Nilitaka Mbowe aendelee lakini !

Nilitaka Mbowe aendelee lakini !

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Heshima sana wanajamvi,

Kila mwanajamvi alijua msimamo wangu sina haja ya kuendeleza ligi uchaguzi umekwisha Lissu na Heche ni washindi.

Nawapongeza Lissu na Team yake ya kampeni kwa kazi kubwa sana.

Nilitaka uongozi wa Mbowe uendele lakini wenye chama waliona ni vyema wakabadilisha uongozi pengine kule kukaa sana kulichangia au hoja za washindani wake ziliwafanya wajumbe waone umuhimu wa kubadilisha uongozi.

Baada ya matokeo ya uchaguzi nilisikitika lakini ghafla najikuta nafurahi tena kwanini nafurahi ?.

Wakati mwingine unaweza kumlaumu mtu kwa mambo yote mabaya bila sababu au hoja za msingi.

Najua mwamba alilaumiwa sana kwa matokeo ya chaguzi zilizopita 2019,2020 na 2024 kwamba ni kiongozi legelege anashirikiana na CCM kuhujumu CDM na nk.

Wengi wetu tuliamini Uchaguzi wa 2019 & 2020 ilikuwa mipango michafu na dhulma ya MWENDAZAKE. Sote tuliamini KUTEKANA &KUTOANA UHAI ilikuwa mipango michafu ya MWENDAZAKE na pengine Mbowe na VIONGOZI wenzake waliamini zile siasa chafu zimekwisha.

Lema & LISSU waliokimbilia ughaibu walirejea nyumbani maana yake walijua nyumbani kumenoga siasa za kutishana,kuuana,kupotezana ZIMEKWISHA.

Uchaguzi wa 2024 umebainisha wazi siasa za wizi wa kura,kuvuruga uchaguzi na mambo mengi machafu hazikuwa siasa za MWENDAZAKE pekee yake bali zilikuwa siasa za mfumo mzima wa watawala. Kupotea kwa viongozi na wanachama wa CDM ni jibu tosha kwamba bado nchi ipo kule kule katika zama za giza.

Bahati mbaya MBOWE kabeba msalaba wote wa uovu wa watawala.Hili lilikuwa wazi kabisa katika kampeni za TEAM LISSU. Kuna wakati walionyesha wazi kabisa hata kupotezwa baadhi ya wanachama MBOWE alihusika au alijua mfano Mzee AlLY Kibao (siasa chafu)

Kwakuwa uchaguzi umekwisha na TEAM LISSU kuibuka washindi ni matarajio yetu kwamba mwelekeo mpya wa chama utaonekana katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika miezi michache kutokea sasa.

Lakini suala kubwa zaidi ni zile propaganda kwamba CDM ni chama cha WACHAGGA zitakuwa zimekwisha kabisa.

NO REFORM NO ELECTION.

Ngongo kwasasa Idodomya.
 
Ngongo, uko spot on. Mimi nilikuwa na bado ninamuunga mkono Mbowe. Ila nilikuwa naombea Lissu ashinde kwa sababu maneno yake na ya wapambe wake yaliashiria fujo kama angeshindwa. Mtu ambae aliangalia tu wakati mtu aliyefanya nae kazi kwa karibu kwa miaka zaidi ya 20 akitukanwa na kusimangwa kwangu mimi hana integrity. John McCain alijijengea heshima kubwa alipomkatiza shabiki wake aliyesema kuwa Obama ni muislamu na sio mzalendo. McCain alimwambia yule mama kuwa " hapana, tunatofautiana mawazo na Obama lakini ni mtu anayestahili heshima na ni mzalendo". Lissu badala yake akawa ana chochea moto kwa tuhuma zisizokuwa na kichwa na miguu za pesa za Abduli. Make no mistake, aliyekuwa akimlenga ni Mbowe, sio Wenje.

Hawa ndio watu waliosema kuwa CDM imeoza, imejaa rushwa. Wataaminika na nani wakisema tofauti ya hivyo? Wengi sana wanalia machozi ati wakimpongeza na kumshukuru Mbowe.

Hiyo propaganda ya uchaga haijazimwa. Bado kuna wakina Lema. Na kwa vile watu wametambua kuwa siasa za maji taka zinalipa, watu waangalia na kujiuliza waislamu wako wapi?

