Niliposikia mchumba wangu niliyempenda sana kaolewa, nguvu ziliniisha

Niliposikia mchumba wangu niliyempenda sana kaolewa, nguvu ziliniisha

Nikifa MkeWangu Asiolewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
6,944
Reaction score
14,351
Kwenye ujana una mambo yake.

Nahisi sio Kwa wanaume pekee la hasha yamkini hata wanawake Huwa Kuta hili.

Niliwahi kuwa na mahusiano na binti mmoja Hivi wakitusi. Huyu dada nilikuwa namzidi miaka5-6 Hivi.

Kipindi hicho nikiwa nimeamimiwa na boss mmoja kuwa agent wa sigara na vocha. Na nilkuwa nalipwa 70k tu Kwa mwezi.

Huyu binti alikuwa anauza maziwa mgando jioni yeye na mama yake.
Wote walikuwa na umbo zuri warefu wenye weusi kiasi. Kwa upande wa binti Sasa hapo usiseme Kila sifa alikuwa nazo za kuitwa mwanamke mzuri. Kifuani chuchu saa6 mubashara wa kushangaza kabisa ulionekana.

Kwa sababu nilkuwa agent hivyo marafiki zangu walikuwa wafanyabiashara wakubwa wakubwa wengi wenye pesa zao.

Siku Moja nikiwa jamaa yangu mfanyabiashara wa sigara mkubwa tu nikamwambia Kuna maziwa huku uwe unakuja nunulia huku asee..

Katika kumwambia vile akaniambia Kuna mama Mmoja na binti yake wanauzaga maziwa mazuri sana lakini nina muda Sasa sinunui kwao kisa yule Binti nili mtongoza akachomoa.

Nikamwambia ndo hapo hapo wale ndo wateja wangu Mimi.
Nikamuuliza kwanini Sasa hununui hapo akasema Kila nilikimuona naumia sana nishawahi muwekea 200k akaikataa na kunambia kuanzia Leo ni mkome kabisa.

Basi tukawa tumefika pale yule mama akamjua yule jamaa akamuulizia habar za siku na kwanini hachukui maziwa Yao Tena.

Jamaa akajitetea then akachukua na Mimi. Nikachukua tukaagana na msela.

Pia story za Wana kijiweni walikuwa wanasema yule demu ni mgumu sana asee atakae muoa huyo kapata mke kabisa.

Kwa maneno hayo yalinipa nguvu na morali ya kumdadisi zaidi yule Binti.

Kwanza nilikuwa na mother wangu mwenye nyumba nilimwambia aniangalizie binti wa kuoa. Yule mama nae hata haikuchukua sekunde akamtaja yule Binti ijapo kuwa nae alikuwa na mabinti japo walikuwa wanasoma chuo mwaka wa mwisho.

Nilishangaa Sana. Nikamuuliza kwanini mama umtaje huyo na siyo Rachel?
Akasema hiyo familia naijua sana Mimi. Ni familia yenye msimamo mkali sana hata dada zake hakuna aliyeachika pia ni familia yenye hofu ya Mungu sio baba,mama Wala Watoto wote Wana hofu ya Mungu mno.

Na kama unamtaka umuoe wewe nenda kwao Moja Kwa Moja nipo tiyari kukupeleka.

Ukweli sikuwa na ratiba ya kuoa kabisa kipindi hicho japo nilianza kushawishika sana. Na geto langu lilikuwa la kiaina ijapokuwa pesa nilikuwa napata sana za Nje na mshahara.

Ikumbukwe tofauti na kuwa agent nilikuwa wakala wa bank kadhaa na mitandao ya simu(super agent wa kuweka float) pia nilkuwa na laini ya lipa Kwa mpesa kipindi hicho ilikuwa haichajiwi kitu hata kama Kuna 10k unaitoa yote halafu Mimi ndo na mkata mteja ninavyoona itafaa.

Wengi huduma ya lipa walikuwa hawaijui kipindi hicho tofauti na Sasa na hii ndo ilinipa Hela sana.

Kwani kuondoka na 250-300k Kwa siku ilikuwa kawaida miamala mingi ya kutoa mpesa nilipitia huko kama siku imegoma kabisa naenda na 80k cash.

Lakini Kwa sababu boss wangu alikuwa akija kupiga hesabu pamoja lazima alale geto langu.

Ukweli geto halikuwa na hadhi na hii nilifanya makusudi Ili boss asisanuke kuwa napiga Hela zake
(Kabila letu tunafahamiana)

Na niliaminiwa sana kwani siku nahamu ya kula kuku nilikuwa naomba Hela kwakwe ananitumia (hapa navunga tu)

Basi ikabidi nianze kununua maziwa kwa mama yake nikawa sinunui kwenye chombo chake maziwa.

Nikifika muda mwingine si msalimii na msalimie mama tu mara nae atanisalimu Kwa heshima kabisa nakupiga goti.


Niliendelea kujikaza hivyohivyo mara nikabadiri upepo.
Kuna siku alikuwa anakuja yeye pekee yake ama mama pekee yake basi nikawa sipiti pale nikitoka ofisini Moja Kwa Moja naenda geto navaa nguo za mazoezi naenda gym.

