Nimekuelewa.
Nna ndugu yangu pia hapati madhara ya wachawi mashamba ya waganga na wachawi anaiba tu vijiweni zikija stori za kichawi anawatukana kabsaa na kuwataka wamloge.
Mwambie nenda sumbawanga kaibe kwa mtu mwenye uchawi alafu akirudi salama uje utuhabarishe.
Kuna vijana watu walikwenda kuiba miwa kwa babu fulani wakajua hakuna shida, baada ya siku mbili kupita babu akatangaza walioiba waende wakamuombe samahani lakini hawakwenda.
Siku 5 zilipita baada ya lile tangazo kisha akatoa nafasi ya mwisho na akasema asije akalaumiwa lakini bado hawakwenda.
Baada ya wiki kuisha tangu wizi utokee mmoja wa wale vijana alidonolewa mguuni na kuku aliyetotoa vifaranga kisha mguu ukaanza kuoza ikabidi ukakatwe na hadi leo ni kilema napo alipona baada ya kwenda kumuomba msamaha mzee wa watu.
Kijana mwingine alipata ugonjwa,macho yalivimba hadi yakatoka nje na yakawa yanatoa maji. Alikwenda kufanyiwa upasuaji wa macho lakini hakuchukua muda akafa.
Watatu alikua ni binti kati ya miaka 18-20 yeye yeye inasemekana alikula tu lakini hakubeba miwa kwenda nayo popote lakini aliugua ugonjwa wa ajabu kama mtu mwenye polio.
Mwili wake ulikonda sio kawaida, mguu mmoja ulikua mwembamba kama fimbo kuanzia paja hadi karibu na unyayo pote palikua sawa na mguu mmoja ulikua kama mwenye matende na alikua akikojoa mkojo sisimizi wanajaa muda huo huo mahali alipokojoa.
Ndugu wakampeleka hospitali kubwa wakampima magonjwa yote hadi kisukari lakini hawakuona kitu. Baadaye wakaenda kwa waganga na mganga akawaambia hana uwezo wa kutibu labda aende alikofanya wizi kwa mzee fulani (akataja jina) ndio akaombe samahani ndipo atapona.
Basi wakaenda kwa yule babu wakaomba samahani na babu akawaeleza kuwa wamechelewa hawezi lakini atajaribu, binti alipigwa kofi zito na kuambiwa toka hapa na ukome kuiba kisha akawaeleza nendeni. Usiku bimti alikua akitokwa jasho sana na baada siku tatu mwili ukaanza kurudi hadi akapona kabisa.
FANYA JEURI USIKUTANE NA KONKODI UTAKUA SALAMA LAKINI UKIKUTANA NA CHAWI HALISI UMEKWISHA.
Karibu Sumbawanga haurogwi bila kupewa nafasi ya kujitetea.
Jeuri zako ndio kaburi lako, unaambiwa ukaombe samahani na ukienda hana shida tena na wewe lakini ukidharau wanatuma makombora ya Atomic popote yanakufikia hata uwe nje ya nchi
Mkorintho wa 6