Nimechomwa na msumari mguuni nitumie dawa gani?

Te Lavista

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2017
Posts
1,626
Reaction score
2,846
Salamu wapendwa,

Mwenzeni nimepata ajali kidogo ya kuchomwa na msumari mguuni. Maumivu yake hayaelezeki jamani mguu umevimba kiasi maana kama nchi moja imeingia.

So nitumie dawa gani wapendwa ili ndani ya siku tatu niweze kutembea na donda liwe limekauka?

Nifanyaje?
Ahsante
 
nenda hospitali haraka acha kudekA HAPA EBO
 
Pole sana,mwagia mafuta ya taa kisha nenda ukachome tetenasi
 
 
Weka kisu jikon paka mafuta ya kula kwenye kidonda gonga kwa kutumia kisu kikiwa cha moto! Gonga kidogo kidogo angalia usiungue!; cku 2 nyingi kidonda kimekauka!!
 
Sina hela ya kwenda private nasubir kesho niende Government
Te Lavista, nimecheka sana kiongozi. Tangu aunzishe thread hukurudi tena kuchukua mrejesho.

Ulivyorudi japo comment zilikuwa nyingi, lakini umeanza kujibu ile ulioulizwa unakaa wapi ili ukachuliwe. Hahahaha nimecheka sana.

Back to topic: sina uhakika na hili japo najua sindano ya tetanus ni bure. Sina uhakika lakini. Ungecheck kwanza private ni shs ngapi kuchoma kwani haiwezi kuwa bure kabisa kwa sababu ya kulipia mishahara ya watumishi.

Ni muhimu upate hii sindano ndani ya masaa 24 kama hujawahi kuchomwa sindano ya tetanus kwa miaka mitano iliyopita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…