Nimeipenda teknolojia hii katika simu ya OKING, nashauri makampuni mengine ya utengenezaji simu yawaige

Nimeipenda teknolojia hii katika simu ya OKING, nashauri makampuni mengine ya utengenezaji simu yawaige

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2017
Posts
8,252
Reaction score
18,335
Nina kasimu kadogo aina ya OKING (OK 1710) nilikokanunua kwa shilingi za kitanzania elfu kumi na nane tu (18,000/=). Kwa kweli kwa bei hii sikutarajia kupata simu yenye teknolojia ya hali ya juu kama hii.

Iko hivi, leo nilikachomeka chaji ili niende nacho kufanya mazoezi maana kina nyimbo ninazozisikiliza wakati wa kukimbia. Sasa baada kukitoa chaji nikaona ninaendelea kuonyesha kuwa kunapokea chaji. Nilishangazwa kwa kweli, nikadhani kuwa hali itakoma baada ya muda lakini kiliendelea kuingiza chaji.

Nimeenda uwanjani, nimefanya mazoezi, nimerudi, bado kinaingiza chaji na kinagonga mziki mwanzo mwisho. Hadi sasa ninavyoandika bado kinaingiza chaji.

Hii ni teknolojia ya hali ya juu sana kuipata kwa bei rahisi hivi, wireless charging. Nashauri makampuni mengine yawaige OKING kwa kutengeneza simu zenye feature nzuri kama hii kwa bei nafuu kabisa. Sisi watanzania wanyonge tutawaombea kwa Mungu awabariki. Kwa sasa sina hofu hata umeme ukikatika bado simu kiswaswadu changu hakitoisha chaji maana kinaendelea kujichaji hadi siku kitakapoharibika.

NB: Leo nimekimbia uwanja round 6 tu nikaanza kuhisi kifua kinabana na nashindwa kupumua na sio kawaida kwangu, mniombee.
 
Huyo jamaa alikuja kutoa simu izo speaker balaa yani ukienda nayo kutongoza demu hachomoi kipindi hicho wanafukuzana na Mwenzake G TIDE kweli maisha yako kasi sana leo naambiwa hakuna mtu anatumia Yahoo wala Siemens inashangaza
Time hio basi ni Buzz ni bomba kuna bundle hilo lilikuwa 1500 unapiga simu kutwa nzima mpaka jioni, unaongea wee unapelekea majirani nao wote wanaongea
 
Huyo jamaa alikuja kutoa simu izo speaker balaa yani ukienda nayo kutongoza demu hachomoi kipindi hicho wanafukuzana na Mwenzake G TIDE kweli maisha yako kasi sana leo naambiwa hakuna mtu anatumia Yahoo wala Siemens inashangaza
Time hio basi ni Buzz ni bomba kuna bundle hilo lilikuwa 1500 unapiga simu kutwa nzima mpaka jioni, unaongea wee unapelekea majirani nao wote wanaongea
Hatari sana mkuu, hadi sasa OKING wanai nickname kama 'music phone'. Vispika vinapasua kweli kweli.
😂😂😂😂
 
Piga nyungu kweli kweli mkuu, kifua kitaachia, utuletee mrejesho...

Everyday is Saturday....................... 😎
😀 😀 😀 😀
Nilipiga nyungu juzi kama sehemu ya kupata uzoefu, aisee sio poa. Joto kali hadi nilichanganyikiwa nikaamua kutoka kabla ya muda elekezi kufika. Hizi tiba nyingine tabu tupu.
 
Back
Top Bottom