Kwhyo we unajua mwisho wa hii story ukoje!?hv mijitu km nyie bdo ipo!?Mbona sijaona cha kuhatarisha maisha bado?
Pole, ila hiyo biashara ya punda hata mie nilishituka nikacheka kidogo [emoji3]Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 3.
Baada ya ile gari kumalizika kuoshwa tuliondoka kuipeleka nyumbani kwa yule tajiri wa ile gari aliyekuwa akikaa mitaa ya Magamaga!..Sasa baada ya kuondoka pale kwa tajiri,Mtatiro akaniambia tuingie gengeni tukapate msosi halafu anipeleke gheto nikapige mbonji na yeye aelekee kulala kwa demu wake.
Basi bana asubuhi kama kawaida akawa amekuja mida ya saa 12 akanigongea nikaamka!.
Mtatiro "Vipi mwanangu nikuache ulale au tusepe zetu?"
Mimi "Ngoja ninawe uso tuondoke mwanangu"
Sikutaka kabisa kulala kwasababu jamaa angeniona mzembe.
Baada ya kujipaka mafuta tuliondoka na Mtatiro akawa ameelekea kwa bosi wake kuchukua ile gari ili ampelekee dereva ambaye angemkuta pale stendi!.
Mtatiro "Ngoja twende kuna jamaa yangu ana kipanya kina piga ruti ya Sirari"
Aliendelea "Siunaweza kukomaa mwanangu?"
Mimi "Nitakomaa mwanangu wala usijali"
Mtatiro "Dingi yako nilikuwa namuona ni mjanja kumbe ana mambo ya kinoko hivyo!"
Sasa mtatiro yeye alichoamini ni kwamba mzee wangu ndiye mzinguaji bila kufahamu yote hayo msababishaji ni mimi.Sikutaka kabisa kumweleza mambo mengi ya nyumbani,nilichomwambia ni kwamba mzee kanitimua nyumbani niende nikajitegemee!.Baada ya kufika pale stendi akamkabidhi dereva gari kisha akamuomba simu ili ampigie yule jamaa yake mwenye kimchomoko aweze kuzungumza nae!.
Walipozungumza na huyo jamaa,jamaa alimwambia niende nitamkuta kwenye njia ya Nyamwaga Road amepaki na akawa amemuelekeza namba za gari!.Nilitembea kwa haraka ili nimuwahi jamaa.
Nilifanikiwa kumkuta jamaa na tukasalimiana!.
Jamaa "Mambo vp?"
Mimi "poa kaka"
Jamaa "Sasa tutaondoka nitakuacha pale sirari,wewe utahakikisha unakuwa unanitafutia abiria wa kuja nao Tarime halafu nitakuwa nakupa posho!"
Mimi "sawa kaka"
Jamaa "Lakini si utaweza?,maana hii kazi siyo lele mama"
Mimi "Nitaweza kaka wala usijali"
Jamaa "Ningekuweka hapa Town sema kuna wakuda fulani watakusumbua pale kijiweni"
Sikuwahi kabisa kufanya kazi za kwenye magari lakini sikuwa na namna ilibidi nipambane kama mwanaume ili nipate pesa!,nilitaka na mimi niwe kama Mtatiro aliyekuwa mchangamfu na mcheshi asiyejali kitu!.Yule jamaa alikuwa akimiliki gari aina ya Pro box(Kimchomoko) na alitaka mimi nikawe mpiga debe wa kumtafutia abiria upande wa sirari!.
Jamaa "Ingia twende zetu"
Basi tuliondoka yale maeneo niliyomkuta na kuelekea kwenye stendi za zile gari za kuelekea sirari,baada ya kufika pale nilitelemka nikakaa pembeni kuangalia wahuni walivyokuwa wakigombania abiria kuwapeleka kwenye magari waliyokuwa wakiyapigia debe!.
Baada ya zamu yetu ya kupakia kufika,kuna jamaa wakaanza kuitia abiria mpaka gari ikajaa!.Gari ilipojaa jamaa akaniambia niingie nyuma ya buti ambapo pia kulikuwa na abiria wengine wawili ili twende akaniache sirari niianze kazi yangu ya kupiga rasmi!.
