Nimekumbuka maisha ya siasa enzi za Hayati Magufuli (JPM) siasa ilichangamka buana, na wananchi kwa ujumla wake!

Nimekumbuka maisha ya siasa enzi za Hayati Magufuli (JPM) siasa ilichangamka buana, na wananchi kwa ujumla wake!

Bulelaa

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2024
Posts
1,342
Reaction score
3,247
Enzi za (JPM) hata aliyekuwa kilaza wa siasa, alivuma

Enzi za JPM, kila raia alikuwa akitamani kushinda kwenye luninga akiangalia matukio ya siku hiyo

Huku mzee wa kuwasukuma ndani aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Tabora mzee Mwaniri, alichangamsha mkoa huo

Dar es salaam akiwapo kijana maarufu kuliko hata mawaziri (baadhi) na siyo wote bwana Paul Makonda, alilichangamsha jiji

Kule Hai akiwako kijana machachari aliyeishia jera bwana Lengai, acha buana, Mzee Lema alotamani ahame mkoa

Kijana wa Kizaramo kipindi hiko akiwa Waziri wizara ya TAMISEMI mh. Jafo, mbona siasa ilikuwa moto? kwa namna ya alivyokuwa akienda, binafisi nalianza kumpa nafasi ya yeye siku moja aje kuwa Rais wa nchi hii, huyu kijana ni alikuwa moto, nilimkubali na kumkubali haswaa

Waziri wa Sheria na mwalimu wa mambo sheria na katiba mzee wetu mh.Paramagamba Kabuudi, jina murua kabisa hili, binafsi nampenda tu huyu mzee, ni muwazi, msomi na mwenye kujiamini sana, heshima kwako mzee wetu na uishi milele, alikuwa waziri na kutumika kama mwalimu hapo mjengoni!

Waziri mkuu enzi hizo na sasa akiwakilisha vema kabisa, mh Kassimu Majaliwa Kassimu! Ulindwe na Mungu mkuu,

Akiwepo sasa na aliyekuwa kiranja wao na Rais wa Jamhuri ya watu wa Tanzanian mh. Dr. Joseph Pombe Magufuli (RIP) hakika, tulianza kuiona TANZANIA ikielekea kuzuri zaidi,

Uhamasishaji uliokuwepo kuhusu kujitoa kwa kila Mtanzania kwa kufanya kazi kwa juhudi kubwa huku wakiongozwa na uzalendo, tuliona mabadiriko makubwa yakitokea kwa kasi kwenye maofis ya umma karibu yote

Watumishi wa Umma wakiendana na kasi ya awamu hiyo,

Mbali na hayo yoyote, mazuri huwa hayakosi changamoto, yapo mengine yaliwaumiza baadhi ya Watanzania wenzetu wakajikuta wakichukuzwa zaidi na uongozi huo mpaka hivi leo

Lakini kwa uwingi wa watanzania walipenda sana na kuchangamshwa na staili ya siasa ilivyokuwa ikifanywa

Hii staili ya siasa enzi hizo, natamani tena ijitokeze huko mbeleni

Naamini, Tundu lissu akishika madaraka, siasa za kipindi cha JPM zitarudi kwa kasi ikiwezekana kuzidi kiwango chake JPM

Mungu Ibariki TANZANIA

MUNGU wabariki viongozi wote wenye nia njema na nchi yetu Tanzania
 
Umewasahau Lukuvi (Ardhi), Kalemani,( Umeme, Tanesco bwawa la umeme), Philip Mpango (Tulifika uchumi wa Kati). Awesome alichangamka wakati ule maji hayakukati ovyo, Mahiga aliiweza wizara ya mambo ya nje, Ummy Mwalimu alikuwa akipiga kazi wakati ule.
 
Ardhi ilikuwa inachimbuliwa kila mkoa, kata na kijiji.. huju tanesco unapishana nao kijiji kwa kijiji..mama ndalichako yupo bize na kukarabati shule na vyuo vikongwe.