Nikifika kijiweni kwao (wauza maziwa walikuwa wengi) na mwambia nipelekee maziwa kwangu. Siku ya kwanza haikuwa rahisi kabisa aligoma nikasema sawa. Siku nunua nikaenda gym kesho yake wapo wote na mama yake nikamwambia mama naomba nikamuonyeshe napoishi awe ananipelekea maziwa.

Mama Wala hakuwa na maswali tukaenda bila kuongea nikafika nikamuonyesha geto nikaingia ndani nakurudi nae Hadi Kwa mama then nikaenda zoezi.

Kweli akawa analeta na Hela nilimwambia awe anachukua chini ya kitabu fln (Think big) na nilikuwa na mtindo Kila nikienda bank lazima niombe Hela mpya kabisa noti za Elfu 1 hata laki2 hizi ni Kwa matumizi ya geto tu.

Hivyo yule Binti akanizoea kama kaka yake. Siku Moja maziwa akaleta mama yake nikiwepo kwangu ulikuwa mtihani kumwigiza geto na Bahati mbaya mvua kubwa ilikuwa imenyesha Nje palikuwa hapakaliki na sikuwa hata na kiti mle geto yani labda ukae kitandani nacho ni chini kabisa sakafuni(godoro juu ya sakafuni)

Ikabidi nimkaribishe mama. Nilikuwa kijana msafi japo kitanda ni Cha chini lkn mpangilio ulikuwa vizuri sana. Mashuka mazuri na unyunyu kiasi.

Mama alipofika nikamwambia mama karibu ukae hapa ni Kwa mwanao kabisa usijari mama karibu akagoma akachukua dumu akakalia lile.

Akaniambia mwanangu Nina mazungumzo nawewe kidogo.
Nikamwambia mama karibu nakusikiliza yamkini mapigo ya moyo yalienda mbio mnoo asee ....

Badae nikajikaza kiume naye akaendelea kuongea.

Wazazi wako wanaishi wapi na huku unajishughulisha na nini? Nilimjibu Kwa ufasaha sana na Kisha nikamwambia nasimia tu ofisi ya boss wangu.

Baada ya hapo akaniambia mwanangu nilikuwa na shida Moja unisaidie nikajibu shida ipi mama yangu?

Mama:- Ni kuhusu dada Yako huyu p nahitaji ajifunze hata kushona cherehani Kwa muda akijua nimnunulie maana Hadi hapo kamaliza form4 na Hana kazi nyingine tofauti na kunisaidia kuuza maziwa.

Mimi:-Mama nimelipokea na nakuhakikishia atapata sehemu nzuri Tena karibu na ofisi yangu kwani Kuna dada yangu hapo Ambae Sasa nimejuana nae amekuwa kama ndg yangu nikamwambia hata weza nikatilia. Nikuombe mama kesho njoo mapema kabula hujafika hapo kijiweni ukifika nipigie simu nikuelekeze uje upaone kwanza ukipapenda ni sawa na hata usipo papenda usiogope tutaangalia sehemu nyingine.

Mama:- Ahsantee kijana wangu kesho nitafanya hivyo nitakuja asubuhi Ili badae nirudi nyumbani kwani asubuhi nitakuwa na kazi mjini hapa pia Kuna vitu nahemea.

Mimi:-Sawa mama

Akaaga hapo ni kama saa2 kasoro Hivi usiku. Nikamsindikiza Kuna sehemu nilikuwa nakula hapo nikamwambia mama samahani unajua Mimi naishi mwenyewe Huwa napika mara1 Moja hivyo naomba tupate chakula hapa.

Alikataa Nami nikamsihi sana Hadi akakubali. Mhudumu alikuja nikamwambia amsikilize mama anachotaka kula amhudumie naye akafanya hivyo.

Baada ya kumaliza kula wote nikanunua samaki wa kuchoma sato mkubwa nikafungiwa na kachumbari na mazaga mengine nikaweka kwenye mfuko kuelekea kijiweni tukiwa na mama.

Tulipofika nikaanza kumtania P vipi unataka kulia ulijua mama amepotea kabisa etii.Akasema Wala hata maziwa yamebaki chupa tatu nilikuwa nataka nimpigie simu nimuulize Yuko wapi mwenzangu akasema Hana Salio.

Nikampa yule samaki nikamwambia dada yangu sisi na mama tumekula nawewe chakula hiki hapa tumekubebea ule. Akauliza Sasa huko nani kapika Sasa hata sufuria sijawahi ona.

Nikajibu sufuria Huwa Unakuta yameenda kutembea tu ila yapo. Nikaaga nikaondoka mida kama saa3 hivi.Mida sio mrefu mama akapiga simu. Nilipopokea ni sauti ya P anashukuru Kwa chakula.

Usiku huu ulikuwa wa aina yake sana kwangu sio Raha Ile Yani nilijiwekea 95 % za kumnasa yule Binti. Japo sikuwa na wazo la kuoa lkn niliadhimu nitaigiza kama muoaji. Na safari ya kumpenda ILIANZIA hapa baada mama yake kuonyesha ananikubali Kwa kiasi hiki.

Kesho yake Kwa dada mwenye cherehani alikuwa na cherehani3 Moja anatumia yeye na nyingine walikuwa wanatumia wasichana wengine2 wa makamo Hawa walikuwa ni mafundi Tyr maana alikuwa anawaita Pindi anapokuwa na nguo za wateja wengi ama anadili la kushona sare. Nje na cherehani hapohapo alikuwa na duka la vitambaa na vitenge.

