Nimekukumbuka Marcio Maximo

Dumelang

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2011
Posts
3,204
Reaction score
5,710
View attachment 260922Alitupatia miaka yakucheka, kushangilia na kuunganishwa kama wa Tanzania kupitia michezo.

Na nakiri hata wasiojua Mpira Enzi izo waliufahamu kwa namna moja ama nyingine, walishangilia ama kuipenda Taifa Stars

View attachment 260923
Magari yaliandika Jina lake, bajaji na daladala miaka ya Marcio na stars, ilikuwa Rais tu kuona Gari limebandika picha au kuandikwa Maximo Marcio

Kuna Watoto waliozaliwa Tanzania kati ya 2006-2009 wanaitwa jina la kocha huyu

View attachment 260924
Walau Enzi za Maximo Taifa stars ikicheza watanzania tukikuwa na Tumaini, tulithubutu kusema Leo tunashinda hata kama mechi yetu ilikuwa ni dhidi ya nguli Nigeria, Cameroon, Ivory cost nk

Ndio maana tulikuwa enzi izo tukijaza Uwanja. Kwa kumbukumbu zangu tulinunua Jezi za Star kuliko kipindi kingine Chochote.

Magari yalipita barabarani tukapiga sahihi Zetu kwenye wallpaper maalumu kuisapoti Stars
Maximo Nimekukumbuka

View attachment 260925
Tumemisi kuipokea Taifa Stars kwa Shangwe.
View attachment 260926



Leo Stars tukisema ipo kundi moja na Nigeria kila mtu anajua tushatoka

Enzi za Maximo wengi tuliondoa uoga kama huu na Jina kichwa Cha mwendawazimu lilianza au lilipotea

Ninakukumbuka Maximo
Leo lile jina la kichwa cha mwendawazimu limerudi 100%

Uliibua vipaji.
Ulikuwa na Msimamo

Naikumbuka mechi Yetu na Burkinafaso Tuliposhinda Bao 1:0 TULISHANGILIA SIKUMBUKI LINI NITASHANGILIA TENA STARS KAMA VILE

Mechi na Sudan kisha CHAN mapokezi mpka Mbunge akavua shati hadharani.

Bungeni wabunge walikubali kuachia Posho zao zote za siku, Jumla ya milioni 33

Nimekukumbuka
Siku za maisha yako ya mwisho na Stars Watu wengi waliomba aje Kocha Mwingine eti Umechoka na Umeishiwa mbinu, mimi nilikuwa bado naimani na wewe.

niliandika hapa JF: Nenda Marcio Maximo lakin Tutakukumbuka

Tangu Enzi hizo Hajaja Kocha zaidi Yako. Ndio maana Nimekukumbuka Maximo

 

Attachments

  • 1434481508752.jpg
    10.5 KB · Views: 336
kwa kweli umenena kweli tupu, soka la bongo zengwe, kilichomuondoa Maximo taifa stars, si kingine bali FITINA.
 
kwa kweli umenena kweli tupu, soka la bongo zengwe, kilichomuondoa Maximo taifa stars, si kingine bali FITINA.

Mkuu kama Maximo ni kocha mzuri, aliporejea Tanzania kwa mara ya pili, ni kipi kilimuondoa Jangwani...?
 
Wakati wa maximo tanzania tukaanza kuonekana kwenye ramani ya soka...
Alikuwa na hamasa ya ushindi kwa wachezaji...
Ila fitina zinaua proffessionalism ya timu zetu za soka...
 
Mkuu kama Maximo ni kocha mzuri, aliporejea Tanzania kwa mara ya pili, ni kipi kilimuondoa Jangwani...?

Kufundisha klabu ni tofauti na timu ya Taifa. Makocha wachache wanaofanikiwa kufundisha timu za taifa hufanikiwa kwenye vilabu.

Mifano ni Capello,Scolari!
 
Kufundisha klabu ni tofauti na timu ya Taifa. Makocha wachache wanaofanikiwa kufundisha timu za taifa hufanikiwa kwenye vilabu.

Mifano ni Capello,Scolari!

Pia Vilabu nyetu fitina, kocha ni pambo tu manager ni mwenyekiti wa Club na kamati za ufundi.

Ila marcio, enzi zake tuliona hata wachezaji wanacheza style fulan wengi Tuliamini Taifa stars ilianza kuwa na Samba la kibrazuka
 
uvumilivu ndio kitu hasa cha kujifunza kocha kufungwa mechi mbili sio ishu ningekuwa mimi rais ningempa nafasi kocha akipoteza mechi 30 ndio nafikiria kumfukuza
 
Maskimo huyu alofurushwa na yebo yebo?

