Nimejifunza kutokufata mkumbo wa biashara inayofanywa na mtu

Nimejifunza kutokufata mkumbo wa biashara inayofanywa na mtu

Captain mopao

Senior Member
Joined
Feb 25, 2021
Posts
133
Reaction score
384
Habari zenu wadau

Mimi ni mfanyabiashara wa jeans za mtumba za kiume, sina muda sana kwenye hii biashara ni kama miezi kadhaa.

Sehemu zangu ni katika minada na magulio katika kuzunguka kwangu nikakutana na jamaa yeye anauza urembo nae pia tunazunguka wote katika minada.

Biashara yake ilianza kunivutia kwa jins alivo na wateja, maana tukifika tutafungua wote biashara lakini yeye ni wa kwanza kupata wateja na kina dada hawakauki katika biashara yake.

Taratibu nikaanza kumdodosa kuhusu biashara yake na jamaa bila hiyana akanipa feed back zote.

Nilichogundua ingawa yeye ana wateja wengi kuliko mimi namzidi mauzo maana mimi nahitaji wateja wawili kuifikisha alfu kumi ila yeye anahitaji wateja kumi au zaidi kufikisha alfu kumi.

Mfano yeye anauza heleni mia 3 au kitana mia 5 au lesso alfu moja.

Wakati mimi nauza kila suruali moja nauza alfu tano,

Nilianza kudata na biashara ambayo ingekuja kunishinda so nimejifunza kutokufata mkumbo.

Siku njema wadau.

1623232041057.png
 
Hata katika faida pia me nimemzidi mfano mimi nanunua robota moja laki mbili na nusu linakua na jeans 125 nakua nimeuziwa kila jeans alfu 2000 kawaida nauza jeans alfu 5 faida yangu ni alfu 3 kwa kila jeans wakat yeye alfu 3 ataipata baada ya kumaliza ki pakti cha hereni chenye pair kumi za hereni
 
Kwenye urembo hiyo elfu 10 anaweza akala yote na mzigo unabak wakutosha wa kesho lakin izo 2 zitoka ni pengo kubwa sna ..muuza urembo y yote mnadan mwenye meza/ggoli la mana hawez kukosa mauzo lakn ma jeniz hata hawe na mziggo wa ukweli ni kawaida kukosa wateja hata hacuzi piece 1
 
Hata katika faida pia me nimemzidi mfano mimi nanunua robota moja laki mbili na nusu linakua na jeans 125 nakua nimeuziwa kila jeans alfu 2000 kawaida nauza jeans alfu 5 faida yangu ni alfu 3 kwa kila jeans wakat yeye alfu 3 ataipata baada ya kumaliza ki pakti cha hereni chenye pair kumi za hereni
Wewe umejuaje una mzidi faida?
 
Mkuu naomba kujua Kama hutajali,hizo za laki mbili na nusu ni grade ipi? Na vipi grade nyingine Bei zake zikoje?
Balo za jeans zimefawanyika kama ifuatavyo
☆ jeans men
Hizi ni kuanzia size 28 kuendelea wanavaa kuanzia wakubwa kuendelea
Namba 1 bei yake ni laki 5
Namba 2 bei yake ni laki 2½
Zinakaaa peace mia za jeans

☆ladies
Hizi ni jeans mchananyiko za kike na kiume mara nyingi ukinunua hii unakutana na modo za vijana kuliko ukinunua jeans men utakutana na ma bwanga ijapokua inategemea mzigo ni kutoka taifa gan ila kwa experience yangu mzigo wa china na Korea hua mzigo mzuri,
Namba 1 ni laki 5
Namba 2 ni laki 2½

☆ alafu kuna boypant
Hii ndo ninayoiuza mimi humu utakutana na jeans kwanzia watoto wa miaka 8 mpka miaka 18 iv
Namba 1 ni lak 5
Namba 2 ni laki 2½
Hizi zinakaa 125
Kama unauzia kijijini nunua namba 2 km unauzia town nunua namba 1

Kwangu mimi hii biashara naona ina faida kama utakua na boypant na ladies, pia kuna jeans kali utakutana nazo ambazo utauza bei zaidi, na hizi bei ni kwa dodoma

Pia kila balo linajina lake ukitaka kununua tafuta duka watakalokupa details za kutosha ujue ni kitu gani unakwendaa kukutana nacho
 
Back
Top Bottom