Nimemsikiliza Mbowe kuhusu Katiba Mpya, naunga mkono hoja ya kwamba amelambishwa asali

Nimemsikiliza Mbowe kuhusu Katiba Mpya, naunga mkono hoja ya kwamba amelambishwa asali

Daisam

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2016
Posts
2,625
Reaction score
3,141
Ndugu zanguni, nimemsikiliza Mh. alipokuwa akiwahutubia Wana Diaspora Marekani. Moja kati ya masuala aliyozungumzia ni Katiba mpya. Nilichotambua ni kwamba, kama tutatembea kwenye mawazo yake, Katiba mpya haitapatikana leo wala kesho. Labda kizazi kingine huko mbeleni.

Kwa sababu kila anapozunguza anasema tuvute subira. Kama ni kuvuta subira tumeshavuta sana tena sana.

Majibu ambayo yalitakiwa yajibiwe na Serikali kuhusu utaratibu na muda wa kuleta Katiba mpya, anayajibu yeye.

Yaani, anaitetea Serikali kwamba haiwezi kuanzisha mchakato wa haraka ili kuharakisha upatikanaji wa Katiba mpya. Mbowe hata akiambiwa Katiba mpya hadi 2040, yupo tayari.

Kama wanaweza kuhujumu mali za umma haraka haraka, kusaini mikataba ya ovyo haraka haraka, kuchukua tozo haraka haraka, wanashindwaje kuanzisha mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya?

Ifahamike kuwa, CHADEMA ndo walioshika Bendera ya Katiba mpya, lakini nyuma yao kuna Watanzania wengi sana wanaopenda mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya.

Serikali inahitaji Pressure ya hali ya juu sana ili iweze kukubali matakwa ya Wananchi.

Kwa hiyo, mimi naungana na J. Heche, T. Lissu na wengineo katika suala hili la Katiba mpya.
 
Mbowe apumzike, kwasasa tunahitaji hardliner kwenye mambo ya katiba mpya sio tuvite subira. Unavuta subira kwa lipi?. Makamba kaongea wazi kwamba kwa ccm katiba mpya sio issue. Sasa unavuta sibira kwa lipi.

Mbowe anadanganywa na maridhiano ya kijinga ambayo hayatafikiwa zaidi anachota akili mpka 2025 ndipo watazinduka walikuwa wanadanganywa.
 
Mbowe apumzike, kwasasa tunahitaji hardliner kwenye mambo ya katiba mpya sio tuvite subira. Unavuta subira kwa lipi?. Makamba kaongea wazi kwamba kwa ccm katiba mpya sio issue. Sasa unavuta sibira kwa lipi.

Mbowe anadanganywa na maridhiano ya kijinga ambayo hayatafikiwa zaidi anachota akili mpka 2025 ndipo watazinduka walikuwa wanadanganywa.
Asikupotoshe huyo mleta mada, Mbowe hajasema hivyo. Tafadhali msikilize kwa kina.



Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Ifahamike kuwa, CHADEMA ndo walioshika Bendera ya Katiba mpya, lakini nyuma yao kuna Watanzania wengi sana wanaopenda mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya.

Nimecopy hichi kipande cha statements yako hapa ili nikuulize lini ulikuwa nyuma ya CDM katika madhila yote waliyopitia?

CDM hawa wamesumbuka sana na CCM/KATIBA MPYA, familia zao zimeishi maisha magumu, Mbowe huyu kakaa gerezani wakati mimi wewe tukilala na wake zetu kwa raha mustarehe, hakuna jambo tumefanya kusaidia, zaidi tuliwatosa na kuona ni jukumu lao kupiga kelele.

Binafsi nasema hivi MITANZANIA sio ya kupigania, itakuacha unataabika yenyewe ina hangaika na upuuzi mitandaoni, hatujuagi masuala muhimu kwa Nchi, umenifanya nimkumbuke Mange Kimambi na maandamano yake, nani alisapoti hata kwa kuvaa tshirt? ni muda wetu Watanzania tunyooshwe labda akili zitakaa sawa.
 
Ndugu zanguni, nimemsikiliza Mh. alipokuwa akiwahutubia Wana Diaspora Marekani. Moja kati ya masuala aliyozungumzia ni Katiba mpya. Nilichotambua ni kwamba, kama tutatembea kwenye mawazo yake, Katiba mpya haitapatikana leo wala kesho. Labda kizazi kingine huko mbeleni.

Kwa sababu kila anapozunguza anasema tuvute subira. Kama ni kuvuta subira tumeshavuta sana tena sana.

Majibu ambayo yalitakiwa yajibiwe na Serikali kuhusu utaratibu na muda wa kuleta Katiba mpya, anayajibu yeye.

Yaani, anaitetea Serikali kwamba haiwezi kuanzisha mchakato wa haraka ili kuharakisha upatikanaji wa Katiba mpya. Mbowe hata akiambiwa Katiba mpya hadi 2040, yupo tayari.

Kama wanaweza kuhujumu mali za umma haraka haraka, kusaini mikataba ya ovyo haraka haraka, kuchukua tozo haraka haraka, wanashindwaje kuanzisha mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya?

Ifahamike kuwa, CHADEMA ndo walioshika Bendera ya Katiba mpya, lakini nyuma yao kuna Watanzania wengi sana wanaopenda mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya.