Baada ya kutoka bank mida ya3 nikamuita yule dada. Alikuwa ananikubali sana kupitia katoto kake kadogo umri kama miezi 7+ Hivi mara nyingi Kila akifika lazima aniachie pale ofisini maana frem zetu zilikuwa zinapakana tu.

Hivyo kupitia huyu dogo dada alinipenda sana tukawa kitu kimoja hata Mme wake pia.

Nilimueleza A to Z yeye akasema Hawa mabinti nimekuwa nao wengi sana wanakuja Kwa upole lakini akijua kazi hata Mme anakuchukulia aliposema sema vile na yule binti alivyo mzuri nikasema hapa Tyr nimekoswa nafasi.

Nikamwambia hapana dada huyu binti namjua siku nyingi hawezi fanya hivyo halafu siku zote Mimi nipo hapa changamoto yoyote si utaniambia akibadirika utaniambia tunachukua maamzi papo hapo.

Dada alinielewa akasema kwakuwa niwewe Wala Haina shida lakini kabla ya kuja aje kwanza mama yake hapa nifahamiane naye nimwambie na gharama japo kidogo nikasema sawa Haina shida.

Muda huo tunaongea mara wateja waje tunasitisha mazungumzo wakitoka wanakuja wengine hivyohivyo alinivumilia Hadi tukamaliza mazungumzo yetu.

Kwenye saa5 simu ya mama ikapiga nikapokea nikamwuliza sehemu alipo akaniambia nilikuwa na boda wangu nikampa location akamchukue chap na kumleta.

Boda hakuchelewa akawaleta Hadi ofisini wakanikuta nikiwa busy na miamala ya Hela za watu maburugutu ya pesa machine ya kuhesabu Hela za watu inalia tu kama Haina wazazi. Baada ya Salam nikapiga simu Kwa mdada wa mgahawa aje chap alipofika tu nikamwambia wachukue wageni wangu ukawahudumie chochote wanachotaka wakimaliza kula uwalete Hadi hapa unikabidhi

Hapa mama alikuja na binti yake Moja Kwa Moja. Japo awali hakusema.

Muda sio mrefu yule dada akawaleta nikampigia simu dada wa cherehani japo ni jirani ila Mimi nisingetoka Kwa muda huo.

Alipokuja tu nikamwambia dada nimeshakueleza wageni wangu ndio Hawa nipo busy naomba uwapokee. Mama ndo huyu hapa Kila kitu Kiko sawa naomba mkute mpo nae mkimaliza muje.

Walikaa hapo kama lisaa wakaja wakanishukuru sana mama akasema amesema hata kesho tu aje Sasa kesho hata kuja ni sabato nae jpili kasema hafungui hivyo atakuja jtatu ahsantee sana mwanangu uendelee na moyo huu. Nikawapa 10k wakaondoka.

Yule dada wa cherehani tumuite joy. Akaja anacheka wewe Alex ndio maana ulikuwa unashadadia kumbe dada mrembo Hivi hapa lazima unambie Nini kinaendelea wewe na huyu binti. Nikamwambia hamna kitu akaenda huku akimwacha mtoto wake kwangu.

NIFUPISHE.

P. Alianza kuja kweli kushona huku dada joy akiniuliza Nami namwambia hamna kitu akasema kama naogopa kumwambia amwambie yeye kuwa nampenda. Nikamwambia acha tu tumsome kwanza tabia.

Siku ziliendelea kwenda kama mwezi muda huo maziwa naletewa Bure na mayai ya kanga mara mahindi hata nyama za mbuzi zilizo banikwa. Nanilimpa ufunguo wa geto kabisa.Na hawataki Hela Tena.

Siku Moja nikajitungua nilimwambia Leo anisubiri twende wote Kwa mama nikamsalimie huko kijiweni. Basi tukiwa njiani nilimuomba tukae kwenye mgahawa fln na kumweleza hisia zangu zote bila kuficha Wala kupepesa macho.

P. Badala anijibu alianza kulia tu machozi yakawa mengi mno nikajitahidi kumfuta na kumwambia Nini kina mliza Sasa Si kama hanitaki aniambie tu nimekosea kumwambia kusudi langu?

Nikaona hapa nimeharibu Kila kitu kabisa. Nikanyamaza kama dk2 then nikamwambia twende Kwa mama Sasa. Bado tu analia nikawaza au nimuache hapa hapa maana Tyr nimesha yakanyaga hapa Sina changu Tena.

Badae kama dk7 akaniambia utaamini nitakacho kuambia nikajibu ndio nitaamini.

P. Akasema Mimi tiyari nimeshachumbiwa na mahali ishatolewa ikabaki kidogo tu. Na mchumba wangu ndo aliyesema nitafutiwe sehemu ya kujifunza cherehani Ili akinioa akanifungulie duka la vitambaa niwe na shona. Kwani mama hajakuambia?

Muda huo Nami machozi yamehamia kwangu asee 😂 🙌🙌
Nikapozi kidogo nikamwambia mama hajaniambia ukumbuke tumeagiza soda tu pale na hazipandi yaani soda naiona kama juice ya pilipili tu.

Nikamuuliza unanipenda akajibu Alex nakupenda sana wewe ni kijana wa mfano sana hata mama haishi kukutaja yani lakini tutafanyaje na Mimi nishatolea mahali?

