Nilio shuhudia leo, yanasikitisha!

Nilio shuhudia leo, yanasikitisha!

Bakulutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2011
Posts
2,557
Reaction score
1,787
Habari JF,
Ni asubuhi na mapema niko ktk shule moja iliopo manispaa ya temeke, kigamboni Mjimwema, shule ya msingi Mjimwema, shule ilio anzishwa miaka takribani 40 iliopita na bahadhi ya viongozi wakubwa wamesoma hapo.

Naona wanafunzi wamekaa chini kwenye sakafu huku mwl akifundisha kwa bidii kweli!
Nikadhan labda ni mazoezi au ni masomo kw vitendo!
Macho yangu yaka zidi kuwa na hamu kubwa ya kutazama madarasa mengine nayo hivyo hivyo isipokuwa madarasa kama matatu tuu ndio kulikuwa na mchanganyiko wa waliokaa kweny madawat na chini!
Nilishangaa saana kuona hali hii kwenye shule iliopo mjini tena DSM pembezon mwa bahar ya Hindi!!
Ni ajabu lakin ni kweli, sasa je zile shule za kule sitimbi/vijijini ndio inakuaje sasa...?
Kw hali hii kwenye div 4 na 0 zitapungua, kwa nn watu wanaangalia shule za sekondari wana sahau msingi wa elimu uko wap?
Eti tume inachunguza matokeo mabaya..yaani una chunguza mwanafunzi aliengia kidato cha kwanza hajui kuandika jina lake!! Unatarajia atafaulu form4...
Tutarajie sinema na epsod za kutosha kwenye matokeo yajayo!!
Sikuweza kuweka picha wadau coz natumia ka nokia ka tochi!
 
80% ya viongozi wetu wako madarakani kwa interests zao na si kwa interests za nchi, za kuisaidia jamii kuondokana na shida iliyonayo. Karne 21 ni karne yenye changamoto nyingi sana, lakini sisi kama taifa hatuna sehemu ya kuegemea wala hatuna cha kujivunia zaidi ya kuendelea kukumbatia misaada. Madawati, meza, viti, and the likes ni vitu vinavyoweza kutengenezwa kwenye magereza yetu vikaenea kila shule.
Tuna rasilimali watu nyingi ambayo huzeeka bila kulifanyia kitu taifa hili, hatuna viongozi wenye kubuni mikakati wa kutatua matatizo ya nchi yakawa historia bali viongozi wanatumia mwanya wa hayo matatizo kujinufaisha. Ndiyo maana tunapiga kelele tubadili chama tawala ili wajifunze. Watakaoingia nao wakichemsha, tunabadili mwisho wa siku tutapata kitu kizuri.
 
Halafu baada ya kuona hayo na kulalamika, bado hutapiga kura 2015..
matatizo yetu sisi tunajiletea wenyewe...hakuna sababu ya kulalamika.
Nchi inawezaje kuwa na watu milioni 23 waliojiandikisha kupiga kura halafu wanaotokea vituoni ni milion 8 tu?!?
..hizi ndizo dividends za uvivu wetu wa kupiga kura.
 
sio siri,kweli Tz ni ajabu la dunian ...
yaaan watu wanasimama majukwaani na kujitapa kwamambo meengi..
hamna kitu yaaani miaka 50 ya uhuru shule ya mjini kama hii... na sio hii tuu nadhan ni nyingi saana..
TUBADILIKE WA TZ KUANZIA MTOTO MWENYE UPEO MPAKA MZEE..
sasa tuzidi kushuhudia wimbi kubwa la vijana mtaani hawana kazi, elimu feki ndio maisha yatapendeza nadhani...
 
sio siri,kweli Tz ni ajabu la dunian ...
yaaan watu wanasimama majukwaani na kujitapa kwamambo meengi..
hamna kitu yaaani miaka 50 ya uhuru shule ya mjini kama hii... na sio hii tuu nadhan ni nyingi saana..
TUBADILIKE WA TZ KUANZIA MTOTO MWENYE UPEO MPAKA MZEE..
sasa tuzidi kushuhudia wimbi kubwa la vijana mtaani hawana kazi, elimu feki ndio maisha yatapendeza nadhani...
Hapo ni kukabana roba kwenda mbele, ukichukua mshahara leo, ujue si wako, ni wa watu kama 20 hivi. ukisikiliza sababu zao, unaweza kukimbia nchi.
 
Sasa ni kweli kabisa serikali ina upande wake wa lawama, hili la madawati kweli ni serikali nayo ndio ilete jamani? Kamati za shule zina kazi gani? bodi ya shule nayo? misitu yote hii, mi nasema watanzania tunahitaji kwanza ukombozi wa fikra zetu kabla ya ukombozi mwingine wowote ule, sisi ndio tunachakachua hela za ujenzi wa shule za kata, tunatoroka maofisini tunaenda kwenye dili zetu. hata kama serikali ni mbovu basi unahaki ya kuiwajibisha kwenye sanduku la kura lakini wewe je, umetimiza wajibu wako?
 