Ni vigumu sana kulirudisha jini ndani ya chupa ukilifungulia. Tuombe Mungu kuwa watatambua makosa yao na kujisahihisha. Lakini I am not holding my breath. Kuna saying inasema " uwe muangalifu sana unapomuomba Mungu kitu maana anaweza kukupa ulicho omba".

Amandla...
 
Uko spot on. Mimi nilikuwa na bado ninamuunga mkono Mbowe. Ila nilikuwa naombea Lissu ashinde kwa sababu maneno yake na ya wapambe wake yaliashiria fujo kama angeshindwa. Mtu ambae aliangalia tu wakati mtu aliyefanya nae kazi kwa karibu kwa miaka zaidi ya 20 akitukanwa na kusimangwa kwangu mimi hana integrity. John McCain alijijengea heshima kubwa alipomkatiza shabiki wake aliyesema kuwa Obama ni muislamu na sio mzalendo. McCain alimwambia yule mama kuwa " hapana, tunatofautiana mawazo na Obama lakini ni mtu anayestahili heshima na ni mzalendo". Lissu badala yake akawa ana chochea moto kwa tuhuma zisizokuwa na kichwa na miguu za pesa za Abduli. Make no mistake, aliyekuwa akimlenga ni Mbowe, sio Wenje.

Hawa ndio watu waliosema kuwa CDM imeoza, imejaa rushwa. Wataaminika na nani wakisema tofauti ya hivyo? Wengi sana wanalia machozi ati wakimpongeza na kumshukuru Mbowe.

Hiyo propaganda ya uchaga haijazimwa. Bado kuna wakina Lema. Na kwa vile watu wametambua kuwa siasa za maji taka zinalipa, watu waangalia na kujiuliza waislamu wako wapi?

Ni vigumu sana kulirudisha jini ndani ya chupa ukilifungulia. Tuombe Mungu kuwa watatambua makosa yao na kujisahihisha. Lakini I am not holding my breath. Kuna saying inasema " uwe muangalifu sana unapomuomba Mungu kitu maana anaweza kukupa ulicho omba".

Amandla...
Poleni sana.
 
Ngongo, uko spot on. Mimi nilikuwa na bado ninamuunga mkono Mbowe. Ila nilikuwa naombea Lissu ashinde kwa sababu maneno yake na ya wapambe wake yaliashiria fujo kama angeshindwa. Mtu ambae aliangalia tu wakati mtu aliyefanya nae kazi kwa karibu kwa miaka zaidi ya 20 akitukanwa na kusimangwa kwangu mimi hana integrity. John McCain alijijengea heshima kubwa alipomkatiza shabiki wake aliyesema kuwa Obama ni muislamu na sio mzalendo. McCain alimwambia yule mama kuwa " hapana, tunatofautiana mawazo na Obama lakini ni mtu anayestahili heshima na ni mzalendo". Lissu badala yake akawa ana chochea moto kwa tuhuma zisizokuwa na kichwa na miguu za pesa za Abduli. Make no mistake, aliyekuwa akimlenga ni Mbowe, sio Wenje.

Hawa ndio watu waliosema kuwa CDM imeoza, imejaa rushwa. Wataaminika na nani wakisema tofauti ya hivyo? Wengi sana wanalia machozi ati wakimpongeza na kumshukuru Mbowe.

Hiyo propaganda ya uchaga haijazimwa. Bado kuna wakina Lema. Na kwa vile watu wametambua kuwa siasa za maji taka zinalipa, watu waangalia na kujiuliza waislamu wako wapi?

Ni vigumu sana kulirudisha jini ndani ya chupa ukilifungulia. Tuombe Mungu kuwa watatambua makosa yao na kujisahihisha. Lakini I am not holding my breath. Kuna saying inasema " uwe muangalifu sana unapomuomba Mungu kitu maana anaweza kukupa ulicho omba".

Amandla...
Mkuu Fundi Mchundo heshima sana.

Uchaguzi umekwisha,walioshinda tayari wapo mzigoni maajabu waliyohubiri kipindi cha kampeni tunayasubiri kwa hamu na shauku kubwa.

Bado miezi michache tuingie kipindi cha uchaguzi mkuu,maandalizi ni sasa muda ni mfupi kweli kweli nguvu iliyotumika kuchafua wengine ilimradi ushindi upatikane sidhani kama itasaidia kutupatia ushindi.