Nikamwambia kwani mahali ni sh ngapi? Mbona ninauwezo wa kutoa mahali zaidi ya mara2 ya pesa aliyotoa huyo jamaa?

P:-Hata kama mzee wangu namjua hawezi kukubaliana. Nikamwambia sawa muda umeenda twende Kwa mama akikuuliza mwambie tulikuwa na kazi dada alinipa nimshikie mtoto. Halafu Mimi sitafika Kwa mama asije hisi kitu.


Siku hiyo sikulala asee nawaza huyu mama aliniona Mimi boya kiasi hiki nihangaikie mke wa mtu kumtafutia sehemu ya kushona Mimi?

Nikajipa moyo kuwa Kwa sababu amekiri ananipenda Wacha nione na amesema ndoa Hadi mwakani kiangazi na saivi ndo kwanza mwezi wa11 huyu atabadiri tu maamzi.

DADA YAKE NA P KAUGULIWA WATOTO WAKE MAPACHA NA KULAZWA WOTE HOSPITAL

Muda huu Sasa nilikuwa nawasiliana na p kupitia simu ya mama yake bila shida kabisa maana mama mtu aliniamini mno.

P:-Akaniambia ameombwa na dada yake aende kwakwe awe anampelekea chakula hospital na pia kubaki na watoto wengine nyumbani. Nikampa pole ila akaniambia angependa awe anaenda na Mimi kupeleka chakula jioni saa1 nikamwambia sawa Haina shida.


Kweli nikifunga Ile jioni naenda oga nampitia Kwa dada ake tunapanda bajaji tunaenda kupeleka msosi wa wagonjwa

Muda huo yule dada alinijua kama Doctor maana nilikuwa navaa koti jeupe la suti nikifika na salimia wale watoto wake na muulizia wanaendeleaje na muaga naenda kitandan kingine hivyohivyo Hadi napotea naenda kumsubilia Nje p wangu.

Hapa nilikuwa natangulia Mimi kuingia ama p kama dk3 ndo anaingia Mimi naweza azia kitanda kingine kujulia Hali wagonjwa wangu nk.(Mbinu za kivita)

Huku Nako nikajizolea sifa lukuki wakisema yule doctor anaulizia vizuri jamani sijui yupo wodi ipi tu mkaka huyu yaani anakuuliza amekula kiasi Gani Leo vipi lakini unavyomuona kwakweli huyu Dr ni mpole sana.😹😹

Sifa hizi alikuwa ananiambia P mwenyewe maana nilipewa masharti kuwa mama na ndg zake hawatakiwi kujua chochote kitu kinachoenedelea kati yetu hata dada Joy(wa cherehani) maana iwapo wakijua tu tutaharibu.

Kipindi hiki P kashasomeka vibaya mno kasoro mzagamuo tu maana aliniambia hajawahi ku do!

Dada yake p aliagwa hospital Mimi nikiwa namjua vilivyo hata kama tukutane gizani namtambua tu.

Tuliendelea kuwa na P kama wapenzi bila tendo kama miezi2 mbele. Huku akiwa anaenda geto kufua muda mwingine kulala kama amechoka anaweza mwambia dada joy nimekuja kuaga Leo naumwa anaenda kulala ama kufua nguo zangu.

Siku Moja aliniambia anaenda kulala nikamuruhusu ila badae nikajiuliza nitakuwa mjinga Hadi lini huyu P nitamkula lini asee Leo hapana. Pale ofisini tulikuwa wa3 nikagawa majukumu wakadai madeni Mimi niende bank lengo tu nikitoka bank niwahi geto nikapige kipochi manyoya.

Kweli kwenye saa7 nikaenda bank sikukuta foreni hata nikahudumiwa chap nikaenda geto.

Nikagonga akafungua akauliza vipi Leo umewahi nikamwambia nimeijia card yangu ya bank.

Nikapiga blah blah za hapa na pale then nikamkumbatia nikaanza romance kama dk25 nishamvua kabisa Kila kitu naona..nilifanya yangu yote nikafeli nikavaa nikaenda dukani. Yeye alidai mchana anaogopa Hadi usiku na usiku ndo kama hivyo chance haipo.

Siku Moja alienda Kwa dada yake kama kawaida alipofika tu akaniambia Leo jioni nakuja kwako uwahi kutoka Sasa.

Nilikuwa na furaha mno mambo yote nikayaweka sawa ikiwa pamoja na kuweka Hela zote bank na kubakiza Kwa ajiri ya wezi(majambazi) wakija kuiba angalau niwape hata laki8 huku nikiwambia Hela Sina ndo nilicho ambiwa na boss wangu kuwa lazima ubakize Hela si zaidi ya m2 za tahadhari ukivamiwa wape jamaa.

Muda ulipofikia akanipigia akasema ndo natoka Kwa dada Sasa. Nikamwambia jamaa zangu wakuu Mimi Leo sipo sawa twendeni tukapumzike kesho nayo siku.

Tukafunga hesabu ya siku tukaondoka Kila mmoja kivyake.
Nikapita sokoni nikanunua kuku na mahitaji mengine mengi Ili nipikiwe ndo ni mle vzr.

Tulipika Kwa pamoja Wakati huo Nina ka ges kadogo hatukuchelewa kwenye saa1 kilakitu kimeiva maana wali ulipikwa Kwa jiko la mkaa.