Tulipofika pale sirari nikashuka na nikaanza kuchangamka maana nilitelemsha mizigo ya abiria kwenye kile kigari,nilianza kuita abiria kwa kuchangamka lakini nikaja kugundua haikuwa kazi rahisi hata kidogo!.Lile eneo kiukweli niliwakuta baadhi ya wapiga debe ambao kila mtu alikuwa na gari zake alizokuwa akiitia abiria!.
Namshukuru Mungu abiria wakajaa kwenye gari na jamaa akaondoka mimi nikabaki!Sasa kwakuwa mimi na wale jamaa kazi yetu ilikuwa moja,tulianza kupiga stori za hapa na pale!.Kuna jamaa mmoja ambaye nilikuwa nasikia wenzie wakimuita pengo na sikufahamu kama ndilo lilikuwa jina lake au ulikuwa ni utani tu!,alikuja tukawa tunazungumza!.
Pengo "Mwanangu Keraryo ni bosi wako?"
Mimi "Keraryo ndiyo nani?"
Pengo "Huyo jamaa uliyemuitia abiria!"
Mimi "Yule ni brother tu"
Pengo "Sikia mwanangu,angalia jamaa asije akakudhurumu posho yako"
Aliendelea "Jamaa wamemkataa watu kibao hapa kijiweni kwasababu hatoi posho!,unamuitia abiria akiondoka ndo imetoka!,na ndiyo maana unaona gari yake ikifika wahuni hawana habari nayo"
Mimi "Hakuna tatizo mwanangu yule ni brother"
Pengo "Sawa mwanangu kama ni brother wako haina noma"
Basi sikutaka maneno mengi sana kwakuwa ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuifanya ile kazi!.
Sasa ilipofika jioni baada ya kujaza tena ile gari,jamaa alinikabidhi posho ya siku ambayo ilikuwa buku 3,kiukweli nilikata tamaa sana baada ya jamaa kunipatia ile hela lakini sikutaka kumwambia,niliamua kujikaza kisabuni kama mwanaume!.Kumbuka tangia asubuhi nilikuwa sijaweka kitu chochote tumboni.
Baada ya jamaa kunipatia ile posho akaniambia niingie kwenye gari turudi Tarime mjini maana sasa ilikuwa giza!,nilipofika mjini nilielekea kwa mama ntilie kupata msosi kisha niliondoka kuelekea kwenye geto la Mtatiro ambaye nilikuta amefunga,nilikaa nje kumsubiri na ilipofika mida ya usiku wa saa 4 jamaa alirudi akiwa na mwanamke!.
Mtatiro "Mwanangu umefika muda mrefu?"
Mimi "nimefika mida ya saa 1"
Mtatiro "Nilienda kwa shemeji yako"
Baada ya kuzungumza,jamaa alifungua gheto akawa ameingia yeye na demu wake,sasa kiukweli niliwaza sana ni wapi nitakwenda kulala maana jamaa alikuwa na demu wake.Sasa nadhani baada ya jamaa kuona nina mawazo aliniambia nisiwaze kwani tungelala wote mle ndani.
Basi bana,jamaa alitandika chini mifuko ambayo juu yake akaweka nguo akanitaka niegeshe ile kibishi ilimradi kupambazuke tukaendelee na mitikasi ya utafutaji!.
Ule usiku kwakweli kwa upande wangu ulikuwa usiku mbaya sana kwasababu jamaa alianza kutafuna papuchi ya yule demu wake bila huruma,hakujali kabisa na wala hakuona aibu!,kibaya zaidi yule demu wake nae akawa analia kilio kisicho cha machozi huku mwanaume mimi nikiendelea kujigeuza kila sekunde kana kwamba nimepakwa upupu!.Niliapa kabisa ya kwamba,nisingethubutu kabisa kulala kwenye geto la mshikaji kama hizo ndizo zilikuwa habari zenyewe!.
Namshukuru Mungu asubuhi kulikucha na sisi tukaondoka zetu huku demu wa jamaa akiwa bado amelala!.
Baada ya kumaliza kazi ile jioni,sikutaka kabisa kurudi Tarime mjini na nilimwambia jamaa kesho angenikuta hapo Sirari nikimsubiri!.Usiku ule niliamua kutafuta guest ya bei nafuu iliyokuwa hapo maeneo ya jirani nikawa nimelipa elfu 5 nikawa nimelala.Baada ya kufanya ile kazi ndani ya wiki moja huku nikiendelea kukaa hapo Sirari,nilipata marafiki ambao pia walinifundisha namna ya kufanya kazi zaidi,badala ya kutegemea gari ya brother Keraryo pekee,nikawa naitia abiria na gari za mabosi wengine kisha napata posho,kiukweli nilianza kuchangamka na kuizoea ile kazi,kwa siku nilikuwa sikosi elfu 15 mpaka 20 mfukoni,hiyo ilikuwa ni posho tu!.
