Nimemaliza kifungo changu leo

Range rover

Senior Member
Joined
Nov 22, 2016
Posts
186
Reaction score
195
Wadau habari zenu.

Mimi ndio nimetoka leo jela baada ya kumaliza kifungo changu. Mnamo mwaka jana mwezi wa 7 nilihukumiwa kwenda jela miaka 2 kwa kosa langu la kuiba hela kiasi cha milioni 17 kwa njia ya udanganyifu.

Nakumbuka kesi yangu ilikosa ushahidi wa kutosha lakini kuna vipengele nilikiri hivyo hakimu akanipiga nyundo 2. Nashkuru milioni 17 nimeikuta sehemu nilipoificha baada ya kutoka jela nimeamua kutafuta passport nikimbie nikatafute kazi Dubai.

Hii nchi sio jamani.
 
yn hapo ni sawa na umeiba kwa mara ya pili, na safari hi tukikukamata lazima tuhakikishe tunakutoa @#¥€~>
 
Unailaumu nchi wakati kweli ni mwizi,najaribu kufikilia uliyemtapeli huenda alikuwa na shida,,aisee karma haitakuacha salama na utaandamwa kokote utakakokimbilia mpaka utubu.
 
iba milioni kumi na saba nyingine kaifiche tumikia miaka miwili ukitoka utakuwa na 34 uraiani kugumu.
 
Umejieleza vizuri hivi ngoja ukamatwe tena maana kila kitu umeweka wazi.
 
Badala ya kufurahi kuishi Nchi ya kisela kama hii ambayo unaiba unafungwa unachat ukiwa jela,unatoka jela unakuta hela uliyoiba halafu bado unalaumu?wenzio huwa wanaenda jela na marinda wanarudi hawana marinda huko dubai umepata mume??





Mungu Ibariki Tanzania[emoji1241][emoji1241][emoji1241]
Mungu Ibariki Chakwake
Mungu Ibariki Gairo
 
Kuna watu waongo. Uibe 17ml adu polisi wasiichomoe uishiwe
 
dah poleeee...uliwezaje fichaaa...manake nchi nilizotembelea hawatangazi kubadilisha fedha namaanisha fedha (sarafu na noti) zilizoko kwa mzunguku zaondoka zenyewe na mpya kuingiaaaa, yaani hawatangazi wala nini, siuku ukija bank na furushi wataanza kukumulika.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…