DOKEZO Nimelipia Bima ya Afya NHIF Mwanza, nazungushwa kupata kadi. Kibali cha matibabu pia hawanipi

DOKEZO Nimelipia Bima ya Afya NHIF Mwanza, nazungushwa kupata kadi. Kibali cha matibabu pia hawanipi

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Wana JF salama humu ndani, mimi ni mwanachama wa siku nyingi lakini ni nadra kuniona nikitumia jukwaa hili la Fichua Uovu, nimeona malalamiko mengi yanayowekwa huku yanafanyiwa kazi na mamlaka, nikaona sio mbaya nami nikifikisha hili langu kwa njia hii ili lifike mbali zaidi.

Sisi wakazi wa Mwanza naomba mtusaidie kupaza sauti kwa changamoto tunayopitia kwa hawa ndugu zetu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) upande wa Mwanza!

Niliwalipia wategemezi wangu watatu (Watoto 2 na mama yao) kiasi cha shilingi 432,000 tarehe 22/08/2023, nikaambiwa baada ya mwezi nikachukue kadi!

Nikaenda baada ya mwezi nikaambiwa “bado”, niende baada ya wiki moja, nikaenda nikaambiwa “bado, njoo baada ya wiki”.

Umefika huo muda nilioambiwa mara ya mwisho naambiwa “bado” (naandika haya nikiwa na hasira sana).

Bahati mbaya mtoto akaugua nikaenda kuomba kibali cha kutibiwa nikaambiwa nisubiri, hadi leo siku ya tatu bado hakuna lolote!

Sijui tatizo ni uwajibikaji au ni nini maana pale Ofisi ya NHIF Mwanza wenye matatizo kama haya ni wengi sana na hakuna pa kusemea, ukibishana nao wanakuitia Mgambo na hela yako wameshachukua!

Risiti ya malipo ipo na hakuna cha kuwafanya NHIF, ninayeteseka na kuumia ni mimi na familia yangu.

Pia soma: Tabia ya NHIF Tabora kuchelewesha kadi za Bima za Uanachama inatuumiza wengi
 
Ukilipia unaanza kutumia bima baada ya siku 90 mkuu, sidhani kama utapewa kibali kwa sasa
Hata kwa wenye kadi wanaanza kutumia baada ya siku 90?

Basi itabidi waseme tuu kuwa bima ni ya miezi 9 siyo mwaka mmoja
 
Hata kwa wenye kadi wanaanza kutumia baada ya siku 90?

Basi itabidi waseme tuu kuwa bima ni ya miezi 9 siyo mwaka mmoja
Kwa mwaka wa kwanza, after that ukirenew unaunganisha tu bila shida.

Tatizo watu walikuwa wanakata leo week mbili mbele wanaenda tumia laki 9 ndo mana wakaanzisha hizo siku 90
 
Africans need to be recolonized whether you like or not. Tuwape tu waarabu bandari, tanesco,Tanroad ,maji na afya pia
 
Pole kwa changamoto.

Ila upande wa pili wa shilingi ni kwamba watanzania wengi tunakata bima tukiwa tunaumwa. Huu si uungwana na janja janja tujifunze kufuata utaratibu wakuu.
 
Hiyo mwezi mmoja walikupiga siasa ili ulipe, kawaida ni miezi mitatu! Hesabu siku 90 baada ya hiyo 22/8.
 
na majibu Yao aisee 🙌🙌 sio mazuri.

Customer care Yao si nzuri

Kuna muda unajibiwa kama wanakupa huduma Bure.
 
Sijui tatizo ni uwajibikaji au ni nini
Fukuza kazi wote wanaoleta uzembe huo wa kijinga na kipumbavu ndio adabu itakuepo bila hivyo mchezo huo wa kutengeneza mazingira ya RUSHWA RUSHWA hautaisha kamwe hapo wanataka uongeze Pesa ili mchongo wako process iwe facilitated very fast
 
Kwa mwaka wa kwanza, after that ukirenew unaunganisha tu bila shida,

Tatizo watu walikuwa wanakata leo week mbili mbele wanaenda tumia laki 9 ndo mana wakaanzisha hizo siku 90
Anhaa hapo sawa. Na vipi kama unataka kuupgrade kutoka bima ya mwanafunzi ili uweze kuitumia kama mtu mzima wa kawaida.
 
Ukilipia unaanza kutumia bima baada ya siku 90 mkuu, sidhani kama utapewa kibali kwa sasa
Mimi mboni nimelipia nimeanza kutumia baada ya wiki moja? Acheni Mambo zenu za kijinga mpeni jamaa kadi zake
 
Kwa mwaka wa kwanza, after that ukirenew unaunganisha tu bila shida,

Tatizo watu walikuwa wanakata leo week mbili mbele wanaenda tumia laki 9 ndo mana wakaanzisha hizo siku 90
Utaratibu huo umeanza lini?
 
