nimechanganyikiwa ..naombeni ushauri wa ukweli wana JF

kwani waliooa na wasiooa ana tofauti gani mbona wote wapo sokoni sasa?
 

Kaunga, haya maneno yako yamenigusa sana. Tunaangalia suala la mahusiano kama ni janga la kitaifa wakati kuna watu they really enjoy being in relationship
 
Last edited by a moderator:
Tatizo unaanza kutafuta pa kutukea baada ya kuingia kwenye ndege, hata kabla ya ajali haijatokea.
 
kwani waliooa na wasiooa ana tofauti gani mbona wote wapo sokoni sasa?

Kuendekeza tamaa tu za miili yetu tu...ukiangalia sana, hata kama ntantafuta mtu mpya kila siku, matokeo ya tendo lile yanakuwa ni yale yale. Sasa mioyo yetu bwana inapenda kuongeza idadi tu katika tendo lenye hatima ile ile. Isipokuwa wapo watu wazuri wengi pia ambao ukibahatika kupata mmoja wao, maisha ya ndoa issue itakuwa sio kusuluhisha ugomvi wa mzee kulala na beki tatu, Smile
 
Last edited by a moderator:
Smile hii ni ishara kuwa wakati wako wa kuingia kwenye ndoa haujafika ndiyo maana huwezi kuona umuhimu na maana yake. Siku utakapokaa chini na kuona marafiki zako wote wameolewa, kwenye sherehe uko peke yako na wenzio wako na wenza wao, wewe unakuwa wa kuchangia wenzio michango ya harusi ya kwako haijulikani lini, wadogo zako wote wanaolewa unabaki peke yako. Wakati huo ukifika hamu ya kuwa kwenye ndoa hata hutajua imetoka wapi.
 
Kaunga, haya maneno yako yamenigusa sana. Tunaangalia suala la mahusiano kama ni janga la kitaifa wakati kuna watu they really enjoy being in relationship

I know, l have 2 brothers, yaani hadi naonea wivu mawifi zangu.

Mmoja wana 14 years of marriage bila mtoto lakini wanaishi vizuri, na my bro ukitaka gombana naye mwambie kuhusu kuzaa nje. Ana mtoto mmoja kabla ya ndoa.

Mwingine, ni mlokole fulani hivi wa kikatoliki na mchumba wake alimpata huko huko kwenye Charismatic.

Too bad, NEWS is always bad news.
 
kama unaingia kwenye ndoa kujionyesha kwa watu naona una hatari mkuu...
 
pole mamie kwa kuinsert mtazamo hasi kuhur ndoa! me c mwanandoa ila huwa nasoma vitabu vya dini na vihusuvyo mahusianô. mpango wa Mungu ulikuwa mzur sana kuhus ndoa bt ndio sekta ambayo shetan kaivamia kwa nguvu kuliko sekta nyngnezo. c kwel kwamba ndoa ni shubir bali ndoa yenye kumtanguliza Mungu na kuishi kufuata kanuni za Mungu ni paradiso ndogo thou majarib yapo kwa kiasi kidgo ukicompare na ndoa zisizofuata kanun za Mungu! omba Mungu atakupa mume mwema na utafurahia maisha yako ya ndoa.. .
 
kiukweli ushauri wako nimeusoma ila sijauelewa labda nina tatizo na huo msitari wa mwisho...dada
Smile i need to play with your psych first. And real nataka nikusaidie utoke ulipo.

hebu sema hivi" wewe nafsi yangu futa taarifa mbaya zote katika akili yangu"

kisha sema tena "wewe nafsi usiyaweke yaliyo ya kushindwa kwenye akili yangu"

pia malizia kwa kusema " akili yangu nikumbushe mema tu"

nnakwambia useme maneno haya kwani yana mahusiano na whatever you are going thru. Yaseme ukiwa unavuta hisia hadi nafsi na mwili wa nyama uchukie kuskia habari hizi. wakati unapo meditate haya give your self a space na uweke nice music for you. uskilize huku ukifanya mediation. Endelea kufanya hivi hadi uone moto wa kuchukia kuskia mambo mabaya umewaka ndani yako. Ukifanikiwa hapa basi haya mawazo yatahamia kwenye uande wa pili ambapo yatakukumbusha swt memories ambaazo umewah kuziona au kuzipata. ukion il hali ya chuk imetoweka na haali ya tabasamu imejaa uson jua kuwa ni dhahd mawazo yenye negative aspects yametoweka ndani mwako.

sasa hapa endelea na hatua ya pili ambayo ni ya kutafuta marafiki wazuri toka nao discuss juu ya aisha and wereva but siyo masuala ya mapenzi. Fanya hvi hadi uone kuwa wanaume kumbe ni marafki tu. Usjisumbue sana juu ya mume wangu atakuwa na tabia gani but wee assume all are positive and kama ni mapungufu basi ni ya kibinadamu sana. usipendee kukaa mpweke, au kusikiliza ushuhuda wa kushindwa tu.
 
