Nimeamini watu wa Mbeya, Iringa na Ruvuma ni waoga kuhusu mlima Kitonga

Pure Scientific

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2015
Posts
716
Reaction score
643
Wakuu salam zenu..
Mmekuwa waoga sana kwa kuongelea mlima wa kitonga ni hatari zaidi kutokana na kuwa na kona nyingi juzi nilipopita pale kweli nimeamini watu wanaishi mikoa hii ya mbeya, iringa, ruvuma ni waoga kuliko kwa kuwa zipo barabara hatari zaidi ya mlima huo kitonga

Barabara hatari zaidi duniani
 
Mbona kona za barabara ya nyang'oro ni kali kuliko kitonga?
Halafu nani amekuambia kwamba watu wa Kusini na Nyanda za juu kusini wanaogopa mlima kitonga?
 
Enzi ya the Mighty Kiswele iga ufe, supu ya mawe suka Marehemu Wiligisi, miaka ya 95 hadi 98 nilikuwa nikienda kunyumba lazima nikae siti namba mbili, namba moja my late bro piga UA tukikosa hizo siti hatusafiri. Kona za ruaha mbuyuni mpaka mikumi gari inapigwa 100 kph halafu wrong side. Wanaoifahamu hii barabara upande mmoja mlima upande mwingine MTO Ruaha acha bana Kiswele noma. Dar linatoka kumi na mbili saa kumi na moja jioni tupo bombambili watu wanashangiliaje. Hiyo kitonga pale mabasi yanashindana na kupigana overtake za hatari akina tahfif, tawaqal matema beach. Pale makambako kuna mbuzi walikuwa wanazurula barabarani hawapishi magari only wakisikia honi ya kiswele ni baru porini.
 
Huo utafiti ulifanyia wapi mdau, hadi unakuja na hitimisho kwamba watu wa mikoa hiyo wanaogopa kona za huo mlima,
Ninachojua mda mwingine wanapita hiyo sehemu hata usiku eneo hilo wakiwa wanaleta mazao jijini DSM kwa ajili ya biashara na kuonesha wameshauzoea huo mlima wanasafiri hata na zile gari ndogo international transit - IT usiku hapo mlimani wakiwa wanarudi ili kuwahi shughuli zao makwao.
Pia unajuwa kuwa madereva wengi wa malori na tanks za mafuta yanayoenda nchi za zambia, malawi, congo n.k pia ni watu wa mikoa hiyo na ndio ambao wanapita mara nyingi usiku ilo eneo.
Thibitisha hoja yako, bila hivyo wewe ni muongo.
 
Nilikua nimepanda coaster za shashui, yule dereva alivyokua analalanazo zile kona, ilinibidi nihame seat ya mbele niende nyuma kabisa daaah.
[emoji75] [emoji75] [emoji75] [emoji75] [emoji75]
 
uwepo wa sehemu hatari zaidi ya kitonga haimanishi kitonga c hatari
 
Mmmh huo mlima no hatar xana mkuu mi piA naogopa sana
 

HAHAAHAAAA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…