Nilipokusanya pesa ya kutosha,ndani ya mwezi huo nilitafuta chumba cha elfu 15000 nikapanga!.
Sasa kwakuwa sikuwa na hela ya kununua godoro,nilienda kwenye duka nikanunua maboksi ya kutosha kutandika chini ili nikilala nisije nikaumia mbavu!.
Uhuhuuuuuuuuu........asante sana wa nyumbani,.. . yani sikuingia huku siku 3 nimekuta uneniita nimekimbiaje?../////
Wala Mzee Lameki aka MakonoHii haina Mwise wala Monica?
Oohh yeah.Ikirunguri ( ubhusara)
Hio gar nsngepanda mmqNilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 17.
Mtatiro "Mwanangu mimi unadhani kwanini sitaki kukaa kwa ndugu!"
Aliendelea "Tatizo ukiongea unaweza kuonekana mbaya wakati unadai chako"
Mimi "Nakomaa sana mwanangu na huku kuna baridi kishenzi,lakini jamaa hilo halioni"
Mimi "Ngoja niangalie hali itakavyokuwa nikiona miyeyusho nachafua!"
Mtatiro "Wewe ukiweza njoo tukapambane minadani mwanangu!"
Aliendelea "Kuna hela nasubiri braza anipe nianze kukimbizana minadani!"
Aliendelea "Kwani ule mzigo uliisha kabisa?"
Mimi "Bado upo kaka lakini kidogo"
Mtatiro "Kama ngapi imesalia!"
Mimi "Ipo kama laki 6"
Mtatiro "Hapo ukichenji utabaki na kasalio kidogo,hebu ngoja wiki hii nicheki braza akinitumia tuangalie tusepe wapi!"
Mimi "Poa mwanangu!"
Yalikuwa ni maongezi kati yangu na rafiki yangu wa damu Mtatiro,huyu jamaa alikuwaga zaidi ya ndugu,mambo yote muhimu nilikuwa nikimshirikisha na yeye pia alikuwaga akinishirikisha mambo yake,nilipokuwa nafeli aliumia sana kama ndugu kwasababu tulipendana sana!.
Basi niliamua kupambana na ile kazi ya uvuvi lakini ilifika mahali nikakata tamaa kutokana na kutopata malipo,niliendelea kusubiri uenda ningepewa ile kazi ya usimamizi kama nilivyokuwa nimeahidiwa lakini ikawa hola,niliamua kuwa mvumilivu maana ndani ya mwezi huo rafiki yangu Mtatiro yeye alianza kazi ya kuuza mitumba huko minadani lakini mimi nikamwambia ngoja kwanza nisikilizie hali itakavyokuwa.
Sasa nakumbuka siku moja nikiwa hapo ziwani nimepauka sina hili wala lile,simu ya Mtatiro iliita nami nikaipokea!.
Mtatiro "vp mwana?"
Mimi "Shwari mwanangu"
Mtatiro "Bado upo mwaloni?"
Mimi "Bado nakomaa mwanangu!"
Mtatiro "Mwanangu leo Gabriel amenipigia simu!"
Mimi "Acha utani mwanangu!"
Mtatiro "Kweli mwanangu kwanini nikutanie!"
Mimi "Duuu!,jamaa yupo uraiani?"
Mtatiro "Kwanza anakuulizia kinoma!"
Aliendelea "Nimemwambia uko Mwanza na anasema anakutafuta sana upatikani,nikamwambia Umughka alishabadili namba siku nyingi"
Mimi "Jamaa anasemaje sasa"
Mtatiro "Hatujapiga sana stori maana alikuwa anakuulizia sana,ila ameniambia anakuja Mwanza na amesema tufanye juu chini tuonane!"
Aliendelea "Mwanangu leo nipo hapa Katoro nilikuja kuleta mzigo ila jioni nageuka Mwanza!"
Mimi "Vipi kazi inalipa!"