Serikali inahitaji Pressure ya hali ya juu sana ili iweze kukubali matakwa ya Wananchi.

Kwa hiyo, mimi naungana na J. Heche, T. Lissu na wengineo katika suala hili la Katiba mpya.
Nadhani huna masikio
 
IMG_20221212_104854.jpg
 
Hii mentality ya mleta mada inaonesha vile bado hatuko serious kama taifa kuhusu madai yetu ya Katiba Mpya, naandika kama taifa kwasababu sitaki kukihusisha chama chochote kwenye madai ya Katiba Mpya.

Chadema wenyewe hawatakiwi kuonekana ndio wapo mbele kila siku kuhusu madai ya Katiba Mpya, kwani hilo pekee linawapa kisingizio CCM wawaambie wananchi madai ya Katiba Mpya ni ya kisiasa, jambo ambalo sio kweli.

Lakini pia, bila kujali kama alichoandika mleta mada ni sahihi au vinginevyo, ila kwa kile alichoandika tu kinaonesha vile bado tumewekeza akili zetu kwa individuals ili watuwezeshe kupata Katiba Mpya, jambo ambalo naamini sio sahihi.

Kimsingi, inatakiwa tusiogope au kuhofia mawazo ya mwingine yeyote kuhusu madai ya Katiba Mpya, kinachotakiwa ni sisi tujue lengo letu na njia za kupitia ili kufanikisha lengo hilo, sio kila siku kusikiliza kwanza fulani anasema kitu gani kuhusu hitaji letu, hivyo tunazidi kukosea na kujichelewesha.
 
Katiba mpya ni tamanio la wananchi, ila ni mwiba mchungu kwa walamba asali............sasa kama mlamba asali ndiyo anatakiwa ku-initiate na ku-implement mchakato wa katiba mpya, what do you expect!?
 
CDM isimamie ahadi zake, isiwe kama Chama chakavu.

Walitoka kutuandaa Kwa mikutano na maandamano kuanzia NOVEMBER 2020.

Leo ni December.
 
Mbowe apumzike, kwasasa tunahitaji hardliner kwenye mambo ya katiba mpya sio tuvite subira. Unavuta subira kwa lipi?. Makamba kaongea wazi kwamba kwa ccm katiba mpya sio issue. Sasa unavuta sibira kwa lipi.

Mbowe anadanganywa na maridhiano ya kijinga ambayo hayatafikiwa zaidi anachota akili mpka 2025 ndipo watazinduka walikuwa wanadanganywa.

Kila siku nasema Mbowe ameshakata moto naona kuna watu hawanielewi.

Mbowe alistahili kukaa pembeni muda mrefu baada ya jaribio la kumpa Lowassa nafasi ya kugombea urais kushindikana. Hii kung'ang'ania uenyekiti ndio anafikia mahali kutaka maridhiano ya kitapeli.
 
Ndugu zanguni, nimemsikiliza Mh. alipokuwa akiwahutubia Wana Diaspora Marekani. Moja kati ya masuala aliyozungumzia ni Katiba mpya. Nilichotambua ni kwamba, kama tutatembea kwenye mawazo yake, Katiba mpya haitapatikana leo wala kesho. Labda kizazi kingine huko mbeleni.

Kwa sababu kila anapozunguza anasema tuvute subira. Kama ni kuvuta subira tumeshavuta sana tena sana.

Majibu ambayo yalitakiwa yajibiwe na Serikali kuhusu utaratibu na muda wa kuleta Katiba mpya, anayajibu yeye.

Yaani, anaitetea Serikali kwamba haiwezi kuanzisha mchakato wa haraka ili kuharakisha upatikanaji wa Katiba mpya. Mbowe hata akiambiwa Katiba mpya hadi 2040, yupo tayari.

Kama wanaweza kuhujumu mali za umma haraka haraka, kusaini mikataba ya ovyo haraka haraka, kuchukua tozo haraka haraka, wanashindwaje kuanzisha mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya?

Ifahamike kuwa, CHADEMA ndo walioshika Bendera ya Katiba mpya, lakini nyuma yao kuna Watanzania wengi sana wanaopenda mchakato wa haraka haraka wa kuleta Katiba mpya.

Serikali inahitaji Pressure ya hali ya juu sana ili iweze kukubali matakwa ya Wananchi.

Kwa hiyo, mimi naungana na J. Heche, T. Lissu na wengineo katika suala hili la Katiba mpya.
Mbowe ameisha kabidhiwa buyu la asali,usikute hata ela ya kwenda huko ulaya kalipiwa na hawa walamba asali,kwangu Mbowe nilimtoa kwenye akili yangu 2015 alivyobadili gia ya angani nilimwona ni mwasiasa ambaye ana malengo na msimamo kitu ambacho mwanasiasa akikikosa huyo anakuwa Sio mwanasiasa bali mganga njaa.
 
Mbowe awapuuze wanaosema hivyo. Asali ni muhimu sana kiafya. Unapoipata ilambe.
 
Katiba mpya ni mwakani watanzania kuweni na amani na Mbowe anaongea anachokijua.Mchakato wa katiba mpya unaanza mwakani .
 
Back
Top Bottom