Nilisema BOT hawana uwezo wa kupambana na ma sharks wa mikopo ya mitandaoni. Riba bado ziko juu, usumbufu upo vilevile

Nilisema BOT hawana uwezo wa kupambana na ma sharks wa mikopo ya mitandaoni. Riba bado ziko juu, usumbufu upo vilevile

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Ni kama mwezi sasa au wiki kadhaa tangu benki kuu ya Tanzania itoe waraka wa kuwataka wakopeshaji wa mitandaoni wanaolalamikiwa kufuata taratibu ikiwa pamoja na kuacha lugha za matusi, kutokusumbua ndugu na jamaa wa mkopaji, kutokusambaza taarifa za mkopaji.

Mimi nilisema hakuna hata kimoja hawa watu watakifuata. Nilijibu waraka wao kwa njia ya maswali yafuatayo;
1. Je, ni BOT ndiyo iliwapa ruhusa kukopesha watu mikopo ya siku 4 mpaka 6 kwa riba ya 40%-50%.

2. Je, ni BOT ndiyo iliwapa ruhusa ya kukusanya namba za phone book ya mteja?

3. Je, ni BOT ndiyo iliwapa ruhusa ya kusumbua mteja na kumdhalilisha katika jamii huyo mkopaji akipitiliza hata siku moja?

Kama waliweza kufanya hayo yote na mengine ambayo ni kinyume cha kanuni na Sheria na hawajachukuliwa hatua je, watautii waraka wa BOT ambao ni toothless?

Umaskini ndio unawafanya Watanzania wawe shamba la bibi. Na viongozi wanapewa Senti na mabepari mchezo unaisha.

Mkopo kwenye fomu unaambiwa ni wiki 2 ukiclick tu kukubali wanaanza kwanza kukukata makato ya hovyo, pia siku ya 4 tu au ya 3 simu zinafuata usipolipa tu umekwisha. Utaundiwa group Whatsapp la kukutukana, kijiji chote kitajulishwa n.k

Soma Pia: BoT yakataza rasmi kampuni za mikopo mitandaoni kuchukua mawasiliano ya wateja ili kuwadhalilisha. Yatoa mwongozo mpya!


Serikali iwakomboe Wananchi. Wana hali ngumu sana. Jana nimepigiwa simu kuna mtu anadaiwa nikamuuliza Mimi kama ni mdhamini wake mbona sijajulishwa kabla hajakopeshwa akasema Mimi sio mdhamini. Sasa kwanini nipigiwe simu kama sio mdhamini jibu analonipa ni upumbavu mtupu.
 
watu wa mikopo wa mitandaoni akili hawana.
Mtu anapopitiliza siku kabla ya kumuandikia meseji za kipumbav. Inatakiwa uende kistaarabu,muulize tatizo nini,na lini atalipa.ila unapoanza kwa vitisho. Wengine machizi kama wewe.anakubadilishia namba tu.hivi kwa maneno kama haya mtu anaweza kukulipa kweli?.sawa tuna kopa kwa shida zetu ndio.ila tukipitiliza siku haimaanishi hatutaki kulipa.jengeni mahusiano mazuri na wateja.alafu mnaweka faini kila siku 1000.ukipitiliza .hii hela mtakwenda kulipwa mahakamani.
 

Attachments

  • Screenshot_20241008_053516_Messages.jpg
    Screenshot_20241008_053516_Messages.jpg
    103 KB · Views: 23
watu wa mikopo wa mitandaoni akili hawana.
Mtu anapopitiliza siku kabla ya kumuandikia meseji za kipumbav. Inatakiwa uende kistaarabu,muulize tatizo nini,na lini atalipa.ila unapoanza kwa vitisho. Wengine machizi kama wewe.anakubadilishia namba tu.hivi kwa maneno kama haya mtu anaweza kukulipa kweli?.sawa tuna kopa kwa shida zetu ndio.ila tukipitiliza siku haimaanishi hatutaki kulipa.jengeni mahusiano mazuri na wateja.alafu mnaweka faini kila siku 1000.ukipitiliza .hii hela mtakwenda kulipwa mahakamani.
Aiseee hao flex nadhani sifa ya kuajiriwa inabidi uwe unajua matusi haswa
 
Ni kama mwezi sasa au wiki kadhaa tangu benki kuu ya Tanzania itoe waraka wa kuwataka wakopeshaji wa mitandaoni wanaolalamikiwa kufuata taratibu ikiwa pamoja na kuacha lugha za matusi, kutokusumbua ndugu na jamaa wa mkopaji, kutokusambaza taarifa za mkopaji.