Shughuli ikaanza muda huo huo ya kuvunja Yai wapi vunja vunja nawewe Hadi nikachoka Sasa nikavunga kulala nayeye akalala kwenye saa5 nikamuasha nikamwambia kama hanipi asepe tu hii Ina maana umemtunzia jamaa kumbe Mimi unaupendo fake kwangu alilia wee akisema ni mvumilie hajawahi vunjiwa Yai lake nikamwambia hapa nikujikaza tu hakuna namna nyingine ajikaze tu.

Kweli tukaanza Tena Hadi kufanikiwa japo Kwa mbinde sana alilia Hadi nikamuhurumia mno na akaonyesha hanipendi Tena Kwa nilicho mfanyia.

Kwa vile Mimi Haikuwa mara ya kwanza kuvunja nikajisea moyoni utajikoki na mepema kabla hujaenda itaombwa tu.

Tulilala na mapema ikapigwa tukaenda oga wote then tukaelekea site na yeye kushona muda huo kashajua jua Kushona kiasi

Tukiwa njiani akasema niende kwanza nyumbani maana wazee wangu Jana walienda msibani kulala huko. Akaenda Nami nikaenda kufungua ofisi.

Nilisubiri atarudi hakurudi siku ya kwanza ya pili kimya yule dada joy akaja akaniamba vipi Tena huyu P haji ama una taarifa zake? Nikamwambia hapana Sina taarifa zake mpigie simu si una no ya mamake akasema Sina dk lete simu Yako nimpigie.

Akapiga na mama akapokea simu huku ikiwa loud 🔊 📢

Joy:-Mbona siku ya2 hii simuoni mwanangu anachangamoto Gani?

Mama:-Mwenzangu alikuwa amechumbiwa huyo kesho anaijiwa na mmewe!!

Joy:-Mbona kimya Hivi jamani Kuna kitu nimewakosea labda?

Mama:-hapana kuwa na amani nitakuja hapo nitakuambia kwanini imekuwa Hivi hata maandalizi ya maana hayapo yaani Hawa mabinti zetu .simu ikakatwa.

Dada joy akasema uwiiii Alex nilikuambia ukajifanya huyo Sasa mrembo kaenda !!

Taarifa hizi zilinifanya nikoswe Cha kuzungumza Kwa muda nikamuita jamaa yangu aliyekuwa store ya sigara aje chapu. Nikamwambia naumwa kichwa hatari muda huo dada joy nae yupo kwakwe kwanza.jamaa alipokuja nikamwambia panga hizi Hela vzr jamaa then ukimaliza niite nipo Kwa dada joy hapa akija mteja mwambie masalio yameisha.akitoa pokea mpe cash.

Nilipofika Kwa dada Joy ikabidi nifungukuke yote akaniambia kwanini ulinificha Sasa Mimi P niliwahi mwambia akasema hata yeye anakupenda Kwa vile sikuona hu kumshobokea nikajua labda humpendi!

Baada kumweleza na kukiri na mpenda sana sijui shida Nini lkn nakuomba twende Kwa dada yake Ili kama Mimi ndo nimeleteleza Kwa namna Moja ama nyingine nipo Tyr kutoa mahali hata mara mbili.

Dada joy akasema twende wewe ni ndgu yangu Dada joy alikuwa na kipawa Cha kuongea haswa!

Tukafunga na nikamuamlu jamaa apeleke Hela bank ilikuwa saa9 alasiri. Jamaa akapelekwa na sisi tukaondoka nikamwambia naenda hospital nikapime. Simu nikazima zote kwanza.

Tukafika Kwa dada yake p na kugonga hodi getini akafungua aliponiona akanikumbuka akaniita Dr karibu akatoa kiti tukakaa.Dada jou akaniuliza umekuwa doctor Tena na mnafahamiana?

Nikamwambia Endelea muda huo dada yake p kadakia ni Dr wangu huyu namjua tangu muda sana.

Dada Joy Akacheka akasema mdogo wangu tukiachana na hayo Mimi hapa sikufahamu na wewe hunifahamu bila shaka akajibu ndio.

Dada joy:-Mimi ndo nilkuwa na mdogo wetu p katika ushonaji.

Dadake P :-ooooh kumbe ndo wewe taarifa ninazo kumbe alikuwa kwako ...yeye ndio.

Joy:- huyu kijana kama una mfahamu Kuwa ni Dr Mimi sijui Hilo ila ndo aliye mleta kwangu Nami nikampokea kupitia huyu.

Sasa Kwa mengine yote yaliyotuleta hapa naomba yeye ni mtu mzima ajieleze zaidi.

Mimi :-Dada kwanza samahani Mimi sikuwa Dr Wala Sina chembechembe yoyote ya kuwa Dr.

Kipindi nakuja pale nilipewa taarifa na mdogo wako kuwa umeuguliwa Watoto Nami nikaona sio kosa kuja kuwaona na nilifanya hivyo Kila siku.

Dada kilichonileta hapa nikutaka kujua ni Nini kinaendelea kuhusu P maana mama kasema Hivi na hili ndo limetufikisha hapa.


Dadake P :-Mmmhhhh Hadi mmesnishitua kwani kafanyaje P ? Tukamjibi hamna kitu kafanya.