Mtatiro "Watu wa huku wanavaa sana maspesho mwanangu,yaani najilaumu kuchukua hii mitumba!"
Aliendelea "Ila wapo wanaonunua tu kiaina!"
Aliendelea "Nikirudi jioni Mwanza nitakucheki"
Mtu niliyekuwa nikiunga bando napiga nae stori nyingi alikuwa ni mshikaji wangu Mtatiro pamoja na wanangu wa Tarime!.Kiukweli baada ya kuona mambo hapo mwaloni yanakuwa magumu niliamua kuondoka kurudi kwa sista ili nione la kufanya,sikutaka kuendelea kukaa sehemu ambayo nilikuwa nikifurahia kula samaki na ugali wakati mfukoni hakuna chochote,nilishazoea kushika hela kwa sana tu kwa wakati huo,kile kitendo cha shemeji kunifanyisha kazi ya uvuvi kwa takribani miezi mitatu pasipo malipo sikukiafiki hata kidogo.Nilipofika kwa sista sikutaka kumwambia kwamba mumewe alikuwa hanilipi ili kujiepusha na uchonganishi,nilifahamu uenda ningemwambia pengine angenihisi mimi ni mvivu tu ambaye sipendi kufanya kazi na nishazoea kuzurura!,hivyo nikaamua kupiga kimya!.
Nilipotoka kule mwaloni Magu niliondoka tu kama naelekea mjini Magu na ningerudi baadae lakini haikuwa hivyo,hakuna mtu niliyemuaga maana wao walidhani nafika tu mjini halafu ningerejea!.Sasa kuna muda shemeji alikuja pale nyumbani kutoka huko kwenye shughuli zake na akashangaa kuniona pale akidhani uenda muda ule ningekuwa mwaloni!.
Hiyo ilikuwa ni baada ya kupita siku 3 baada ya mimi kutoka huko!,jamaa alikuwa amechukia sana lakini nahisi alishindwa kuongea sababu ya mkewe,mimi ile hali niliiona na kwasababu nilikuwa mtu mzima niliamua kujiongeza ili kuepusha mambo mengi!.Haiwezekani nikufanyie kazi miezi yote hiyo ushindwe kunilipa halafu bado niendelee na kazi!,yeye alidhani mimi kwenda kwake ndiyo sasa aanze kunitumikisha kama punda,nilikuja kugundua kumbe hata lile suala la kumwambia sista kwamba kuna muhindi alikuwa akihitaji usimamizi kwenye mitumbwi yake zilikuwa ni fiksi tu,hakukuwa na muhindi wala bibi yake na mihindi!.
Nadhani mwanzo kama mtakumbuka nilisema ya kwamba,ninao ndugu kibao tu hapa mjini Dar es salaam lakini huwa nawapotezea kwasababu wengi wao wanajifanya matawi ya juu huku wakiwa na nyodo pamoja na dharau kibao!.,Huyo shemeji na dada yangu kwasasa wanaishi Dar es salaam lakini sijawahi kuthubutu kukaanyaga kwao kwasababu jamaa ana roho mbaya mno!,simsemi vibaya lakini hapendi ndugu wa mwanamke!,Maza mwenyewe alishakata miguu kuja kwa binti yake baada ya kuona hali ya jamaa anavyokuwa akitembelewa na ndugu wa mke!.Mimi nampenda sana jamaa kama navyowapenda watu wengine na namuheshimu lakini sitaki kabisa kujishobokesha,napambana tu kivyangu,nikiwaga nina shida za hapa na pale huwa nina wasiliana na sista basi inatosha!.
Basi baada ya kuona yale mazingira sitoyaweza,nilimwambia dada yangu kuna mahali nimeona nikajaribu maisha kwasababu yale maisha ya kisiwani yamenishinda!.Dada aliamini ni kweli maisha ya kule yamenishinda lakini kiukweli haikuwa hivyo!,niliamua nifunike kombe mwanaharamu apite!.
Kweli!,Dada yangu nakumbuka alinipatia shilingi laki moja na akaniambia nikiwa napata tatizo niwe namjulisha!.Nilimpigia mshikaji wangu Mtatiro akawa ameniambie nipande gari za kuelekea Usagara nitamkuta ananisubiri maeneo yale!.
