Nimemaliza taratibu zote September project hii

M-FINANCE

Senior Member
Joined
Aug 19, 2017
Posts
107
Reaction score
142
Ndugu zangu pole Na majukum pili pole kwa kuchelewa kwa ndege Yetu kule Canada, pili tusubiri makinikia,

Ila kama nilivyowaambia ninafungua project hii ni maalumu kwa mama ntilie Na watu wa magenge,
Sababu za kuwahusisha hawa ni kwamba wao wanapata hela kila siku Na pili ni watu wanaoitaji mtaji kuendeleza biashara zao,

Nimefurahi sana kuona proposal yangu imepokelewa vema,

Kwakuwa ni mwanzo ngoja nijilipue tu,

Nitadili Na kuwakopesha akina mama wa mahoteli madogo madogo, Na vijana wa uza genge,

Nimepata watu walio tiyari kupokea mkopo huu , idadi ni 37 nimeshawapata,

Mikopo Na aina ya urejeshaji

Mkopo wangu utakuwa Na riba ya 50% kwa mwezi Na viwango ni kama ifuatavyo

1. 50,000 anarejesha daily sh 2500 ndani ya mwezi mmoja

2. 100,000 anarejesha daily sh 5000 ndani ya mwsezi mmoja

3. 150,000 anarejesha 7500 daily ndani ya mwezi mmoja

4. 200,000 anarejesha 10,000 daily ndani ya mwezi mmoja


Nimefuata utaratibu wote wa usajili, Na nimepata kibali simple tu. Kodi muhim kulipa, sasa nipigane kufungua office niajiri kijana mmoja atakaye kuwa anazunguka kukusanya mrejesho hayo daily nadhan kamshahara ka 350,000 kanamtosha sana,


Zingatia siji kiholela kupigwa hela yangu, niko very strict. Lazima udhaminiwe, Na uweke kitu chenye thataman rehani,

Kwanini nimechagua aina ya urejeshaji uo?


1. Ni friendly haimuumizi mrejeshaji

2.dawa ya Deni ni kulipa taratibu kidogo kidogo sitaki madeni ya mkupuo yatakayoleta shida,

3. Mtu itamufanya awe Na uchungu wa kulipa yote maana makubaliano ni kwamba ukifeli kwa siku ndo mazima Mali yako imeenda hiyo,

4. Nimechagua hao KINA mama maana wanapata hela sana Na hawadhurumu,


Mungu hawabariki,

Jaman uwekezaji muhim
 
Mkuu mkopo wangu mwisho ni 200,000 ndo maan nkachagua hawa wasio Na presha Na ni majaribio, maana kuanza unatoa 4 nje alafu nikipigwa hiyo nne
Hapo kwenye miezi 16 ni errors, angalia nimesahihisha. Mkuu 200,000 ata ww mwenyewe ni ngumu kuiendesha labda kwa hizi biashara za dada zetu km mama ntilie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazo zuri mkuu.
Mimi nilishafanya biashara inayolingana na hizi lakini niliambulia hasara.
Ila nadhani kwa system uliyoweka ya dhamana,I think itasaidia kidogo japo hawatokosekana wasumbufu.
 
Umekurupuka....mara paaa! 50%

Fanya utafiti wa kutosha kabla ya kuwatoza hio 50%


Samsung Galaxy S8+
 
Mkuu mkopo wangu mwisho ni 200,000 ndo maan nkachagua hawa wasio Na presha Na ni majaribio, maana kuanza unatoa 4 nje alafu nikipigwa hiyo nne
Mkuu wewe huna nia njema na maskini.
Unataka kuwafanya watu wakimbie nyumba zao kwa madeni yasiyolipika.
 
Duuh mbona riba kubwa hivyo mkuu , na hicho kibali nani alikupa kwa riba hio umedeviate human right na unapaswa uhukumiwe kosa la kutaka kuwatapeli wananchi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahani mkuu mimi naomba kujua ni vibali gani hasa vinahusika kwenye hili. Ninafanya hii kitu japo kilocal sana na kwa watu wachache sana huku kwetu japo naifanya friendly sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu nani amekuruhusu kukopesha kwa riba ya 50%.
kwa kweli unaingeza maskini nchi hii haumsaidii mtu ila unadidimiza
 
Ungepiga na gharama za kufuatilia hayo marejesho pia
 
Mkuu riba yako ni kubwa sana, biashara ya hivyo inabidi iwe win win, ili kusudi na wao waweze kupata faida ili warejeshe hela yako bila usumbufu, fix riba then kila la heri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…