Nikamwambia kuwa labda nisikufiche kitu hapa. Nimekuwa kwenye mahusiano na P Kwa miezi kadhaa Sasa na juzi alilala kwangu asubhi anaenda nyumbani akaniaga akasema aende nyumbani kwanza akawaone then atarudi kushona ndo ikawa mwisho Hadi tulipoongea na mama akasema kuwa anaolewa!

Dadake P:-Ukweli ni Hivi. Juzi hiyo asubuhi nilipigiwa simu na baba simu haikuwa karibu hivyo sikupokea baada ya kuja kuona nimetafutwa na mzee nikampigia mzee. Mzee akaniuliza mdogo wako P kalala kwako? Nami nikajibu hapana hajalala kwangu nikauliza kulikoni kwani mzee?

Mzee akajibu mdogo wako tulimuacha nyumbani sisi tukaenda msibani japo alikuwa ametuaga kuwa atakuja kwako lakini kilichotushitua ni yeye kufika saa2 asubhi ndo tukapata mashaka ya kukuliza wewe.

Dadake P:-Hapana mzee yeye kasema kalala wapi? Mzee kasema kalala kwako!
Dadake P:-Hapana.

Dadake P:-Haya ndo yalikuwa mazungumzo yangu na mzee Sasa ikabidi nimpigie mama.
Mama alipomuuliza P kuwa amelala wapi akasema alilia Kwa mkaka muuza vocha na wakala!

Mama akawa anakujua vizuri tu na mpaka sasa mama aliambiwa P asitoke getini Wala Asipewe simu na baada ya hapo mzee alipiga simu Kwa mchumba wake akamwabia amuijie kama mahali atamalizia badae. Ndo wakasema kesho wanamuijia na Mimi kesho naenda kumuaga japo ni ghafla sana.

Akaniuliza kumbe ulikuwa wewe? Kwanini hukuwa muwazi Sasa hata kwangu tu?. Nikamwambia P alinikataza mno akisema yoyote akijua ndo itakuwa mwisho. Akajibu kwangu Mimi hata kumtorosha ningehusika kabisa mi nakujua tangu pale hospital na Mme wangu akawa ananiambia Dr namuona snaa bank atakuwa mfanyabiashara mkubwa yule.

Aisee nimeumia na kukuhurumia sana.

Dada joy:- Tumekuja hapa na mdogo wangu Kwa nafasi ya mwisho kama ipo kwamba wewe ufanye lolote atoroke na hii inamanisha mdogo wangu alikuwa na nia thabiti ya kuwa na mdogo wenu sio kumchezea.

Dadake P :- shida ipo Kwa baba yaani mzee atanilaani kabisa mzee dini ishaingia mno hawezi kukubali hata kupokea mahali yake afadhari kipindi akiwa huru ilikuwa rahisi.

Nikuombe tu kaka yangu mdogo wangu haikuwa riziki Yako pole sana umeshachelewa!!!

Tulimsihi sana lkn hatukufanikiwa tukaaga tukaondoka. Kama tumenyeshewa na mvua yenye baridi Kali mno. Usiku sikula.

Kesho yake nikaenda dukani lakni mambo yakawa sivyo nikapiga simu Kwa boss nikamwambia naumwa sana boss akaniambia kama Hali ni mbaya funga ofisi umwambie mwenzio mmoja akulete huku. Nikamwambia acha tuone Leo Jana nilipewa dawa japo hata malaria Sina!


Akasema sawa kapumzike na Kila kitu unijurishe na hakikisha upo na fln muda wote akikupa msaada nikamwambia poa Haina shida. Tukafunga ofisi nikazima simu maana simu ikiwa hewani wateja walikuwa wanasumbua sana.

Inaendelea...

FB_IMG_1714568039005.jpg
 
Inaendelea.......

Jamaa nilimwambia wee nenda misele tu akikupigia mwambia Nimelala.

Nilipitia Wakati ngumu sana kuwahi kutokea na kujiona kumbe Sina thamani kiasi. Pamoja na yote haya mama kakubalije P aende? Nilijaribu kulala usingizi hata hauji hukuna huko lakini wapi.


Basi nikatulia tu muda huo nilikuwa sinywi hata pombe hata wazo halikunijia kwamba nikanywe pombe nitoe haya mawazo yaani naichukia hata kazi yangu.

Nilikuwa na demu wangu kipindi hicho pia tukiachana na p nae nilkuwa na mkubali kiaina sema yeye sikuwahi muonyesha napo ishi.

Kwa siku hizi mbili nilikuwa sijibu hata rxt zake kabisa akipiga sipokei. Kitu kilicho mfanya aulizie ninapo ishi aje hapo baada ya kufika ofisini akakuta pamefungwa na haikuwa sio kawaida kufunga ofisi.


Nikiwa Sina hili Wala lile mlango ukagongwa nikajua ndo jamaa sikufungua nikampigia simu kwanza Simu akapokea akasema yupo sehemu fln mbali tu anazurula nikamwambia nipo poa muda huo nae anaitwa Alex vipi wewe sikuelewi nikaenda fungua mlango akaingia Sina furaha kabisa.

Akaniuliza vipi unaumwa? Nikamwambia heri hata kuumwa yaani hapa niache Nina mazito sana.

