Nimeachana na hawara nachanganyikiwa

Hebu kaa na mume wako na mwambie kwamba unamwacha uone atafanya nini....
 

tatizo unaweza kuishi na mume mzinzi miaka na miaka na usigundue!!!!!!!
pole kisukari...
 
Sasa kama mume humpendi wala humtaki wa nini unabaki nae?!Kama umeona hamna kitakachobadilika kaanze maisha yako upya mlee kila mmoja akiwa kwake!


Watu wengi wanaishi kwenye ndoa za kitumwa ilimradi waonekane ni wanandoa lakini ni bora kuivunja ndoa inapodhihiri kuwa wanandoa hawana amani wala furaha kutokana na tabia na matendo ya wenziwao sijui maana dini nazo zinadai tubebe misalaba ,hata kama ni ya cuma na inawaka moto,
Mtazamo wangu ni either kujitahidi kuijadili kwa wema hiyo ndoa yenu na kama mtaona kuwa hamuwezi kabisa kuendelea kuishi ni bora pia kuachana kwa wema kila mmoja anaweza pata mwingine mkaishi vizuri na kusahau yaliyopita
 
vidumu oyeeeeeeeeeeeeee,kwani huwezi kuwakeeep wote wawili?mbona wengine wanaweza?lol:confused2::whistle:

Na hii ndo dawa ya wanaume wazinifu! kumuacha huwezi as jamii zetu bado talaka inaonekana ni kitu cha aibu! so kidumu chako kimya! Heshima ya uongo ndani n big love kwa watoto maisha yanaenda, yaani kuwa na kidumu kunapunguza hizi stress na kushuka sukari sababu ya ndoa,
 
Mi naona tatizo ulikimbilia kutafuta suluhisho nje ya ndoa(the so called kidumu) kabla hujashirikisha wahusika wa familia as advised b4, mbaya zaidi huwajui wanaume hata kidogo!Mtoto tulia,tena nakwambia utakuja juta wewee,shauri yako.Utahesabu wanaume weeeee at last utakuta umri umeenda,hakuna anayekutamani tena,unaishi as single mother(maisha ambayo ukiwa kijana utaona ni matamu,si uko free) ila ukishazeeka utajikuta kwenye TATIZO la UPWEKE usioelezeke.

Tatizo unataka UKALE UJANA ndani ya NDOA.Kama wewe ni islam ruksa kudai talaka,naona wenzetu hawa ndoa IN/OUT ni kawaida kama kupanda daladala na kushuka,tena waume nao kibao,unaachwa leo kesho anakuoa ?(????????????NIDHAMU NA SAIKOLOJIA YA WATOTO JE)


Mimi sijaona tatizo serious kwa mumeo hapa,ninachoona ni wewe kupagawishwa nje ya ndoa.Binadamu wote hukosea,ulichukua hatua gani?

Si ulishamkuta kaacha mara2,sasa ulidhani wewe ni malaika na wenzio waliotangulia walikuwa mashetani?Huyo kidumu chako ushaishi naye ukajua mapungufu yake,nakuhurumia sana mdogo wangu.
 

Hizi sentensi huwa zinaniacha njia panda. Miezi miwili tuu unatokea kumpenda mtu hivyo? Maana kuna thread nyingine hapa, mwanamke aliishia kukopesha mwanaume milioni sita baada ya kuwa kwenye mahusiano naye kwa miezi mitatu tuu. Wanawake kwa nini mnapenda ghafla hivyo?
 
You said it all. Two wrongs does not make it right. Sasa wewe wasema mumeo hajatulia, na wewe umetafuta kidumu; yaani kwa kuwa yeye kamwaga mboga na wewe wamwaga ugali. Mimi naona huo ni ubinafsi!

Kuna watu wawili ambao hauwajali. Mwanao na huyo kijana.

Kama mumeo ni mzinzi (japo kwa sasa na wewe ni mzinzi mwenzie) hauoni kuwa ulikuwa unahatarisha maisha ya kijana unayezini nae. Tena masikini ya Mungu kijana alikuwa hajuhi kuwa wewe ni mke wa mtu? Je una uhakika gani kuwa wewe na mumeo hamna maradhi hadi kwenda kutembea na kijana "unayempenda" kama kweli unampenda au unataka kumuua?

Pili unaposema mumeo kapokea simu ya huyo kijana na akamfokea unanifanya niwe na mashaka kama kweli mumeo ni mzinzi. Tabia za wanaume wazinzi ni wakali kuliko maelezo kwangu mimi mumeo kumfokea tu mwizi wake inanifanya nihisi unamsingizia kuwa ni mzinzi, mzinzi ni wewe mumeo unamuhisi tu.

Mimi pia ni mwanamke na najua wanawake ni wavumilivu, inapofikia mwanamke kutojali familia na kuanza kushindana na mumewe lazima nikemee hata ungekuwa ni ndugu yangu.

Kama ndoa imekushinda chapa lapa sio kuchanganya wanume.

Sorry kwa kuwa too critical
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…