Nimekumbuka wimbo wa Chidi Benz uitwao 'Mmenisoma?'

Mwandwanga

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2011
Posts
3,059
Reaction score
1,572


Chid Benz
Mkali toka ILALAAAAA dah amenikumbusha mashairi ya HIT SONG Mmenisoma.
Ndani ya ngoma kuna sehemu CHUMA ana ghani.... "mwenye dawa mfukoni nyonga tumeze".[emoji15]

Pia mbele kidogo anasema "hawezi kujibana, nataka ni ule ujana kwa nia njema bila kufanya laana.
Kinga madhubuti na kuepuka vishawishi kwani anajua akiteleza ANA ANGUKIA MAZISHI"

Chid anasema ruka utakavyo, jiachie uwezavyo ila JALI UHAI MARA NYINGI UONAVYO!... baadaye anatuasa hivi "Mkumbushe Mwenzio kama hujapatana nae, kama somo halimwingii MPOTEZEE achana nae kisha ana malizia kwa kusema JIACHIE RUKA MAJOKA, RUKA STYLE ZOTE UNAZO PENDA, UWANJA WAKO, MUDA WAKO CHEZA VILE UNAVYOWEZA, Ila DUNIA CHAFU KUWA MWANGALIFU USIFUATE MGUU UNAPOKWENDA.

Ubeti mwingine ana anza hivi "akili ishalegea, wengi wanapotea hasa waliofumba macho wakahisi wanatembea, maneno yao UTASIKIA NA_TAKE CARE

Mvuta Bangi ana kamatwa!
Mnywa gongo anakamatwa
Kwanini Watumia madawa ya kulevya
Wasikamatwe?

Nimeichomoa Facebook [emoji119]
 
Huu wimbo ulinifanya nimuheshimu sana Chid.

Beat nzuri kutoka kwa Goodfather P.Funky Majani ilibebwa na sauti nzito yenye mamlaka kutoka kwa Chid Benzino.
Verse anazungumzia starehe tu na kujiachia viwanja na hata wenye dawa mfukoni anawapa ruksa wanyonge fresh tu.

Ila verse ya pili na ya tatu anabadilika kabisa kama sio yeye anazungumzia UKIMWI kwa namna ya kipekee kabisa ambayo itakuacha na mstuko.
Mtu aliekwambia muende club,kuruka majoka na kuvuta bange anakuhusia kuhusu ukimwi.

ukiondoka Alikufa kwa Ngoma ya FA na Starehe ya Feroos Huu ndio wimbo bora zaidi wa UKIMWI kwenye bongo flava.

Kwangu Huu ndio wimbo bora zaidi kutoka kwa Rashidi pembeni ya Dar es Salaam stand up na Hasira za nini
 
Daah so sad aisee,mtoto wa Ilala Chid Benz kawa Chid Bajaj?..
 
Chidiiii dah alkua noma sana zile mbwembwe zake, hii si nyimbo ya ku party ni nyimbo ya kuhamasisha niliwavuta kwa party ingawa weng wangebsha
 
Anawafuata waliotangulia
 
ile nyingine aliimba"haki ya Mungu natubu naacha mavurugu"saivi angetoa nyingine atubu aache poda
 
Mpiga Debe - Mzimuni Family, Msinitenge - Prof Jay, Sukari na Pilipili - SoloThang, kuna nyimbo nyingi kali za ukimwi bila kusahau ile ya ngwea ft TID -Bado Nimo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…