Kuna Hela ya boss haionekani kama milioni Saba nakaa napiga hesabu Toka juzi sijui imepoteaje 😹😹

Akashituka sana then akasema si atakufunga jamani Hela yote hiyo.
Asee muda huo naona anapiga kelele tu masikioni mwangu. Nikamwambia naomba uniachie na mawazo mazito sana hapa. Kwa vile unapajua ninapoishia Sasa kuwa na amani nikiwa sawa nitakucheki tu.

Alileta ubishi kutoka nikamwambia uliobaki mi nitaenda lala loudge nikuache hapa peke Yako.


Akaondoka kishingo upande huku anatumia txt kibao na sijibu.
Binti huyu nikweli alikuwa ananipenda sawa shida wahuni walikuwa wameshavunja Yai na alikuwa mzuri wa kiasi chake.


Alipotoka likaja wazo niende kule nilkuwa napaki vitu vyangu nilivyokuwa na nunua Ili boss asivione huko alikuwa anaishi mtoto wa mjomba kwahiyo ni binamu yangu Nje kabisa nikiomba chumba kule akanipa.

Kwa muda huo nilkuwa nimenunua mabati 45 futi10
Godoro inchi12
Kitandan kikubwa tu vyombo seti kadhaa na majaba makubwa lita200 3 na vyombo vidogo vidogo vilikuwa humo kwenye majaba.

Mashuka pia nilikuwa na nunua Kila nikilipenda tu nalipia! Hasa Yale ya special. Inshort nilikuwa na geto kamili na P siku Moja niliwahi mpeleka kule kuona hakuamini.


Nilipofika tu nakuona hivyo vitu huku nimenunua samaki sangara mkubwa tu. Baada ya kufika tu Watoto wa binamu wakanipokea shemeji nae akanipokea Kwa furaha ghafla mawazo yaliisha ikabaki Hadi nimuwaze ndo naumia Tena😅😅

Huwa Nina ulevi wa kucheza na watoto hata kama ndo nimefika kwako dk 5 nyingi nimezoeana nao mnoo kama wanapenda kucheza tutcheza hata mziki. Kupitia Watoto Hawa nilijihisi kupona maumivu yangu na kuchukuliwa kawaida na kuanza kujilaumi kwanini sijafungua ofisi.

Nilikula nikawaanga muda huo saa9 alasiri Moja Kwa Moja geto nikachukua funguo za ofisini na Kila kitu mhimu nikabeba begi nikampigia boss nikawa nipo sawa Kwa Sasa nikatoka na oda ya vitu vilivyo pungua hasa Embassy na Winston ndo zilikuwa zimepungua.

Nikafanya mahesabu kadhaa nikaona kazi yangu ni njema. Muda huo nimejifungia tu ndani sitaki buguza na ndo siku P anaenda.

Kalibaki ka harufu fln yamkini Kila mtu anako asee hiyo harufu ilinitesa sana.


Siku hiyo ikapita na kesho yake nikaenda fungua wateja kama niliwashika asee walikuwa wengi mno sio vocha Wala sigara ilikuwa siku ya mauzo mazuri mno Mimi nataniana tu na wateja wangu tuliozoeana nao.

Siku hiyo ikapita pia Kwa uzuri mno.
Kesho yake mapema tu nipo ofisini nimefungua nagawa majukumu Kwa jamaa zangu tu.


Nilipotoka bank mida ya saa4 nikakuta no ngeni imenipigia. Ikumbukwe nilikuwa na simu ya ofisini na simu yangu binafisi hivyo nilipigiwa kwenye no yangu binafisi.

Nikaitafuta Ile no akapokea halafu akakata akiri ikanituma huyu atakuwa p tu siyo mwingine huyu. Muda huo nipo normal tu badae akapiga akakata Tena nikatumia txt "Sikia kama hutaki kuongea namimi naomba usipige simu nipo kazini Sina muda wa kuchezea" then akajibu samahani nimekosea no.

Sikujibu kwenye saa9 Hivi akapiga Tena nikapokea nikamwambia nishakujua nambie za huko?

Akajibu salama naomba unisamahe sana Kwa hili nilicho fanya nikamuuliza ilikuwaaje...?


Akajibu baada kufika home nilimkuta baba na mama wamekaa wakaniuliza ndo unatoka kwa dada Yako bila hata kumsaidia kuosha vyombo kweli? Akasema na wahi kwenda kushona mzee wake akanyanyua simu na kumpigia dadake. Simu haikupokelewa yeye akaingia ndani kubadirisha nguo Ili aje mara baada ya muda akaitwa na mama yake akaambiwa hutakiwi kutoka Nje ya geti kuanzia Sasa na kunambia umelala wapi?

Muda huo mzee wake nae alitoka akaenda mtaani baada kupigiwa na yule dadake kama nilivyosema Ali amru P asiruhusiwe kutoka Nje na akapiga simu Kwa mchumba wake P kuwa amuijiie.


Wakati huu anaongea Nami akiwa tiyari Kwa jamaa ndo kwanza anasiku2 tu. Akasema kama Nia nae kweli yupo Tyr kutoroka hata muda huo nimpeleke kijijini Kwa wazazi wangu hata miezi 2 bila taarifa Kwa maana Bado ananipenda Mimi na kashindwa kunisahau kabisa.

Nikamjibu kweli nakupenda sana na niliumia mno mambo mengi nilipanga nawewe na pia ulikuwa mwanamke mwenye akili ya maisha lakini Sina jinsi zaidi ya na kukubaliana na ukweli kuwa wewe si wangu Tena!