Miradi ya maji ilipamba moto hatari..traffic na wafanyakazi wa uma walikuwa hawapokei rushwa kama hawakujui, ukiingia ofisi ya serikali unaambiwa karibu ukae hapo..umeshahudumiwa
 
Enzi za (JPM) hata aliyekuwa kilaza wa siasa, alivuma

Enzi za JPM, kila raia alikuwa akitamani kushinda kwenye luninga akiangalia matukio ya siku hiyo...
Kipindi cha Giza 🤣🤣🤣
 
KABENDERA ANADAI BEN SANANE ALIUAWA NA 'BWANA MKUBWA'!

Mwishoni mwa mwaka 2020, nilipata ujumbe mzito kutoka kwa Rais Magufuli kupitia kwa mtu wake mmoja ambaye jina lake linatunzwa. Rais alimtuma kwangu akiniomba nishawishi Mhe. Freeman Mbowe na Mhe. Tundu Lissu waridhie wabunge wanawake 19 waapishwe kuwa Wabunge wa Viti Maalum.

Nilijitahidi kufurukuta kueleza Rais ajue kuwa sikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA wala mimi sikuwa na ushawishi wowote katika jambo lile. Lakini Rais aliamini kuwa Lissu na Mbowe watanisikiliza mimi. Lilikuwa jambo gumu sana kwangu kumshawishi mtu yule aniamini mimi. Ahadi niliyoahidiwa na ambayo pia CHADEMA wangepewa kama 'dili' lile lingefanyika ingali katika kilindi cha moyo.

Nakiri kuwa baada ya ombi la Rais la kunitaka niwashawishi Lissu na Mbowe kushindikana, zoezi la uapishwaji liliendelea na mimi nikajua kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari. Lakini hoja la andiko hili sio jambo hili.

Mwezi Januari 2021, alitumwa tena kwangu mtu yule yule. Safari hii haikuwa kunishawishi ili niwashawishi Mbowe na Lissu, bali ilikuwa ni kunitisha niachane na harakati, la sivyo basi nilikuwa nachungulia mauti. Nilikuwa nimetoka kuitangazia dunia kuwa maisha ya Mhe. Lissu yalikuwa hatarini na ndipo Ubalozi mmojawapo ukamchukua na kumpeleka nje ya nchi.

Kwa hiyo jibu langu kwake lilikuwa moja tu: "Mwambie Mheshimiwa kuwa akitaka aniue, lakini Askofu hatarudi nyuma"! Vitisho vya aina hiyo niliwahi kupewa na Polisi mmoja nikiwa Central Polisi, Dar es Salaam mwezi mmoja kabla Rais Magufuli hajafariki dunia.

Baada ya majibu yale, yule mtu alitetemeka na ikabidi aropoke mambo mengi sana ambayo sio sehemu ya andiko hili kwani kwa sasa Bado mambo yale ni 'classified information'! Baada ya hapo nikaanza kupata taarifa nyingi ambazo zilinitisha na kunipatia matumaini.

Siku moja nilitafutwa na mtu mmoja ambaye ni mzima na kada wa CCM. Kwa kuwa mtu huyo tunaheshimiana na kwa kuwa aliaminishwa ya kuwa mimi nilikuwa natumiwa na 'mabeberu'; ilibidi nimueleze pia baadhi ya mambo ambayo yalikuwa yanamzunguka Rais. Nilifanya hivyo ikiwa kinga yangu kwani nilijua kuwa ataelewa mazingira yangu na hivyo ataweza kupangua hoja dhaifu dhidi yangu akiwa katika 'Pango la Wakilindi'. Aliishia kunikodolea macho na ndipo tukaagana akiwa kama mtu asiyeamini.

