Nimechoshwa na unene,sasa nimeamua

Nimechoshwa na unene,sasa nimeamua

Sir M.D.Andrew

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2012
Posts
201
Reaction score
37
Nafanya mazoezi sana,nimejinyima chakula nikaambulia madonda ya tumbo,asali,maji ya uvuguvugu,ndimu vyote nimetumia mwaka sasa unaisha,matunda mboga mboga mpaka zimenichosha-jana nimepandwa na ugonjwa wa ghafla nimepimwa naambiwa presha juu,uzito wangu sasa ni kilo 98 ukilinganisha na urefu wa futi 5.4 tu,umri mdogo miaka 27 tu lakini naonekana baba wakati bado! Nimeamua kitu kimoja tu wana jf,mnisaidie kupata contacts za hebalists au clinic wanapouza dawa za kupunguza unene/kitambi...nahitaji kubaki na uzito wa kawaida! Naombeni mnisaidie
 
Sijui ratiba yako ipoje ya hizo diet zako ila kwangu zinafanya kazi napungua napohitaji na nanenepa napohitaji...kwa miezi mi3 nmepunguza kilo 6 hv na kitambi kimepungua vya kutosha nilinenepa mapaja yakawa yanasuguana na suruali kupanda katikati ila sasa historia nmeyashinda.....
Ratiba yangu
Asubuhi nilikua nafanya mazoezi nazunguka uwanja mara 10 nikirudi na kupumzika napata asali then baadae ntapata chai yangu ya viungo mdalasini iliki tangawizi...mchana nakula kama kawa jioni napiga matunda kibao....nikiamka mwepesi choo napata swafi....pia nkapunguza matumizi ya gari natembea inapobidi ...baada ya kuanza kupungua nmeacha mazoezi ya kupungua ila ratba ya msosi ipo vile vile....muhimu mwili uushughulishe na uongeze kunywa maji...
Hayo madawa utakayopewa hayana maajabu zaidi ya kukufanya uharish,,e tu.... Uamuzi ni wako
 
Back
Top Bottom