Aliongeza Kwa hisia sana na baada ya kumwambia Mimi si wangu Tena akasema kumbe hukuwa na Nia Nami ya kunipa Alex? Imekwambia nipo Tyr kutoka huku Kwa sababu Yako hapa nahitaji utayari wako tu kwani hayupo ameenda kwenye duka kuuza.


Nikajibu nimekuelewa naomba nikutafute nikitoka kazini akasema sawa Mme wangu anarudi saa2 nitafute kabla ya hapo. Nikasema sawa.


Mawazo yarirudi mwanzo ikabidi nimpigie dada Joy aje nikamwambia akajibu nakuomba achana nae huyo ni mke wa mtu hata kurogwa mtarogwa yeye angekutafta kabla hajaenda ilikuwa afadhari.

Dada joy nilimjibu tu nimekuelewa ila moyo ukigoma kukubaliana naye. Nilimpigia mama mzazi nikamwambia japo nilikuwa sijawahi mwambia kitu hiki nae aligoma mnoo akasema unajitafutia matatizo.

Nilipo funga nikamtafuta tuliongea kama dk40 hataki kuelewa Tena anadai jamaa hajapewa Bado kaambiwa anaumwa.

Nilishikilia msamo nikamwambia sitaweza wewe utabaki kuwa rafiki yangu tu siku zote. Alozila kama siku3 hanitafuti Nami nipo kimyaa vilevile badae akanitafuta lake ni lile lile kuwa sija badirisha tu mawazo nikamjibu ndio.


Basi akipika na kuivisha lazima anikaeibishe Kwa njia simu😅😅niliona huyu P anahangaika sana kipindi hicho Mimi nimezoea kabisa.


Siku zikaenda tunachati tu nikakaribishwa kwakwe. Siku Moja nikaenda muda huo Nami nahitaji kuachana na boss wangu ninitegemee baada ya kuwa na mtaji kiasi kama m9 Hivi Nje na assets nilizokuwa nimenunua.

Nilimwambia P nahitaji kujitegemea Sasa Nami nioe asee. Akasema ukija nitakupa vyombo vingine kama kumbukumbu. Na kweli siku nafika kwakwe alinipokea na akampigia Mme wake kuwa kaka amekuja ila hatachelewa anakuhitaji akuone.

Jamaa kweli hakuchelewa akaja tukala then akasema shemeji nimekuona acha nirudi huku siku nyingine uje Kwa kulala kabisa tutembee hapa mjini akanitoa na 50k


Baada ya jamaa kwenda nilimwambia umekosea sana kumuita atakuwa anakuulizia kuhusu Mimi utamjibu vipi?

Tuliongea mengi nikaaga nakuondoka akanipa set ya hotpot mbili nilimshukuru nikaondoka.


Tuliendelea kuwasiliana badae nikawa sijibu txt zake. Siku Moja akapiga analalamika nikamwambia hapana siwezi kuendelea kuwasiliana na mke wa mtu. Japo Hadi Leo Huwa tunawasiliana na teshaonanaara4 Hadi Leo hii na hatujawahi fanya kitu.


Upande wa mama alikuja Kwa Dada joy na kumwambia yote akawa huyu kijana jamani kwanini alikuwa msiri kiasi hiki. Kwakweli kama angekuwa muwazi nilikuwa tiyari kumruhusu binti yake aolewe nae tu. Nilikuja onana na mama tukaongea mengi huku akinipa pole nyingi tu muda huo Sha zoea kabisa.



Nilitoka huko baada kuagana na boss wangu japo ilikuwa sio rahisi kuniacha. Nikaenda kufanya biashara ya samaki nikafirisika vibaya mno.

Japo assets zangu si kuziuza ila mtaji wangu uliisha wote. Nikawaza kubua dagaa. Nako nikawa mhuni tu nikarudi Kwa wazazi kujipanga almost mwaka.

Vitu vyangu nilivyonunua kipindi kile tiyari nilikuwa nimeshaviweka Kwa kaka yangu wa damu japo sikuvikita vyote hasa vyombo lakni vingine vilikuwa salama kabisa.

Mwisho. Ukiona mwanamke Ambae hujavunja Yai automatically umeoa mke wa mtu na hii haipingwi. Kilicho sababisha nisi mle ni Mimi tu yule p hata Leo Huwa ananikumbushia na Hadi kumuonea wivu wife.yeye Sasa Hivi ana watoto5.
 
Hahahah kwa hiyo ww umemtoa bikra ila ameenda kuolewa na mwanaume mwingine na ana watoto wa 5, Na kipochi kinachapwa kila siku. Wewe unayesena jamaa kaoa mke wa mtu kisa hakumtoa bikra unafaidika nini? U nice guy ndo unakutesa
 
Ujinga gani huo mwanamke unamtolea mahari nusu halafu umamuacha kwao...halafu tambua mke wa mtu sumu...mtoa mada wewe ni miongoni mwa mabaharia...nanyie wazazi ambao mlishachukua mahari kidogo mnapata ujasiri gani huo wa kuwapa uhuru watoto wenu badala ya kuwabana? Huu ni ufedhuli kabisa...mwisho kabisa kabisa, "tunaoa tusiowapenda maana tuliowapenda tuliwakosa"
 
Back
Top Bottom