Ilikuwa rahisi kwakuwa wapiga kura walikuwa 1,200 au 1,300 hivi.Sasa tunatakiwa kuwafikia wapiga kura 15 to 20 million.
Hoja lazima zibadilike habari za kilamba asali au amekaa sana au blah blah si hoja tena ni viroja.
 
Mbowe alitakiwa ku step aside kabla ya uchaguzi, kilichotokea kime hurt legacy yake Kwa kiwango kikubwa
 
Mwaka 2013 nilijiondoa Chadema baada ya kugundua ni kikundi cha kikabila chenye lengo la kuchukua dola...

Leo 2025 naangalia namna Lissu atavyotengeneza sura mpya ya chama ili nifanye maamuzi ya kurejea...

Mbowe alikua kiongozi mzuri mwenye mapungufu mawili makubwa...
(1) Ukabila
(2)Ni mwepesi kushawishiwa kwa pesa...

Naamini Lissu ataipa Chadema sura mpya ya kitaifa na kufanya kuaminika nchi nzima...
 
Mbowe alitakiwa ku step aside kabla ya uchaguzi, kilichotokea kime hurt legacy yake Kwa kiwango kikubwa
Sasa mnataka kumgeuza Mbowe Biden? Legacy ya Mbowe imejengeka zaidi kwa kuendesha uchaguzi uliokuwa wazi na huru. Na kwa kukubali matokeo. Lissu alimshauri apumzike baada ya kutangazwa mshindi. Sasa kwa nini mnaendelea kumfuata fuata? Hamna luxury hiyo maana uchaguzi mkuu ni kesho tu. Wenzenu waliisha anza kampeni.

Amandla...
 
Ngongo, uko spot on. Mimi nilikuwa na bado ninamuunga mkono Mbowe. Ila nilikuwa naombea Lissu ashinde kwa sababu maneno yake na ya wapambe wake yaliashiria fujo kama angeshindwa. Mtu ambae aliangalia tu wakati mtu aliyefanya nae kazi kwa karibu kwa miaka zaidi ya 20 akitukanwa na kusimangwa kwangu mimi hana integrity. John McCain alijijengea heshima kubwa alipomkatiza shabiki wake aliyesema kuwa Obama ni muislamu na sio mzalendo. McCain alimwambia yule mama kuwa " hapana, tunatofautiana mawazo na Obama lakini ni mtu anayestahili heshima na ni mzalendo". Lissu badala yake akawa ana chochea moto kwa tuhuma zisizokuwa na kichwa na miguu za pesa za Abduli. Make no mistake, aliyekuwa akimlenga ni Mbowe, sio Wenje.

Hawa ndio watu waliosema kuwa CDM imeoza, imejaa rushwa. Wataaminika na nani wakisema tofauti ya hivyo? Wengi sana wanalia machozi ati wakimpongeza na kumshukuru Mbowe.

Hiyo propaganda ya uchaga haijazimwa. Bado kuna wakina Lema. Na kwa vile watu wametambua kuwa siasa za maji taka zinalipa, watu waangalia na kujiuliza waislamu wako wapi?

Ni vigumu sana kulirudisha jini ndani ya chupa ukilifungulia. Tuombe Mungu kuwa watatambua makosa yao na kujisahihisha. Lakini I am not holding my breath. Kuna saying inasema " uwe muangalifu sana unapomuomba Mungu kitu maana anaweza kukupa ulicho omba".

Amandla...
Binafsi nimemdharau sana Lissu na mashabiki zake wengi… walieneza shutma na kashfa mbaya sana Mara ooh pesa zinagawiwa Chooni Mara Samia na Mbowe wamekubaliana kuongeza pesa kwenye uchaguzi hii issue Lissu atailipia vibaya sana!
 
Binafsi nimemdharau sana Lissu na mashabiki zake wengi… walieneza shutma na kashfa mbaya sana Mara ooh pesa zinagawiwa Chooni Mara Samia na Mbowe wamekubaliana kuongeza pesa kwenye uchaguzi hii issue Lissu atailipia vibaya sana!
Poleni sana na endeleen kuumia na kama mkiona vipi hameni chama. Lissu ndio mwenyekiti kwa sasa mpaka 2029 wanachama watakapoona hafai watamuondoa lakini kwa sasa ndio hitaji la wakati. Nendeni na Mbowe mkatafute mafekeche kama alivyosema.
 
Back
Top Bottom