Nimeahirisha kuoa.

Sangari

Senior Member
Joined
Oct 31, 2011
Posts
172
Reaction score
59
Ndugu wapendwa wa MMU, Nimeona niahirishe kuoa baada ya kukutana na wapenzi 2 humu jf tukakubaliana na suala zima la ndoa lakini mwisho wake wananitosa. Mmoja tulifikia hatua ya kwenda kutambulisha dakika za mwisho akaingia mitini. Wa pili tulifikia hatua ya kuonana tufahamiane baada ya kuafikiana kila kitu kwenye mawasiliano nae akazamia kusikojulikana. Haikuishia hapo, mwingine nikakutana nae kanisani tukaweka mambo sawa mwezi sasa umepita kakata mawasiliano. Anadai suala la kuolewa halipo tena kwenye akili yake. Kwangu mimi umri unasogea lakini nimeona tu bora niahirishe kuoa niendelee na maisha ya peke yangu kama kawaida kuliko kuendelea kudanganywa na hawa wanawake. Kama kuna ushauri nipeni waungwana.
 
shida ni nini......? au una mkono birika.....?
 
Pole...
Ila sasa unamkomoa nani? Unajua Law ya Use and Misuse???
Umebakizwa mwezi mmoja tu, unaamka kitu kimepotea, si haukitumii.
 
Mkuu ukiona wapenzi, wachumba wanakukimbia ni lazima ujikague na upige magoti kwa imani yako umuulize mungu kulikoni. Jichunguze kwa hakika utagundua unapobugi step!!
 
Hawa wanawake wa sasa wenye price tag??

Asugue labda apate hela

Katika hawa hawa kunawengine ni wifing material sasa aombe mungu ampe mke mwema ambaye atendana naye. Maana naona anachukuwa wale ambao si wake ndio maana wanamkimbia.
 
Ila kweli

Au jamaa analoose focus kwenye vidate??
Katika hawa hawa kunawengine ni wifing material sasa aombe mungu ampe mke mwema ambaye atendana naye. Maana naona anachukuwa wale ambao si wake ndio maana wanamkimbia.
 
hebu wataje ? maana wengine tuna watu wetu huku unapogenerolize mambo unatufanya tuonekane vibaya! au mnataka niachwe?
 
Hawa wanawake wa sasa wenye price tag??

Asugue labda apate hela
hivi hao wadada wa jf wanaolalamikiwa kila siku ni kina nani?
mbona mimi sipati jameni mchumba huku? au mimi sio mzuri? au nimelogwa?
 
Njoo nikutengeneze

Kuna wachumba wengine kuliko kuwapata bora uwakose, mtu anaombwa unyumba na mama mkwe ili azae? Khah!

hivi hao wadada wa jf wanaolalamikiwa kila siku ni kina nani?
mbona mimi sipati jameni mchumba huku? au mimi sio mzuri? au nimelogwa?
 
Hebu mwaga wasifu wako hapa, pengine tatizo unalo wewe na ukikaa nao muda mfupi tu wanakuwa washakufahamu na kuamua kukukimbia
 
hivi hao wadada wa jf wanaolalamikiwa kila siku ni kina nani?
mbona mimi sipati jameni mchumba huku? au mimi sio mzuri? au nimelogwa?
Tatizo jingine AVATAR zenu ni tofauti na mlivyo.... MTU KAWEKA AVATAR KA YA Smile halafu mnapanga kuonana, unamwona mtu anafanana na avatar ya Ngalikihinja, unategemea nini? Mtu lazima atoke baru, akikuvumilia sana mwezi
 
Tatizo jingine AVATAR zenu ni tofauti na mlivyo.... MTU KAWEKA AVATAR KA YA Smile halafu mnapanga kuonana, unamwona mtu anafanana na avatar ya Ngalikihinja, unategemea nini? Mtu lazima atoke baru, akikuvumilia sana mwezi

Wote kila mmoja alimtumia picha mwenzake. Na mwingine nilimfungia safari kwenda kuonana nae live.
 
Miliki hela, vyote utavipata, hata ukimtaka malkia elizabeti

Hela ninayo ya kutosha mahitaji ya kila cku, shule ninayo graduate, nafanya kazi, Si mlevi, usafi naujua kwa ujumla, ni mrefu c mfupi. Kanisani kwa sana. Pafomansi niko vizuri. Nina afya njema, si mropokaji,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…