Last edited by a moderator:
nikuulize swali moja dada... ni mimi peke yangu naona haya matatizo?
 
usiangalie theory twende kwenye real life dada
 
Ukimaliza kumcouncil Smile, jua unatafutwa na Kaizer kule chumbani!

 
Last edited by a moderator:
kama unaingia kwenye ndoa kujionyesha kwa watu naona una hatari mkuu...
siyo kweli Smile kama binadamu lazima wakati ukifika utaona kabisa maisha unayoishi na nyendo zako ni tofauti na binadamu wengine na ndiyo hapo utapata msukumo wa kuingia kwenye ndoa. Kuna heshima fulani kuwa kwenye ndoa ati na ni ndoa pekee itakutofautisha na machangudoa/malaya wa barabarani.
 
kuna waaofunga ndoa ili wapate wenza.........
kuna wanaofunga ndoa ili ili wapate mtu wa kuwapikia na kazi zingine zinazojitokeza
kuna wanaofunga ndoa ili wapate walezi wa wazazi wao
kuna wanaofunga ndoa ili wapunguze makali ya maisha
kuna wanaofunga ndoa kwa sababu ni fashion
kuna wanaofunga ndoa kwa kuwa wanahofia umri umeenda
kuna wanaofunga ndoa kwa kuwa wanapendana
kuna wanaofunga ndoa ili wapate watoto
kuna wanaofunga ndoa ili wapate makaratasi nchi za watu
kuna wanaofunga ndoa kwa kuwa wanaogopa kuzeeka lonely
kuna wanaofunga ndoa ili wacheze ngoma na kuchangiwa michango
kuna wanaofunga ndoa ili walee watoto
kuna wanaofunga ndoa kwa kuwa wametia/tiwa ujauzito bila kutegemea
kuna wanaofunga ndoa kwa kulazimishwa na wazazi, ndugu au jamii



kila ndoa ina style yake.................kutegemea na sababu za ndoa husika



 
Smile,
Ndoa ni taasisi ambayo Mungu mwenyewe aliiweka. Alimuumba mtu hakumkamilisha, unalijua hilo.
Ndoa ina kila kitu, na inatakiwa iwe na kila kitu ili iitwe ndoa.
Huwezi pata barabara isiyo na kona.

Na kitu kikubwa tunakosea, ni kuangalia mataizo ya ndoa za wenzetu na kuyafanya yetu!
 
Yaani Smile kwen ndo hujaona zuri hata moja?:angry:
 
Last edited by a moderator:

Kwa kifupi, maana ya kuoa/kuolewa/ndoa ni kuwa na mtu wa jinsi tofauti ambaye mnapendana kwa dhati na kuamua nyie wenyewe kuishi pamoja na kuanzisha familia huku mkishirikiana kwa kila kitu! Lengo la ndoa ni kuanzisha familia huku mkitimiziana matakwa ya mwili. Katika hali ya kawaida, jamii inategemea baada ya ndoa, wanandoa kuonyesha heshima na adabu mbele ya jamii kwa kuitunza miili yao na kujiepusha na vitendo vya uzinzi.

Tofauti na hali ya sasa, ndoa nyingi zimekuwa na matatizo ya ndoa kwa sababu ya wanandoa kufunga ndoa wakiwa ktk hali ya kutokupendana kwa dhati. kwa lugha rahisi wanakuwa wamelazimishwa na mambo fulani kama kupeana mimba, kufuata pesa au uwezo wa kiuchumi wa mmoja wao, kulazimishwa na ndugu, kujichukulia umaarufu nk nk. Ndoa kama hizi ni lazima ziwe na hayo mambo ambayo umeyatolea mfano.

Kwenye hiyo mifano uliyotoa, ni kweli hayo mambo hutokea kwa wanandoa na ni kwa sababu ambazo nimezitaja hapo juu. Suala la kufanya ni kumuomba Mungu akupe mpenzi ambaye ni mwaminifu na mwenye mapezni ya kweli ili uenjoy maisha ya ndoa kama mimi kaka yako HorsePower inanivyofurahia maisha na wifi yako mama HorseJunior! Mwamini na kumtegemea Mungu, utampata mtu wa kufaa asiye na hizo tabia zilozotajwa hapo. Ukiwa kwenye asilimia, bado tunaoenjoy ndoa ni wengi zaidi kuliko walio na hayo matatizo sema tatizo mabaya huvuma sana kuliko mema.

Tafakari!
 
kwa maneno ni vizuri ila m,atendo yenu bwana loh..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…