BlackBerry
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 1,839
- 958
Imenichukua muda kuisimulia hii hadithi iliyo ya kweli..
Nahisi ni mie mwenyewe katika dunia hii nilokumbwa na mkasa huu wa aibu na ambao sitausahau maishani..
Ama kweli sikusikia la mkuu na hayo yakanitokea na mpaka leo najutia..
Sikupenda iwe hivyo hadi leo wewe usome habari yangu hii lakini natazama na kwa mbali, maji yalishamwagika.
Walezi wangu waliniamini tangu nikiwa mdogo kuwa kijana mwema, hakika hawakukosea.
Kunipeleka shule nikatoe ujinga na kusoma elimu ya dini walinipatia.
Sikuwa mgomvi, mtukani wala jeuri ila kimoja tu kilinifanya kuangamia,
Dhakali iliyo ktk maungo yangu ilinitia topeni ikanichafua..
Kipindi hicho namaliza kidato cha sita binti mrembo nyumbani akaingia..
Si kwamba aliletwa nimweke gambani na kunililia..
Bali awe Dada wa kazi nyumbani kutusaidia..
Tamaa za tupu ya mbele zikanizidia, baadaye nikamwingilia..
Zikapita siku za kufurahia.. Aah kumbe machungu yaningojea..
Kaniita siku moja huyo dada/mpenzi akaanza kunambia..
Nimejaa my dia nataka kuitoa..
Wote nyumbani wakajua, nkabaki kuchukia binti kawa harufu mbaya sitaki hata akisogea..
Wote wakagundua vikao kukaliwa..
Binti akasanua ati mie ndo nilokamua,
sina la kuamua tusubiri kumpokea..
Mpaka sasa naongea mwana yu miaka tano..
Nimetaabika sana moyo wangu ukiungua..
Kumwoa sikupanga je? Nifanyeje kumlipia!
Nampenda mwanangu aishi kwa ulezi wa baba na mama..
MAMAYE KUMWOA SINTAWEZA...
Ushauri wenu utanifungua mawazo..
Wasalaam..
Muowe awe mke wako unasemaje?Umesha muharibia maisha yake, Hata kwa Mungu una makosa wewe ukimuacha Solelemba.
Maisha ni kweli nimemuharibia japo nami nimepata athari kutokana na kwayo,
Lakini katika suala la dhambi hilo kiimani kila mtu ana mbinu zake za kuomba msamaha...
Kumwoa hakika sintaweza kwakua bado nina kumbukumbu mbaya iliyokuja baadaye..
Yeye pia anajua na yuko radhi mie nipatapo mtu nimwoe,.@Mzizi
Kama alivyosema Gaijin,
Jaribu kadri uwezavyo kumuona na kutumia muda mwingi uwezavyo na mwanao.
Baada ya muda mtapendana tu!!...it's so natural!
Usimfiche, mwambie mimi ni baba yako, nakupenda kwa moyo wote ila sintaweza kuishi na mama yako, ila namweshimu sana kwa kukubeba wewe kwa miezi tisa(au kumi...whatever).
Akikua.....nduguzo hawatamtupa, watamkubali tu.
Mwisho ndugu yangu, wala usijute..... mtoto ni baraka. Ila ashiki yako uihusishe na mapenzi, kwani ngono bila mapenzi ni sawa na besheni tu!
Unataka mwanao aishi na malezi mama na baba, ila hautaki kumuoa mama yake. Hakuna njia ya kufikia lengo lako isipokuwa kumuoa huyo Mke.
kwa nini hutaki kumwoa huyo dada? kwa kuwa umesoma naye hakubahatika unaona sasa sio wa class yako sio? pupa zako zilimharibia malengo dada wa watu huenda maisha yake yangekua mazuri baadae sasa unaona haya kumuoa kisha una elimu kumliko. tafdhali hebu tafakari kisha uchukue hatua. japo kwa kiasi unampenda mwanao kumbuka machozi ya huyo dada yatakufuata mpaka kaburini na katika maisha yako yote hutokuwa na raha. hadithi hii imenisikitisha sana kuona wanawake wanafanywa kama carpet/dust bin/dekio kukidhi mahitaji ya wanaume wasiokua na huruma. Jamani ukimuoa huyo dada utapungukiwa na nini? kama ni kusoma unaweza kumsomesha akafikia kiwango utakacho.
haipendezi hata kidogo. mwonee mwanao huruma pamoja na mamake. nakusihi sana fikiria mara mbili.
yangu macho tu.
