Nimejikuta nasomba vitu vyote vya rafiki yangu kisa pombe

Nimejikuta nasomba vitu vyote vya rafiki yangu kisa pombe

Mkogoti

TAPELI Mkubwa
Joined
May 3, 2020
Posts
2,415
Reaction score
3,924
Wadau humu habari za saa hizi,

Okey jana bwana kuna kisanga kimenitokea kisa Kunywa pombe ila kuweka sawa tatizo hilo ni hivi Mimi huwa nikinywa pombe huwa napata vibe la hatari.

Yani nakuwa mchangamfu balaa kama kazi napiga usiseme kama ni watoto ama pisi kali basi ntaongea mpaka nakubaliwa kiulaini.

Tuachane na hayo bwana. Bwana jana hiyo nikapiga pombe zangu nipo na wana kitaa wenyewe hawajalewa ila mimi tu ndo nipo Nacheck naelea hewani, basi rafiki mmoja akaja kusema mi nahama ila nipeni kampani ya kubeba vitu kupakia kwenye mkokoteni (sio mbali na anapohamia)

Basi hao mpaka gheto kwake mi ndo mstari wa mbele kama mimi ndo nahama 🤭 Basi ili kufupisha story ni kwamba nilijikuta vitu nasomba peke angu chumba kizima😆kupeleka sehemu mpya, kila wakibeba nawaambia acha tulia nikuoneshe.

Kwakweli pombe inanipa ushujaa sana kasoro kuwakoromea polisi na wanajeshi huko watanikunja nisije nikafa bure.

Alamski🤦🤪🏃🍺 cheers
 
[emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787]ww hauna utofauti na Mimi japo umenizidi kdogo na haya ndo matumizi mazuri ya pombe tuendeleee kupiga vyombo mwana.[emoji482][emoji482][emoji39]
 
Kuna Mwana tulilewa nae kwenye kiduka cha Mangi baada ya kulewa alimsaidia Mangi kushusha kreti Kenta nzima alikuwa yuko maji baada ya kumaliza Mangi akataka amlipe Mwana kamwambia take it easy 😹
 
Back
Top Bottom