Nimeambiwa Simba SC wakitumia Low Block na Counter Attack Wydad Casablanca FC anatupeleka Semi Finals CAFCL

Nina wasiwasi wale warabu watatulazimisha tufanye makosa wenyewe yatakayotugharimu either Red card au Penalty.

CAF kugumu sana kumejaa majabali ya Africa tofauti na kule ndondo cup.
Hiyo ni kweli,sasa ili wasitulazimishe cha kufanya ni kumalizana nao kwenye nusu yao huko huko,marufuku kabisa kuwasubiri waje kwenye zone ya simba afu ndo waanze kukaba ni hatari sana..watakuja na mbinu mbadala ya kupiga fly over hapa sasa ndo kibu d na kina kapombe na zimbwe na mwenzie saidoo wanapotakiwa kuwa sharp kuziba flanks,ili wasipite.
 
Aina ya wachezaji wa Mamelody ni tofauti na Simba, mchezaji tegemeo Simba ni chama, spidi ya konokono, wengine wazee, mwarabu inatakiwa umpeleke spidi mwanzo mwisho, utawezaje timu imejaa vibabu kina Onyango?
 
mambo ya kifundi tuwaachie makocha
 
Pompoma USikhofu

Mnyama anashinda
 
Mamelodi hawanaga ujinga,

Wale mwanzo mwisho wanamwaga mwaniii,njugu,
 
Nina wasiwasi wale warabu watatulazimisha tufanye makosa wenyewe yatakayotugharimu either Red card au Penalty.

CAF kugumu sana kumejaa majabali ya Africa tofauti na kule ndondo cup.
Onyango afungwe spidi governor ya kufanya rafu
 
Low block ni mfumo unaohitaji kuwa na Wachezaji wanaoshinda battle ya aerial balls angalau Kwa 75%. Je tunao?
 
Ally mwenye Komwe, Kamwe hawezi kuwa na akili..
 
Coach nimemshauri kutumia Mfumo wa.

3: 4: 2. :1

MABEKI 3 wa kati.3

KENEDY.
Inonga.
Onyango

Wingback na Viungo. 4
Kapombe.
Shabalala.
MZAMIRU.
Kanute.

No Viungo wa juu. 2.
KIBU
Chama.

Mshambuliaji. 1
Baleke.

N:B. Nilitamani tuangalie pia vimo vya wachezaji warefu wangekuwa na msaada mzuri.
Sawadogo, Ottara, Boko
Lakini woote ni Mizigo.
 
Inawezekana ikiwa Onyango na Chama hawatacheza.
 
Yaani ni hivi ata mkicheza back block mtachapika kivyovyote vile, Iwe kwa kuwahonga marefa, iwe kwa kupitia dirishani, iwe kwa red card, ni lazima whydad asonge nusu fainali, kama nyie mlishindwa kutumia home advantage vizuri msifikirie waarabu watakuwa na huruma na nyie, wale jamaa awanaga huruma kwenye mechi za maamuzi ata kidogo, wao wataingia na plan A na B, Plan A ni kuakikisha mnapigwa ndani ya uwanja, wakiona mmekuwa wagumu kwa kuzuia sana wanakuja na plan B ambayo ni refa kurahisisha mambo, itatafutwa penalti au red card na mission inakuwa complited, kwaiyo izo plan mlizonazo sijui kuchezesha mabeki 7 na wakabaji wote waliobaki aitowasaidia chochote, Mlikosea mechi ya kwanza kushinda kigoli kimoja sasa wao wataenda kuwaonyesha ni namna gani unatakiwa utumie home advantage vizuri
 
Au hata mfumo wa 8 - 1 - 1 utatufaa sana
 
Hakuna namna yoyote ya kumzuia mwarabu Kwa kupaki basi, hatua izo walishavuka, wata watandika ata goli 10.

Ili umweze mwarabu chezeni mpira, muda mwingi muhakikishe mpira mnao nyinyi.
Mwambieni Kocha wenu akaangalie Yanga ya Plujin ikicheza na Ahly ugenini, waarabu waliutafuta mpira Kwa tochi na dk chache za mwisho ambazo Yanga waliamua kupaki Basi ndipo Yanga walipo adhibiwa Kwa goli la pili
Mechi Ili kwisha Kwa 2-1.
 
Mbinu pekee kwa Simba ni Defence na Counter attacks, hivyo mfumo wa 4-5-1 ndio bora zaidi. Wakati jamaa wakija kushambulia kwenye zone ya Simba, viungo wawili wanapungua na kurudi nyuma kuzuia.
Mambo mengine ni kuwa makini na nidhamu, huyu muarabu anapenda kukuadhibu kila unapokosea au kujisahau, ni timu inayojitahidi kucheza kwa akili zaidi.

Wachezaji kama Kanout, Onyango na Inonga wajipange haswaa, hao ndio wamebeba mabomu (Yellow card, Red card, Penalty, Fouls), muarabu ndio atakapopatumia akiishiwa mbinu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…