pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 282
- 561
Salamu, basi jana nikaona nichukue pombe kali nikanywee nyumbani, yule muuzaji akaniwekea kwenye bahasha nyeupe yenye maandishi pande zote.
Nilipofika nyumbani nikapiga fundo la kwanza na la pili kisha nikaanza kuipitia ile bahasha nilishtuka kidogo maana ina taarifa za wachangia damu wawili ikiwa na majina kamili, umri, anuani ya makazi.
Namba za simu hali ya afya ikiwa ana maambukizi ya magonjwa ya zinaa, ikiwa amewahi kufanya ngono kwa njia ya haja kubwa, au kwa njia ya mdomo....kweli hapa wizara ya afya mmetuangusha, utaratibu wa faragha ya wapatiwa huduma ukoje? ama utaratibu wa kuharibu nyaraka (disposal plan/policy) ni upi?
Bado naangalia kama itakuwa ni vyema hizo fomu nikiziweka humu ingawa kuna baadhi ya sehemu nitazificha ila pale chini kwenye jina la Afisa mtoa huduma na sahihi yake nitaomba nipaache kama palivyo... utu wa mtu uheshimiwe
Nilipofika nyumbani nikapiga fundo la kwanza na la pili kisha nikaanza kuipitia ile bahasha nilishtuka kidogo maana ina taarifa za wachangia damu wawili ikiwa na majina kamili, umri, anuani ya makazi.
Namba za simu hali ya afya ikiwa ana maambukizi ya magonjwa ya zinaa, ikiwa amewahi kufanya ngono kwa njia ya haja kubwa, au kwa njia ya mdomo....kweli hapa wizara ya afya mmetuangusha, utaratibu wa faragha ya wapatiwa huduma ukoje? ama utaratibu wa kuharibu nyaraka (disposal plan/policy) ni upi?
Bado naangalia kama itakuwa ni vyema hizo fomu nikiziweka humu ingawa kuna baadhi ya sehemu nitazificha ila pale chini kwenye jina la Afisa mtoa huduma na sahihi yake nitaomba nipaache kama palivyo... utu wa mtu uheshimiwe