Wana JF salama humu ndani, mimi ni mwanachama wa siku nyingi lakini ni nadra kuniona nikitumia jukwaa hili la Fichua Uovu, nimeona malalamiko mengi yanayowekwa huku yanafanyiwa kazi na mamlaka, nikaona sio mbaya nami nikifikisha hili langu kwa njia hii ili lifike mbali zaidi.

Sisi wakazi wa Mwanza naomba mtusaidie kupaza sauti kwa changamoto tunayopitia kwa hawa ndugu zetu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) upande wa Mwanza!

Niliwalipia wategemezi wangu watatu (Watoto 2 na mama yao) kiasi cha shilingi 432,000 tarehe 22/08/2023, nikaambiwa baada ya mwezi nikachukue kadi!

Nikaenda baada ya mwezi nikaambiwa “bado”, niende baada ya wiki moja, nikaenda nikaambiwa “bado, njoo baada ya wiki”.

Umefika huo muda nilioambiwa mara ya mwisho naambiwa “bado” (naandika haya nikiwa na hasira sana).

Bahati mbaya mtoto akaugua nikaenda kuomba kibali cha kutibiwa nikaambiwa nisubiri, hadi leo siku ya tatu bado hakuna lolote!

Sijui tatizo ni uwajibikaji au ni nini maana pale Ofisi ya NHIF Mwanza wenye matatizo kama haya ni wengi sana na hakuna pa kusemea, ukibishana nao wanakuitia Mgambo na hela yako wameshachukua!

Risiti ya malipo ipo na hakuna cha kuwafanya NHIF, ninayeteseka na kuumia ni mimi na familia yangu.

Pia soma: Tabia ya NHIF Tabora kuchelewesha kadi za Bima za Uanachama inatuumiza wengi
Mmatapeli hao kama ni hivyo
 
Mimi mboni nimelipia nimeanza kutumia baada ya wiki moja? Acheni Mambo zenu za kijinga mpeni jamaa kadi zake
Kadi gani hio? Ulikata pvt au chuon ? Zile za vikundi ndio unaweza anza tumia soon, ila hizi pvt ni siku 90
 
Wana JF salama humu ndani, mimi ni mwanachama wa siku nyingi lakini ni nadra kuniona nikitumia jukwaa hili la Fichua Uovu, nimeona malalamiko mengi yanayowekwa huku yanafanyiwa kazi na mamlaka, nikaona sio mbaya nami nikifikisha hili langu kwa njia hii ili lifike mbali zaidi.

Sisi wakazi wa Mwanza naomba mtusaidie kupaza sauti kwa changamoto tunayopitia kwa hawa ndugu zetu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) upande wa Mwanza!

Niliwalipia wategemezi wangu watatu (Watoto 2 na mama yao) kiasi cha shilingi 432,000 tarehe 22/08/2023, nikaambiwa baada ya mwezi nikachukue kadi!

Nikaenda baada ya mwezi nikaambiwa “bado”, niende baada ya wiki moja, nikaenda nikaambiwa “bado, njoo baada ya wiki”.

Umefika huo muda nilioambiwa mara ya mwisho naambiwa “bado” (naandika haya nikiwa na hasira sana).

Bahati mbaya mtoto akaugua nikaenda kuomba kibali cha kutibiwa nikaambiwa nisubiri, hadi leo siku ya tatu bado hakuna lolote!

Sijui tatizo ni uwajibikaji au ni nini maana pale Ofisi ya NHIF Mwanza wenye matatizo kama haya ni wengi sana na hakuna pa kusemea, ukibishana nao wanakuitia Mgambo na hela yako wameshachukua!

Risiti ya malipo ipo na hakuna cha kuwafanya NHIF, ninayeteseka na kuumia ni mimi na familia yangu.

Pia soma: Tabia ya NHIF Tabora kuchelewesha kadi za Bima za Uanachama inatuumiza wengi
Wabongo bana. Mnang'ang'ania bima za matibabu wakati miili yetu ina natural immunity hatuugui kizembe zembe.

Acheni kuiga bana.
 
Ukilipia unaanza kutumia bima baada ya siku 90 mkuu, sidhani kama utapewa kibali kwa sasa
Hii imeanza lini. Kadi za watoto Ile ya 50400 ndio ilikuwa miezi mitatu,Ila watu wazima ni siku 30
 
Tz wajuaji ni wengi. Kwanza hawajui maana ya bima. Wengi kazi wanayojua ni kuzani wanaonewa na kulalamika ovyo ovyo
 
Kuna hawa wa pale bukoba sasa. Kuna ajira mpya ya mwezi wa 6 wame process taratibu zote za kupata bima maombi yametoka halmashauri za KAGERA yako pale ofisi za NHIF bukoba tangu mwezi wa saba hadi hadi leo hola wana namba yao huduma kwa wateja ukiwapigia wanakuomba check namba unawatajia wanakujibu baada ya saa moja tutakupa majibu maombi yako yamefika hatua gani😅😅 hao wanazima simu hutowapata tena.

Swali la msingi yaani maombi ya mwezi wa saba kuna wengine wa mwezi wa tano hadi leo kweli.
 
Back
Top Bottom