Lakini kabla mtu huyo hajaondoka, aliniuliza: "Wewe umejuaje habari hizi'? Nikamjibu kuwa: "Mimi ni mskofu wa mnyororo na pia mimi ni askofu wa kiapo"! Mambo haya yaliaminiwa pia kwangu chini ya kiapo kwa hiyo nisingeyasema hadharani wakati ule na hata sasa. Hapa sio mahali pake kuelezea kisa cha askari aliyeacha kufanya ibada baada ya kushiriki kuwaua watu na baadaye kumbukumbu za watu wale zikawa zinamjia na kuharibu akili yake.

Mambo haya ni ya kitubio na kwa hiyo mtu ye yote atakayemuendea Mchungaji (Padri) au Askofu kwa kitubio, jambo lile linabakia katika kifua cha mtubishaji, anayetubu na Mungu.

Taarifa za kuchapishwa kwa kitabu cha Erick Kabendera zimeanza kusambaa kwa kasi sana mitandaoni siku ya leo tarehe 3 Januari 2025. Kitabu kinaitwa: 'In the Name of the President: Memoirs of a Jailed Journalist'. Nimesikiliza mahojiano ya Erick Kabendera kuhusu kitabu hicho. Nimeanza kufuatilia maudhui ya kitabu. Mengi ya mambo anayojadili ni sehemu ya yale niliyojulishwa kama 'sisi Askofu'! Ila sikutarajia mambo yale yangewekwa hadharani wakati wa uhai wangu. Ujasiri wa Kabendera unaivuka mipaka ya Nshamba na Kamachumu.

Ninaamini watu ambao walinishangaa kwa nini mimi nilijitoa muhanga kwa ajili ya kutetea haki nchini sasa wataanza kuelewa baada ya kuona na kusoma kitabu cha Erick Kabendera. Taarifa nyingi zilizofikishwa katika kilindi cha moyo wangu ziliishurutisha nafasi yangu kuchukua ili kupaza sauti na kutetea pale nilipoweza. Lakini pamoja na uropokaji wangu, mambo ambayo yalitiwa muhuri (sealed) katika moyo wangu yameamriwa na dhamiri iliyo kuu ili yasiyoke.

Kitabu cha Kabendera kitasaidia katika mambo muhimu. Kwamba tukisome na kumjua Rais Magufuli nje ya uelewa uliojulikana. Baada ya hapo, tuone kuwa alikuwa binadamu kama sisi na mwenye mapungufu na kisha tumsamehe. Kikubwa, kama jamii tutafute njia ya kuponya ikiwemo kuondoa vimelea au masalia ya yale aliyoayaasisi ambayo hayakuwa mazuri na hili itawezekana kama tutasoma na kuielewa sura ya mwisho ya Kitabu cha Kabendera.

Kitabu hiki kinaposambazwa na kusomwa ni vizuri tujue kuwa kinayahusu maisha fichika ya Rais Magufuli na sio maisha ya familia na ukoo wake. Hatuhitaji kwa namna yeyote kuwaona ndugu hata familia kama sehemu ya mambo aliyoyafanya kama Rais kwani nao walikuwa ni washangaaji kama sisi.

Mwisho, natoa wito kwa viongozi wa dini walio karibu na familia ya Ben Sanane na familia ya Azorly Gwanda kuzifikia kwa ajili ya huduma ya kiroho. Kupitia kitabu cha Erick Kabendera na mahojiano yake ni rasmi sasa ya kuwa umma umejulishwa kuwa watu hao hawapo pamoja nasi katika maisha haya.

Hekima iliyo ndani ya kilindi cha moyo wa Rais Samia inaweza kumsaidia afanye nini kwa ajili ya familia hizo. Bila shaka, CHADEMA itatafuta namna njema ya kuhitimisha kwa heshima kwa kumkumbuka Ben, mwanachama na Msaidizi maalum wa Mhe. Mbowe. Kadhalika, Gazeti la Mwananchi litaona pia namna ya kulihitimisha l kwa heshima ya Azorly, aliyekuwa mtumishi.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 3 Januari 2025; saa 2:00 usiku
 
Back
Top Bottom