Kutenda kosa si kosa bali kurudia kosa ndio kosa...sasa naona wewe unataka kulirudia...please muoe huyo dada ili mtunze huyo mtoto. Usiwe selfish kaka mfikirie na yeye...umemuharibia future yake...angefanya mangapi ya maendeleo hadi sasa bila ule ujauzito na mtoto aliyezaa...dhihiriisha uungwana wako kaka ... just marry her... mapenzi huja baadae... manake ht waliooana wanapendana baadhi yao ndo hawa tunakutana nao mahakamani wanadai au kutoa talaka zao...
Unasema huna mapenzi naye je tangu mmeanza mahusiano ulishamuona au kuskia kuwa ana mwanaume mwingine? je ni mwaminifu kwako? sio kwamba nasapot ww kujichanganya na mdada ila mlishakuwa na wadada wangapi hapo kwenu is she the first one?if not may be there's somthing btn u two,mke mwema mtu hupewa na bwana haijalishi watu wanasemaje ila cha msingi tambua kuwa wote mlikosea na huna haja ya kuendelea kumchukia you need to start over.Kaka yangu yaliwahi kumkuta hayohayo na mdada akafukuzwa imagine kaka alikuwa haonekani home kumbe akawa amempashia chumba somewhere huko na akampa mtaji akawa na biashara ndogo,the girl was smart,alikuwa anamshauri kaka mambo mengi tu ila baada ya wazazi kugundua walinyan'ganya mtoto mradi tu kaka asiende huko na kweli yule mdada akaolewa na mwanaume mwingine na sasa hivi kaka yangu yupoyupo tu mara leo ana huyu kesho huyu ..sometime wazazi wanajuta niliwahi kuwaskia wakisema bora tungemsomesha yule binti. You will never know what future holds for you ,kama yeye anakupenda pls think twice kama anaendelea na mambo yake i think thats fine you may carry on also but its good to raise your son with his mom.
tatizo ulimpenda kwa ajili ya kumaliza haja zako na tayari ulikuwa na mapenzi nae sasa yamekuja matokeo unaanza kumuona mchafu .... acha tabia za ajabu kaa chini mjipange jinsi ya kulea mtoto
honestly Swahilian nashindwa kukuelewa,are you feeling guilty kwa kuzaa kabla ya kuoa au una feel guilty kwa kuzaa na house girl? if it is the latter kwangu litakuwa jambo la kusikitisha sana maana ina maana ungezaa na airhostess au nesi basi usingefeel guilty? huo sasa utakuwa ni ni unyapapaa ambao haukubaliki.Kiila siku tunaimba humu mmu tujifunze kuwathamini watu si kwa sababu ya taaluma zao au pesa zao bali kwa sababu ya utu wao,umenipata Mkuu?Always remember housegirl ni mwanamke kama mwanamke mwingine yeyote na ana haki ya kupendwa na kuenziwa just like any woman!
Muoe tu huyo msichana, kaanze kumsomesha hata veta, inaonekana unampenda sana, ila unaona tu aibu kwamba ni HG
kwani hawa wafanyakazi wa ndani wanatofauti gani na wadada wa ofisini kama siye?mbona tukienda ulaya na sie huwa tunakuwa watumishi tu wa ndani?au inakuwaje, hamuoni mifano hata kwenye tamthilia, wakaka wengi tu wanaoa watumishi wa ndani, aaaarghhh,, wasichana sijui watadhalilishwa mpaka lini
Hapa nimekusanya tu baadhi ya dondoo ambazo Wana JF wanakushauri. Maoni yangu ni kama ya hawa walonitangulia. Ninachokushauri uzipitie tena hizi, bbadaye mwenyewe utaamua.The best man is one who take care of his wife and chilldren ole wao wafanyao zinaa na kuwafanya wengine waangamie kwa maovu yao Baba yetu hatakuwa na huruma kwa watu hawa bali kwa kuomba msamaha kwa wale waliowakosea na hata kuwatendea mema wasibaki wakijuta kwa maumivu waliyopata..... huwezi kumwoa... unataka malezi ya baba na mama kwa mtoto..... mtendee mtoto wako haki ya malezi ya wazazi wake wote
Maisha ni kweli nimemuharibia japo nami nimepata athari kutokana na kwayo,
Lakini katika suala la dhambi hilo kiimani kila mtu ana mbinu zake za kuomba msamaha...