Nilifanikiwa kufika na nikamkuta Mtatiro ambaye tuliongozana nae mpaka kwenye nyumba ya kaka yake aliyokuwa akiishi yeye na familia ya kaka yake tuliyemuacha Bunda akikomaa na madini!.Ile nyumba ilikuwa na braz ake aliyekuwa mwanajeshi wakati huo huko Kigoma!.
Siku nazo hazikuganda zikawa zinapepea kama upepo,sasa nakumbuka siku moja tukiwa katika mihangaiko mnadani kwenye kijiji kimoja kilichopo huko Geita kinachoitwa Nzera,nikapigiwa simu na mshikaji wangu Magesa ambaye aliniambia ya kwamba,yule mzee aliyekuwa akimiliki ile nyumba niliyokuwa nimepanga pale Sirari amekuwa akienda pale kijiweni kunitafuta bila mafanikio,sababu ya yeye kunitafuta ilikuwa ni kuhusu kodi yake ya nyumba,nilichofanya nilimwambia Magesa kama anaweza aende anihamishie vile vitu na ningevikuta kwake kwasababu yeye alikuwaga amejenga japo nyumba ilikuwa kama pagale tu maana kuna vyumba vingine vilikuwa havijaisha!.
Mimi "Mwanangu nitakutumia hela ya kubebea wewe nisaidie nitavikuta kwako!"
Magesa "Kwani huko ulipo utachukua muda mrefu?"
Mimi "Naweza kuchelewa kaka,ndiyo maana nakuomba unisaidie!"
Mimi "Unavyoweza kuvitumia wewe tumia kaka ilimradi visiaribike tu!"
Magesa "Sawa haina noma,we kama itawezekana nitumie hela ya usafiri nitavifata!"
Baada ya yale mazungumzo niliendelea kupiga mwano kuita wateja wa kununua mavazi pale mnadani!.
Sasa baada ya mwezi kukatika baada ya mimi kuanza kuifanya ile shughuli ya uuzaji wa mitumba huku mimi na Mtatiro tukiendelea kuzunguka katika minada mbalimbali huko vijijini,siku moja Gabriel alimpigia simu Mtatiro na akawa amesema inapaswa tuonane haraka!.
Kweli,baada ya kutoka kwenye mnada mmoja huko Sengerema tuliamua kesho yake hatutoenda mnadani bali tungeenda kumuona Gabriel.Kesho yake mida ya saa 4 asubuhi tuliondoka kuelekea Nyakato ambako Gabi alikuwa amemwambia Mtatiro tukifika hapo tumwambie!.
Tulipofika Mtatiro alimpigia simu Gabi akawa amemwambia tumefika hapo Nyakato,jamaa alimwambia tusubiri hapo kuna gari ilikuwa inakuja kutuchukua.
Hazikupita hata nusu kuna jamaa akawa amempigia simu Mtatiro akimuomba amuelekeze mahali tulipokuwa tumesimama ili asogee kutuchukua,baada ya maelekezo tukaona Gari land cruiser hard top la njano likiwa na vioo vyeusi likisimama na dereva akitufanyia ishara ya kutakiwa tupande tuondoke!.
We jamaa ilikuwaje ukakaa kwa shemeji miezi 3 bila kudai chako? Ingekuwa mimi mwezi mmoja tu ningepiga simu kumuuliza mshahara wangu vip
Kwenye masuala ya hela usionee mtu aibu aisee , mi nilishajifunza ukimuonea mtu aibu kudai hela yako na yeye anakupotezea full..!
limradi unadai kweli, hata kama ni mtu ubanuheshimu namna gani usione aibu kumdai hela yako
Halafu huyo Gabi ilitakiwa ukate nae mawasiliano moja kwa moja baada ya kukamatwa tena, atakutia matatizoni tena
Anyways yameshatokea tayari
Hio gar nsngepanda mmq
Ikawa mchana ikawa jioni Umughaka anaisogelea jela
Acha kufuatilia stori basi. We achana nayoMbona sijaona cha kuhatarisha maisha bado?
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 15.
Mimi "Sidhani kama ningekuuliza kama ningekuwa nayo!"
Yeye "Jamani!,ila wanaume nyie hamuaminikagi kabisa!"
Aliendelea "Yaani umughaka leo nakupigia simu unaniuliza mi nani!"
Mimi "Hii line nime renew ile ya kwanza ilipotea!"
