Nimekosea kutuma MPESA, je kuna msaada au basi!

Columbus

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
2,002
Reaction score
651
Baada ya kufanyiwa kazi fulani na kukamilika nilipatiwa namba na wafanyakazi hao ili nimtumie bosi wao malipo kwa njia ya M-pesa, kwa bahati mbali walinipatia namba ya mtu mwingine kwa makosa na hivyo fedha kumuendea mtu huyo. Baada ya kuwasiliana na Vodacom huduma kwa wateja walinijulisha kuwa huyo niliyemtumia hizo fedha ameshazitoa toka kwa wakala.
Baada ya mtu niliyemtumia fedha kutokuwa hewani kwa muda mrefu hatimaye aliwasha simu na nikaweza kuongea naye, alikubali kupokea fedha hizo na kuzichukua lakini aliniahidi kunirudishia. Pamoja na kumtaka achukue kiasi cha sh. elfu kumi(Tsh 10,000/- kutoka ktk fedha hizo kwa usumbufu alioupata, hata hivyo amekuwa akinibabaisha na kuzima simu yake muda mwingi na hivyo nimeona ananikwepa, Hivi kuna namna nyingine yoyote ya kuzipata fedha hizi au ndio basi tena! naomba mawazo yenu.
 
Ulifanya kosa kuongea naye. Ulipaswa kuongea na Vodacom - Huduma kwa wateja. Vodacom wangekurudishia hela yako. Ila bado hujachelewa sana.
 
Ukiongea na Vodacom huduma kwa wateja basi hata kama katoa siku akitumiwa hela kupitia line hiyo inakula kwake.

Kuna siku ilishawahi kunikuta na mimi nikampigia mhusika akawa anafanya kama huyo jamaa lakini mwishoni baada ya kwasiliana na huduma kwa wateja alifurahi pamoja na mbwembwe zake zote.
 

Pole sana mkuu,utazipata ila kwa kuchelewa coz tayari ameshazichua hivyo kwa kuwa umesharipoti,voda watakachofanya watamvizia akiweka hela tu wanazikomba,ila akiamua kubadilisha line na kuachana nayo itakuwa imekula kwako mjomba
 
Ilikupasa uongee na huduma kwa wateja,huko wangeifunga akaunti ya huyo mtu kwa muda, kila akiweka pesa inarejea kwako had hapo hela yako itakapo kamilika.
 
hata hao waliotuma namba kwa makosa nao ni hata sijui niwaiteje.
 
kuna rafik yangu alitumiwa pesa kwa mpesa kimakosa kwenye simu yake million 1 jamaa alichofanya kutoa pesa fasta na akaichana line,sasa hiv ana line nyingine mpya yuko kwa mtaa
 
kuna rafik yangu alitumiwa pesa kwa mpesa kimakosa kwenye simu yake million 1 jamaa alichofanya kutoa pesa fasta na akaichana line,sasa hiv ana line nyingine mpya yuko kwa mtaa
Huu usajili wa namba kwenye mambo kama haya sijui kwa nini haujatusaidia!!

Kwa nini wasidhibiti mpaka kwenye matumizi ya line zingine? Hivi huwa hawawezi kujua mpaka simu inayotumia line fulani? Kwa mfano Maulid kasajili line kwa kutumia kimchina chake, hawawezi kurekodi hiyo line na hicho kimchina ili kama Maulid ataweka line nyingine kwenye hicho kimchina chake ajulikane mara moja?

Tutaendelea kulizwa tu kila uchao!!
 

huo ushauri mzuri nafikiri apa kuna wadau wataufanyia kazi
 

Hioy inawezekana kabisa, ndio mana nchi zetu za jirani wameamua kuzifungia simu feki a.k.a za mchina kwani hazina IMEI, au IMEI zake feki. Ila inahitaji ushirikiano na mitandao youte kwani mtu anaweza kutupa sim card ya Voda akachukua ya TiGo na kuendelea kutumia kwa handset ile ile kwenye mtandao mwingine
 
Unakoseaje na jina linatokea pale?inabidi tuwe kamini na pesa wana JF wenzangu;maana hadi upate line na ku report,unakuta alietumiwa na njaa za sikuhizi anakuwa ameshaitoa inaanza lawama sasa,tujaribu kuwa makini sana,maana jina linatokea kabla kuthibitisha na pesa kutoka kwa mtumaji!nakubali kukosea kupo ila tujitahidi kuwa makini kwa confirm jina kwanza maana linatokea pale na una muda kuhakikisha unaemtumia!
 
Pole mzee, I hope utazipata hela zako. Next time ukipewa namba ya mtu umtumie pesa uliza jina lake kisha mpigie kwanza ku-confirm kama ni yeye ndio umtumie. It's a little inconvinience but its better than risking losing your money.
 
mi nimewahi kosea ila bahati nzuri nilipoenda mpesa WALIFANIKIWA kunirudishia. ila hii huduma ya simu pesa niliona haiko salama kabisa.inatakiwa watafute utaratibu wa kuwashitaki watu wanaotoa pesa zisizo zao. pia hawa mawakala wa simu pesa wengi hawana elimu, wanafikiri utaratibu wa vitambulisho ni mbwembwe kumbe una maana yake. pole sana ndugu kama hujapata hela yako
 

Hii mbona inajulikana kabisa mkuu na inawezekana!!
 
Mpaka sasa jamaa kazima simu yake, lakini naelewa wazi kuwa voda wangeweza atleast kum-trace kwa kujua watu aliokuwa anawapigia kabla. Lakini pia nina imani siku moja akilizwa mtu mkubwa serikalini hili suala litatafutiwa ufumbuzi ukizingatia kuwa watu wengine tunawatumia fedha bila kuwajua ili mradi ametoa na kukamilisha huduma uliyohitaji.

Mnakumbuka namna wauaji wa afande Balow walivyokamatwa! simu ndio ilifanikisha zoezi zima,ingekuwa mwenzangu na mimi ndio basi tena lakini kwa kuwa alikuwa mtu mkubwa haikuchukua muda tukasikia wahusika wa uhalifu ule wamekamatwa tena wengine nje ya mkoa wa Mwanza.
 

Mkuu,tatizo la mpesa,hawakuletei uthibitisho wa jina la mtu unayemtumia,tofauti na tigo pesa ambao wanakupa uthibitisho kwa jina la mtu unayemtumia,jina ni rahisi zaidi kwa watu walio wengi kuliko namba pekee,voda warekebishe hili.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

Toa ushauri jinsi ya kuwashitaki maana kama kosa ni lako ulietuma kwa nini umshitaki aliepokea bila hata kuomba wala hamfahamiani?kosa litaitwaje?toa ushauri tafadhali!
 

sio kweli ndugu, uthibitisho wa jina unakuja kama huyo mtu kasajili namba yake, kama hajaisajili iwe ni tigopesa au mpesa zote uthibitisho wa jina haupo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…