Habari JF,
Ni asubuhi na mapema niko ktk shule moja iliopo manispaa ya temeke, kigamboni Mjimwema, shule ya msingi Mjimwema, shule ilio anzishwa miaka takribani 40 iliopita na bahadhi ya viongozi wakubwa wamesoma hapo.

Naona wanafunzi wamekaa chini kwenye sakafu huku mwl akifundisha kwa bidii kweli!
Nikadhan labda ni mazoezi au ni masomo kw vitendo!
Macho yangu yaka zidi kuwa na hamu kubwa ya kutazama madarasa mengine nayo hivyo hivyo isipokuwa madarasa kama matatu tuu ndio kulikuwa na mchanganyiko wa waliokaa kweny madawat na chini!
Nilishangaa saana kuona hali hii kwenye shule iliopo mjini tena DSM pembezon mwa bahar ya Hindi!!
Ni ajabu lakin ni kweli, sasa je zile shule za kule sitimbi/vijijini ndio inakuaje sasa...?
Kw hali hii kwenye div 4 na 0 zitapungua, kwa nn watu wanaangalia shule za sekondari wana sahau msingi wa elimu uko wap?
Eti tume inachunguza matokeo mabaya..yaani una chunguza mwanafunzi aliengia kidato cha kwanza hajui kuandika jina lake!! Unatarajia atafaulu form4...
Tutarajie sinema na epsod za kutosha kwenye matokeo yajayo!!
Sikuweza kuweka picha wadau coz natumia ka nokia ka tochi!


Siku nyingine chukua picha maana hiyo huweza kupunguza kuwa na wasi wasi na habari za kizushi

Maisha bora kwa kila Mwanamtandao
 
sasa wasipounda tume watakula wapi, watahalalisha vipi posho wanazolipana?
 
Sasa ni kweli kabisa serikali ina upande wake wa lawama, hili la madawati kweli ni serikali nayo ndio ilete jamani? Kamati za shule zina kazi gani? bodi ya shule nayo? misitu yote hii, mi nasema watanzania tunahitaji kwanza ukombozi wa fikra zetu kabla ya ukombozi mwingine wowote ule, sisi ndio tunachakachua hela za ujenzi wa shule za kata, tunatoroka maofisini tunaenda kwenye dili zetu. hata kama serikali ni mbovu basi unahaki ya kuiwajibisha kwenye sanduku la kura lakini wewe je, umetimiza wajibu wako?
Inategemeana una define vipi serikali. Hizo shule zipo chini ya serikali za mitaa (halmashauri) na ni wajibu wa halmashauri kuhakikisha shule zake zinapata huduma zote zinazostahili. Sasa kama halmashauri hazijatekeleza wajibu wake, ilihali mkurugenzi wa halmashauri anateuliwa na Rais, kumbe alaumiwe nani? Kama si serikali tena kuanzia Rais aliyeteua Mkurugenzi asiyejua wajibu wake na bado hawezi kumwajibisha?

Unasema misitu yote hii? Dar es salaam kuna misitu wapi, ambayo unaweza tu kwenda kukata ukachana mbao na kutengeneza madawati? Najua vijijini tatizo la madawati si kubwa kama hapa Dar, kwa kuwa kule kijijini kwetu kwa mfano, kila balozi huwa anapewa kazi ya kutengeneza angalau dawati moja kila mwaka. Kwa hiyo kila mwaka kuna replacement ya madawati kwenye shule yetu ya kijiji. Hata nyumba za walimu zinajengwa na wananchi ambao wanafyatua tofali wenyewe na kujenga. Sijui huku mijini kama haya yanawezekana.

Unaongelea juu ya uchakachuaji wa hela za ujenzi wa shule. Je ulishajiuliza kama huwa zinachakachuliwa na nani? Hao wanaochakachua hela za ujenzi wa shule ni sehemu ya serikali. Na hela ya ujenzi wa shule haichakachuliwi na wanakijiji, bali viongozi wa halmashauri. Sasa utajiuliza serikali ya CCM inao ubavu wa kuwachukulia hatua wachakachuaji hawa?
 
Ngoja nimkumbushe mbunge wangu akatembelee shule zote za msingi jimboni kwake asije 2015 akaangukia pua.
 
Serikali ya ccm imeunda baraza la mawaziri kwa manufaa ya ufisadi na ukada wa kimtandao na matokeo yake maendeleo yamefanywa propaganda ila in real sense watu wanataabika na wananunuliwa kwa hizo taabu zao alafu wanazidi kuzalisha jamii ya maskini wa mawazo na kuzoea taabu kama vile ni haki yao juu ya dhamana ya serikali aliyoiweka madarakani.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Nmesoma hapo darasa la kwanza mpk la nne

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
peleka basi hata madawati mawili, au kwanini usitafute jamaa uliosoma nao hapo muone mnawezaje kuisaidia shule yenu?
 
Back
Top Bottom