Yeye "Haya bhana,mi Leah"
Kiukweli ile sauti ya huyo mwanamke ilikuwa ni sauti mpya kabisa katika masikio yangu,mimi sikutaka mambo mengi nikawa nimeamua tu kumdanganya ya kwamba line ilipotea nika renew hivyo majina nayo yakaenda na maji,sasa aliponitajia jina la Leah ndipo akazidi kunichanganya kabisa kwasababu hakuna mwanamke niliyekuwa nikifahamiana nae akiitwa Leah.Nilikuwa nikijaribu kuvuta picha alikuwa ni Leah wa wapi lakini picha inakataa!,sasa nilifahamu uenda wakati nikiwa pale Sirari na washikaji wakati tunapiga mtungi kuna demu nimewahi kuchukua namba yake lakini kwasababu ya pombe nikashindwa kuisevu,niliamua kubaki na hiyo tafakari moja tu ya kwamba uenda tulikutana kwenye mabar huko!.
Sikutaka kumkatisha ili asijisikie vibaya,mimi nikaungana nae na kumpokea kwa kauli iliyoonyesha kumfahamu!.
Mimi "Oooh! za siku!?"
Yeye "Nzuri tu,uko wapi!"
Mimi "Nipo kijiweni"
Yeye "Mmh unanidanganya!"
Mimi "Kweli!,nipo kijiweni"
Yeye "Nimepita nikusalimie lakini sijakuona"
Mimi "Kwani we unajua mi nafanyia wapi kazi?"
Yeye " Tuachane na maswali mengi bhana,tuonane basi"
Mimi "Lini?"
Yeye "Leo kama itawezekana"
Aliendelea "Lakini leo sitaki kwenda Guest nataka kuja kwako"
Kiukweli nilijaribu kuvuta picha alikuwa ni mwanamke gani huyo lakini bado sikupata majibu yanayoeleweka!,lakini pia katika maisha yangu pale Sirari kwa wakati ule sikumbuki kama niliwahi kulala na mwanamke Guest,mimi nilikuwaga napenda kampani na washikaji tu na kunywa bia mbili tatu lakini sikuwahi kabisa kuwa addicted na masuala ya wanawake mpaka ifike steji ya kulala nao kwenye magesti,mademu wengi tuliokuwa nao wakati huo walikuwa ni mademu wa washikaji zangu na ndiyo wengi nilikuwaga na namba zao kama mashemeji zangu!.
Ile nyumba ambayo nilikuwaga nimepanga pia sikuwahi kabisa kumpeleka mwanamke wa aina yeyote,sasa ilikuwa ajabu kuongea na huyo mwanamke na kuniambia eti " Lakini leo sitaki kwenda Guest" kana kwamba hata hiyo gesti yenyewe nishalala na mwanamke!.Fedha yangu kubwa iliishia kwenye Misosi na Kupiga pamba,kiukweli hadi leo ndivyo vitu vinanilia hela na wala si wanawake!,sina hobby kabisa na mademu ingawaje ninaye demu mzuri tu wa kiwango cha kimataifa!.
Niliamua kumpigia mshikaji wangu Nyamori ili pengine anieleze uenda angekuwa anamfahamu yule demu lakini pia akasema yeye alikuwa amfahamu,pia nikampigia mwanangu Magesa nikamuuliza kuhusu jina la huyo demu nae akasema hamjui,nilijaribu kumpepeleza Magesa ili anifahamishe uenda kuna demu amewahi kuja kunitafuta pale kijiweni kwa siku za karibuni lakini jamaa akasema hakuna!.Sasa niliamua kumshirikisha Mtatiro lile suala ndipo akaniambia inapaswa niwe makini uenda mapongo walikuwa wakiandaa mtego wa panya ili wanidake kupitia mwanamke.
Mtatiro "Hebu nipe hiyo namba tuone"
Nikampatia Mtatiro ile namba akajaribu kuipiga,alipoipiga bahati nzuri ikapokelewa na mwanaume lakini mtu aliyepokea ilionekana alikuwa kwenye kelele kama za watu wengi hivyo hawakuweza kusikilizana!.
Mtatiro "Hii namba inabidi uachane nayo maana wajinga watakuwa bado wanakusaka"
Aliendelea "Tena huyo demu akipiga we usipokee mkatie kabisa"
Sikuwa na shaka na maelezo ya jamaa yangu Mtatiro maana ni mtu ambaye mara zote alikuwaga akinishauri sana!.