Mimi nilisema hakuna hata kimoja hawa watu watakifuata. Nilijibu waraka wao kwa njia ya maswali yafuatayo;
1. Je, ni BOT ndiyo iliwapa ruhusa kukopesha watu mikopo ya siku 4 mpaka 6 kwa riba ya 40%-50%.

2. Je, ni BOT ndiyo iliwapa ruhusa ya kukusanya namba za phone book ya mteja?

3. Je, ni BOT ndiyo iliwapa ruhusa ya kusumbua mteja na kumdhalilisha katika jamii huyo mkopaji akipitiliza hata siku moja?

Kama waliweza kufanya hayo yote na mengine ambayo ni kinyume cha kanuni na Sheria na hawajachukuliwa hatua je, watautii waraka wa BOT ambao ni toothless?

Umaskini ndio unawafanya Watanzania wawe shamba la bibi. Na viongozi wanapewa Senti na mabepari mchezo unaisha.

Mkopo kwenye fomu unaambiwa ni wiki 2 ukiclick tu kukubali wanaanza kwanza kukukata makato ya hovyo, pia siku ya 4 tu au ya 3 simu zinafuata usipolipa tu umekwisha. Utaundiwa group Whatsapp la kukutukana, kijiji chote kitajulishwa n.k

Soma Pia: BoT yakataza rasmi kampuni za mikopo mitandaoni kuchukua mawasiliano ya wateja ili kuwadhalilisha. Yatoa mwongozo mpya!

Serikali iwakomboe Wananchi. Wana hali ngumu sana. Jana nimepigiwa simu kuna mtu anadaiwa nikamuuliza Mimi kama ni mdhamini wake mbona sijajulishwa kabla hajakopeshwa akasema Mimi sio mdhamini. Sasa kwanini nipigiwe simu kama sio mdhamini jibu analonipa ni upumbavu mtupu.

RIBA ni ndogo sana, ujanja wanaofanya ni cost ya technology Kuwa juu!

Acha Kuwa mtumwa wa mikopo!
 
Kampuni za mikopo zinatakiwa kusheshimu watu stara zao kwa sababu pamoja na shida za watanzania lakin bado hizi kampuni ndio zinafaidika na mkopo ba wala sio mkopaji kufaidika.

Vijana wengi wanakopa kiholela alafu wanabet so kudhalilishwa na kunyonywa kwa riba kubwa ni haki yao maana ni wapumbavu zaidi ya wakopeshaji.

Shida zipo ila sidhani kama kuna mtu Alishawai fariki kisa hakukopa mtandaoni.

Watanzania tuache kujiendekeza na mikopo ya kiholela mtandaoni

Hii mikopo ilikuwa hakuna zamani je watu walikuwa wanakufa hovyo.???

TAFADHALI BOT KIPENGELE CHA KUDHALILISHWA NDIO KIWE KIPAUMBELE KWA WAKOPAJI AMBAO NI ZERO BRAIN UNAKOPA CHA MTU UKIAMBIWA ULIPE DENI UNAKIMBIA MTANDAONI KULALAMIKA HII SIO SAWA.

NAONA HIKI KIPENGELE NDIO KITAPUNGUZA KASI YA WAKOPAJI MANA TAARIFA ZIKIWAFIKIA NDUGU NA JAMAA KAMA UNADAIWA ELFU 10 UTAKUWA UMEDHALILIKA NA KUACHA KABISA KUKOPA.

tafadhali bot msitoe kipengele hicho ndio dawa yao.!
 
Hawa ni matapeli tu,dalili ya tapeli ni kuwa na namba nyingi kiholela..hizi taasisi unakuta wananamba zaidi ya 20 . TCRA nao wachukue hatua ikiwezekana kufungia hizo Apps mpaka watakapokizi vigezo. BOT wamefeli sana maana walitakiwa baada ya ule waraka watangaze kusitisha huduma kwa ambao hawajakizi with immediate effect. Kuna uzi pia nilielezea hili
 
Back
Top Bottom