Kumwoa hakika sintaweza kwakua bado nina kumbukumbu mbaya iliyokuja baadaye..
Yeye pia anajua na yuko radhi mie nipatapo mtu nimwoe,.@Mzizi
Imenichukua muda kuisimulia hii hadithi iliyo ya kweli..
Nahisi ni mie mwenyewe katika dunia hii nilokumbwa na mkasa huu wa aibu na ambao sitausahau maishani..
Ama kweli sikusikia la mkuu na hayo yakanitokea na mpaka leo najutia..
Sikupenda iwe hivyo hadi leo wewe usome habari yangu hii lakini natazama na kwa mbali, maji yalishamwagika.
Walezi wangu waliniamini tangu nikiwa mdogo kuwa kijana mwema, hakika hawakukosea.
Kunipeleka shule nikatoe ujinga na kusoma elimu ya dini walinipatia.
Sikuwa mgomvi, mtukani wala jeuri ila kimoja tu kilinifanya kuangamia,
Dhakali iliyo ktk maungo yangu ilinitia topeni ikanichafua..
Kipindi hicho namaliza kidato cha sita binti mrembo nyumbani akaingia..
Si kwamba aliletwa nimweke gambani na kunililia..
Bali awe Dada wa kazi nyumbani kutusaidia..
Tamaa za tupu ya mbele zikanizidia, baadaye nikamwingilia..
Zikapita siku za kufurahia.. Aah kumbe machungu yaningojea..
Kaniita siku moja huyo dada/mpenzi akaanza kunambia..
Nimejaa my dia nataka kuitoa..
Wote nyumbani wakajua, nkabaki kuchukia binti kawa harufu mbaya sitaki hata akisogea..
Wote wakagundua vikao kukaliwa..
Binti akasanua ati mie ndo nilokamua,
sina la kuamua tusubiri kumpokea..
Mpaka sasa naongea mwana yu miaka tano..
Nimetaabika sana moyo wangu ukiungua..
Kumwoa sikupanga je? Nifanyeje kumlipia!
Nampenda mwanangu aishi kwa ulezi wa baba na mama..
MAMAYE KUMWOA SINTAWEZA...
Ushauri wenu utanifungua mawazo..
Wasalaam..
kaka kwanza mshukuru mungu kwa kupata mtoto kuna watu wanatafuta sana watoto hawapati, pili wape wote huduma, mtoto na mama yake coz mwanamke ukishamzalisha (tena mwenye maisha ya chini) ni sawa na kumuharibia maisha yake kwani si rahisi sana akapata mwanaume atakayemthamini.
Tatu, wala usijiskie vibaya, kwani alikubaka? Si ulimtamani na mkaenjoy tunda pamoja? Iyo ndo result, ipokee kama zawadi, hakuna haja ya kufeel guilty hapo, na wewe sio wa kwanza (hata mahita alizaa na hg hahahaa), we jua tu "shit happens"
Hapa nimekusanya tu baadhi ya dondoo ambazo Wana JF wanakushauri. Maoni yangu ni kama ya hawa walonitangulia. Ninachokushauri uzipitie tena hizi, bbadaye mwenyewe utaamua.
The best man is one who take care of his wife and chilldren ole wao wafanyao zinaa na kuwafanya wengine waangamie kwa maovu yao Baba yetu hatakuwa na huruma kwa watu hawa bali kwa kuomba msamaha kwa wale waliowakosea na hata kuwatendea mema wasibaki wakijuta kwa maumivu waliyopata..... huwezi kumwoa... unataka malezi ya baba na mama kwa mtoto..... mtendee mtoto wako haki ya malezi ya wazazi wake wote