Huyo huyo alikuwa Bora kwa Taifa stars, sisi vijana wa miaka ya 90s hatukuwai ipenda Taifa stars na kufuraia Mpira wa Timu ya Taifa zaidi ya enzi ya the hero and the only Maximo

Tena tungekuwa na msingi bora ya wachezaji Basi Maximo hata World Cup angetufikisha
 
" Pamoja tutashinda" (In maximo voice)
 
" Pamoja tutashinda" (In maximo voice)

I miss it " Tupo Pamoja, Tutafika" he had a Vision that we could do it, he went down streets to explore Underground talents. Mimi narudia Nimekukumbuka Marcio Maximo
 
Shida ya wabongo tulitaka kuiona pepo bila kufa

Sana tu kiongozi,tena hakuna watu wanafiki kama watz,ukifanya vizuri kweny fani flan wataanza kukupiga majungu ili ushuke chini,tena muda mwingne utasikia ashazeeka yule awaachie vijana.
Bt baada ya muda watajifanya wanakukumbuka sana.
 
Kiufupi mbongo hapendi maendeleo anaweza kujichukia hata yeye mwenyewe kisa kafanikiwa.
 
ni unafiki tu maximo hakuwa na jipya si alirudi hapa bongo au mmesahau? nini kilitokea? ni unafiki leo hii kujifanya kumkumbuka maximo... hakuna mpira aliokuwa anafundisha zaid ya kucheza na akili za watanzania.si alirud hapa akapewa team ikamshinda akaleta watoto wa dada yake waje kuchezea yanga kisa wana uzungu? tatizo uongoz wa TFF ndo wa hovyo unashindwa kudeal na wachezaji kuwafanya wawe team na ni kwakuwa viongozi wamewekana kwa kujuana .hamwez kuwa serious mkamchagua mtu kama malinzi awe rais wa TFF mkategemea kufanya vizur. HAMWEZI KUWA NA LIGI MBOVU YA KUNUNUA MECH MKATEGEMEA KUWA NA TEAM YA TAIFA NZURI. MBONA TUNAFAHAM TEAM ZINAVYONUNUA MECH?
 
Wewe ndio walewale wenye fikra zilizodumaa. Kwa taarifa yako hata angekuja Mournho au Wenga kufundisha simba na yanga siajabu baada ya ligi zisiwe hata 3 bora. Timu zetu hizi kila mchezaji ameletwa na mtu wake hivyo ni wazi atakuwa tu LOYAL kwake na sio kwa kocha.

Kuhusu maximo kutokufanya vizuri Yanga mimi naamini kuwa ni fitina za baadhi ya viongozi na wachezaji hasa wenye majina kutompa ushirikiano wa kutosha kwasababu zao binafsi au kwa maelekezo ya waliowaleta.

Naamini pia kuwa maxiomo kuleta kina Jaja na courtinho alikuwa na makusudi yake, kiufundi jaja ni mchezaji mzuri tu akipata viungo wazuri na wasiokuwa na wivu kumlisha mipira. Tukumbuke kuwa ujio wa jaja na jinsi alivyoanza kufanya vema mechi za mwanzo kabla ya ligi kuanza kulisababisha majina ya kina Ngasa kufunikwa kabisa na gumzo likawa ni Jaja, Jaja. Sasa hii ni hatari kwa mchezaji anayetegemea kulishwa tu mipira na hata kukaba hakabi. Sasa haya ndio yaliyomkuta jaja kunyimwa ushirikiano kutoka kwa Ngasa na wenzake.

Maxiomo pia alikuwa ni mtu wa msimamo hasa akisema au akiamua jambo lake kama kocha basi hakuna wakumbadilisha hivyo ni wazi kuwa kwenye maamuzi yake kuna baadhi ya mambo ya watu yatakwama na ndipo FITINA zinaanza kufanya kazi. Mfano isue ya kaseja na Boban kama sikosei ilijenga chuki kubwa kwa baadhi ya wachezaji, viongozi na mashabiki waliopo nyuma ya wachezaji hawa

Na haya ndio yaliyomkuta Maxiomo sababu ya Fitina na Roho nyeusi ya mtu mweusi.

Lakini ukweli Maxiomo alileta hamasa kubwa sana katika soka letu kipindi kile na nikipindi kile hata tuliona umuhimu wakuwa wazalendo kwa vitendo kwani tulikuwa hatuoni umuhimu wakuvaa nguo yenye bendera yetu au hata kununua flags nakuweka kwenye magari yetu.

Kipindi cha Maxiomo kiwango cha soka la Tanzania kwenye ranking za fifa kilikuwa kinapanda na alivyoondoka tu mshale ukageuza direction kwenda chini.

Maxiomo alichokifanya cha kwanza nikubadilisha mentality za wabongo na hasa wachezaji kujitambua. Pia alijenga spirit ya kizalendo kwa wananchi kuipenda nakui support timu yao ya Taifa.
 
Mwambieni mjomba amrudishe tena huenda atainusuru Stars, binafsi mimi nilifurahia ubunifu wake kwenye matangazo kama lile tangazo la Serengeti na Chui, pia jamaa alijiingiza kwenye Bongo Movies sipati picha kama angekuwepo mpaka sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…