Nilichokifanya nilikopi majina yote muhimu kwenye ile simu na kisha nikatoa ile line ya simu nikaitupa,kesho yake nikaenda kusajili line mpya ya Airtel. Baada ya kuona hapo Nyasana mambo hayanilipi niliamua kumwambia Mtatiro ya kwamba mi inabidi nieleke Mwanza kwa sista.Mtatiro nae ni kama alikuwa keshakata tamaa ila braza ake ndiye alionekana kikwazo kwake!.
Mtatiro "Mwanangu mi namuaga kama akikataa kuondoka namuacha yeye apambane,atajua mwenyewe!".
Mtatiro alitaka arudi na yeye Mwanza akaangalie ishu nyingine maana pale kijijini ni kama alikuwa akipoteza muda,sasa aliniambia hapo Mwanza kuna nyumba ilikuwa imejengwa na kaka yao mkubwa ambaye alikuwa mwanajeshi na ndipo alipofikia,na huyo braza ake aliyekuwa hapo Nyasana mgodini pia alikuwa akiishi pale na familia yake kwakuwa hiyo nyumba haikuwa na mtu!.
Baada ya Mtatiro kumwambia huyo braza ake waondoke maana hapo ni kama alikuwa akipoteza muda lakini jamaa alikuwa haelewi kabisa,yeye alikuwa akisema lile eneo kuna madini na atabaki kukomaa,sisi kama tunaondoka basi tuondoke na yeye tumuache!.Hatukuwa na namna ilibidi sisi tuondoke kuitafuta Mwanza.Sasa mpaka wakati huo zile hela feki zilikuwa zimebaki Tsh milioni 1.8,na ambazo tulikuwa tumechenji na nyingine kutumia zikabaki halali laki 4.Hivyo zote halali na feki zilikuwa Tsh milion 2.2.
Tulipokuwa hapo Bunda tulinunua nguo na viatu pia mara kibao tulikuwa tukienda hapo mjini kupata beer na kula vizuri,hivyo kujikuta hela zinazidi kupukutika!.
Nilipofika Mwanza niliamua kutengana na Mtatiro,mimi nilielekea kwa sista aliyekuwa akiishi Meko na Mtatiro yeye akaelekea huko Usagara!.Nilimpatia jamaa yangu hela kama laki 6,feki nilimpa laki 4 na halali nikampatia laki 2 ili angalau zimsaidie atakapokuwa huko!. Baada ya kufika hapo kwa sista kiukweli sikutaka kabisa kukaa,sasa shemeji alikuwaga akitoka kuna alikuwa akimaliza hata wiki ndipo anageuka nyumbani!.Nilimwambia sista aongee na shemeji ili amwambie yule muhindi kama bado ile kazi ipo nikaifanye lakini kwa bahati mbaya jamaa akasema ishapata mtu muda mrefu tu!.
Kuna siku shemeji akawa ameniambia niende nae akanifundishe kazi ya kusimamia wavuvi wake kwenye ile mitumbwi yake ili nitakapokuwa na ujuzi wa kutosha awe ananiachia usimamizi na yeye kuendelea na shughuli nyingine,nikawa nimekubali maana sikutaka kukaa tu hapo kwa shemeji nionekane mzigo!.
Tuliondoka na shemeji tukawa kama tunaelekea Musoma,sasa tulipofika Magu tulishuka,kuna gari ilikuja kumchukua pale tukawa tumeondoka hadi kisiwani huko ndani ndani, kile kisiwa kilikuwa kinaitwa kisiwa cha Ijinga,Aisee nilipofika hapo nilikuta kuna mitumbwi kama uchafu,kuna ambayo ilikuwa imefungwa injini za Yamahama na Honda,pia ipo mitumbwi ambayo ilikuwa ya kawaida tu!.
Baada ya kufika hapo shemeji akawa amemuita jamaa mmoja wakaanza kuongea!.
Shemeji "Aisee nimewaongezea mvuvi"
Jamaa "Aaah ndo huyu bwana eeh!"
Shemeji "Eeeh bhana mfundisheni kazi ni shemeji yangu"
Jamaa "Sawa bosi wangu"
Nilibaki kuduwaa na kushangaa maana niliambiwa naenda kusimamia mitumbwi lakini baada ya kufika kibao kimebadilika na kuitwa mvuvi!.