni, nilimhudumia kwa kila kitu, mpaka mama yake alifahamu juhudi zangu na alinipa heshima kubwa. Baada ya kumaliza masomo, nilimtafutia mchongo akawa anajitolea TRA, na hatimaye akapata kazi pale. Mwaka mmoja, tukiwa kwenye maandalizi ya harusi, aliajiriwa rasmi. Kipindi hicho, alikuwa na ujauzito wa miezi saba. Siku moja nilipewa taarifa kuwa amelazwa hospitalini ujauzito umeharibika.
Ukweli, kiumbe kilichotolewa kilikuwa kama mtoto kamili kabisa, lakini hakikudumu dakika mbili kikafariki. Nilifika nikiwa nimechelewa, na ndipo niliulizwa tunamzika wapi mtoto. Niliumia sana kumwangalia mke wangu akiwa amenyong’onyea kitandani, iliniumiza sana kuona hali hiyo.
Nilimhangaikia sana mpaka alipokuwa sawa. Nikamwambia tuendelee na mipango ya ndoa, lakini akanambia tusubiri kwanza. Nilipomuuliza kwa nini, akanijibu kuwa amepoteza mtoto, hivyo hataki kusherehekea. Nilimuelewa, na kuna wakati nilihisi vibaya kumwambia kuhusu ndoa wakati alikuwa amepoteza mtoto. Nilimuomba msamaha na mambo yakaisha.
Baada ya wiki mbili, nasikia mchumba wangu anaolewa. Kuna mwanaume kamvisha pete, nikamuuliza kulikoni. Akanijibu amepata mtu wake hivyo kama ni pesa ya kumsomeshea nimuambie tanilipa. Nilidhani ni utani, lakini hata mama yake aliniambia, "Wewe bado unajitafuta tu, mwanangu ana kazi nzuri, utamrudisha nyuma."
Walifunga ndoa na yule mwanaume, na akawa mke wa pili. Ni mzee mtu mzima, walikutana huko kazini, akiwa na kampuni yake. Inaonekana waliingia kwenye uhusiano baada ya kufanya kazi pamoja kwenye mahesabu. Iliniumiza sana, lakini nilikuja kugundua kuwa hata mimba alitoa kwa sababu mwanaume alimwambia hataki kulea mtoto wa mtu mwingine.
Hapo ndipo nilipompotezea na kuamua kuendelea na maisha yangu. Sikutaka kulipwa chochote, niliendelea na maisha yangu, lakini mpaka sasa bado sijapata nafuu kabisa. Hata hivyo, maisha yanaendelea.
MWISHO