habarini wakuu?
kiujumla mimi nilikuwa mshabiki mkubwa wa timu hii ya msimbazi,lakini kwa kutazama future ya timu hii nimegundua haipo vizuri,hali hiyo ikapelekea kutojihusisha nayo kwa muda ikiwa ni pamoja na kupumzika kufuatilia soka la kibongo !
kuna rafiki yangu akanipigia simu na kuniuliza kuwa amesikia nimehama timu mimi nikamwambia kuwa sijahama timu,yeye akanishauri niende nikaondoe dought ktk tawi letu la klabu la hapa mpira pesa magomeni mikumi,mimi nikamwambia waambie kwa niaba yangu!
basi rafiki yangu huyu akawaambia jamaa yupo simba na hatoacha kushabikia simba,
mimi nilivyorudi nikasikia maneno hayo!na juzi katika ile mechi na mwadui ilivyoisha ninasema hivi"HUWEZI KUWEKA NADHIRI NA KLABU YA SOKA,MIMI NIMEACHA KUSHABIKIA SIMBA RASMI NA NAENDA KUTAFUTA CHANGAMOTO NYINGINE SEHEMU NYINGINE"
haiwezekani simba ininyime raha na arsenal ininyime raha...
hivyo nafikiria yanga au azam kuwa kimbilio langu wakati arsenal fc nitaitolea tamko tarehe 2 sept baada ya dirisha la usajiri kufungwa...
siku njema