Nimemfuma mke wangu akiiba nyama jikoni

Mimi sioni sababu ya yeye kuonja mimi kinachonisibu ni kwanini atake kujificha?? si ageonja tuu mambo yaende?
Halafu mnavyosema kwetu hatuli nyama sio kweli nyama tunakukula pia tunachanganya na dagaa na samaki mambo yanakwenda.
 
kuna shida gani yeye kuonja mboga
Tena mke wako unayempenda
Kwa nini asienjoy vya mume wake
Au ulitaka akaonje nyama anayosupply mtu mwingine

Wanawake wa digitali kazi mnayo
Mungu awape nguvu
 
mh hakuwa na sababu za kudokoa alikuwa anakula kwani kuna ubaya gani...acha roho mbaya kijana mbona hilo ni jambo la kwaida sana...kwani wewe haijawahi kukukuta hamu ya kula kitu kilichopo jikoni baada ya kuhisi harufu nzuri ya chakula?
Mwanaume unagubu wewe.Aya kukiw na nyama au samaki ingia jikon mwenyew[emoji57]
 
Nashindwa kuamini kuwa na wewe ni MWANAUME mwenye mke na watoto!
Hii sio insu ya kuiweka kwenye mtandao wa kijamii UMETUFEDHEHESHA sana wanaume wenzako.
 
Dah!...Hivi mnajua huu mtandao tunausoma mpaka huku nchi za watu?...
 
Me sijaona tatizo la mke wako, maana yeye ndiye mpishi, halafu unabahati anakupikia daah!
Mwache bana, endelea kumpenda zaidi, kuonja muhimu.
Halafu kuna vitu ukivichukulia simple inakuwa poa sana,
yani kitu kama Nyama wengine huwa zinachosha, kwa kifupi achana na mambo madogo, kama mkeo anakupenda wala usiangaike na haya madogo, wewe komaa na mipango.
 
Wewe hapo unakosea, Sasa umeamua kumbana mpaka jikoni? Au unabana matumizi katika serikali yako ya nyumbani? Kwanza lazima ujue mwanamke yuko kazini(kukupa penzi) na a atakiwa ale vizuri, Sasa unataka akae legelege? Hata watoto kama wakiona mama yao anakula vizuri wakakuuliza mbona unampendelea, waambie huyu yuko kazini. Mimi kwenye suala la kula hata simbanii wifi yenu kabisa, nahakikisha anakula ili anipe matibabu Mazuri maana nilipomuoa nilimuajiri.
 
Acha kututia aibu bhana sisi wanaume wenzako, mambo ya kitoto hayo, kwaio we ulitaka asionje? Angekuletea linyama halijaiva ungesemaje? Mambo ya jikoni hayatuhusu.
 
Yaani kijinyama nusu kilo mtu anapika unamuwinda kiasi hicho? hivi kupika ukaonja ni issue? wewe ni mwanaume kweli? Eti mkeo anaiba una gubu wewe! mwanaume wa hivi bora pili pili

Madam umenichekesha mpaka basi asubuhi hii! [emoji14][emoji14][emoji14]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…