Nimefikisha miezi miwili ya kufanya mazoezi bila kutumia vyuma vizito, nafanyia home tu

Unapohisi njaa ni vyema kula ndizi mbivu au kutafuna karanga mbichi, na matunda mengineyo.

Usiagize soda
 
Push up round 10@ reps20
Squat round 10@ reps 20
Squat left leg round 10@ reps20
Squat right leg round 10@ reps20
Trycep round 10@ reps20
Kukata tumbo 10@ reps20

= reps 1200

1 hour
Jaribu na kuruka kamba ili uongeze pumzi.
 
Karanga mbichi sijui ndizi ntatapika!
Weee hujui kuziandaa,,

Nenda sokoni nunua kilo moja ya karanga zilizokaushwa,, ni kama elfu 2500 bei yake,,

Rudi home zioshe alafu ziloweke na maji ya chumvi hata kwa dakika 10, alafu zitoe na uzianike juani hadi zikauke, baada ya hapo, uwe unatafuta, hutojuta yaaaaaan
 
Hivoo?...asante ntajaribu
 
Kama nimekuelewa mkuu unafanya body building ,ukishayaanza mazoezi hutakiwi kuyaacha ili mwili wako uendelee kuwa fit.
 
Hivi kuruka kamba zaidi ya pumzi inasaidia nini? Mi naruka kamba 500 @ morning!
Hiyo wajuzi wa mambo wanakwambia inaongeza pumzi, inapunguza uzito pia[emoji16]

Ila hivi karibu nitaanza kuruka kamba, kumbe nawe mdau
 
Hiyo wajuzi wa mambo wanakwambia inaongeza pumzi, inapunguza uzito pia[emoji16]

Ila hivi karibu nitaanza kuruka kamba, kumbe nawe mdau
Yes tuko wote.... Vyote nafanya ila push up hata mbili siwezi[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kama nimekuelewa mkuu unafanya body building ,ukishayaanza mazoezi hutakiwi kuyaacha ili mwili wako uendelee kuwa fit.
Shukrani kwa kunielewa mkuu, ni vile mwili kuwa strong
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…