Nimenunua luku unit 0.5KWH kwa shilingi 1200/=, picha inaeleza

Lexus SUV

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2016
Posts
4,493
Reaction score
5,591
Dah, haya ni majanga aisee, kwa kutumia tigo pesa muda huu nimenunua unit 0.5KWH kwa 1,200/ aisee. Hivi hii ni shida gani tena?! Sms ya mwisho inaelezea ufisadi huo wa unit 0.5KWH kwa shilling 1200 aisee, sina jinsi najiuliza tatizo nini?
 
Makato ya mwezi buku
 
Pesa ndogo sana hio mkuu,angalau ikifika tsh.25,000 unapata 1/4 unit ndipo itakua sawa.

Kua mzalendo mkuu.Nasema uongo ndg zanguuuuuuuuuuuuu?
 
Hiyo ni sawa, kiuhalisia umenunua umeme wa shilingi 200 sawa na unit 0.5, shilingi 1000 inakatwa kwenye kila Luku kwa mwezi. Sitetei hili swala ila halijaanza leo, lina miezi kadhaa nyuma ni vile umekurupuka huku bila hata kumuuliza hata mkeo au jirani akufafanulie.
 
Buku miambili kweli?

Dah
 
H
WAMECHUKUA BUKU YAO MBANA HILI NI HALALI TU NA TUMESHALIZOEA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…