Nimenusurika kuambukizwa HIV na mwanachuo wa miaka 24 ambaye yupo kwenye mission ya kulipiza kisasi

Nimenusurika kuambukizwa HIV na mwanachuo wa miaka 24 ambaye yupo kwenye mission ya kulipiza kisasi

Execute

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
3,000
Reaction score
7,336
Huyu binti nilifahamiana naye kupitia mtandao wa LinkedIn akiwa anatafuta field. Baada ya muda tukawa tunachati kwa karibu na hatimaye mahusiano.

Kwangu mwanamke yeyote akija kimapenzi lazima kwanza tupime. Yaani ukiingia tu mlangoni unakutana na 'pharmacy' yangu, unapima ndipo uingie.

Binti kafika pale na ndio ilikuwa mara ya kwanza kabisa kumuona. Awali kwa siku kadhaa alikuwa anakataa kuja home akitaka tukutane sehemu nyingine. Nilipokubali akajifanya amebadilisha kwamba ananiamini hivyo atakuja tu home.

Nikamwambia haya tupime akaanza kujizungusha akasema tukae tu tuangalie movie. Kwenye maongezi yetu siku za nyuma alisema alipima mwaka uliopita na yuko poa.

Basi nikasema isiwe kesi, kaa hapo. Kumbe mpango wake ni kuninasa nimle baadae akishanitega. Tumekaa pale kama saa zima kisha nikaanza kumgusa. Nikaona na yeye anakubali. Taratibu tukaendelea kushikana na mwishowe nguo tushazitoa.

Hapo sasa nikamwambia kwasababu tupo ready hebu tupime kisha tuendelee ndipo binti kashtuka na kukataa. Nikamwambia unaniamini niingie hivyo hivyo akasema 'wewe tu'.

Hapo niliamka faster nikawahi bafuni kuoga kwa dettol na kupiga mswaki. Tayari nilikuwa nimeshamshika sana na alikuwa ametoka kumaliza period. Nilikuwa nishafanya romance zote mpaka kunyonya maziwa.

Nikarudi pale na kumwambia avae na kuondoka. Hapo faster nikamcheki jamaa yangu daktari anipatie pep nianze dozi ya haraka. Nimekunywa vidonge siku 28 na nilikamilisha wiki mbili zilizopita.

Sasa bwana yule binti akaanza kunitafuta baada ya siku tatu akijifanya anajutia. Akawa anaandika kwamba alichofanya ni Mungu tu anayeweza kumwelewa. Nikasema ni kitu gani? Akasema akiniona ataniambia.

Kumbe anajua yakipita masaa 72 unakuwa umeupata hivyo hata pep hazifanyi kazi. Anakutafuta ili ujue kwamba amekuambukiza. Alionesha kushtuka na kuwa disappointed baada ya kumuonesha kopo la pep.

Basi nikamwambia tuonane mahali na kweli akaja. Akaniambia yeye ni muathirika na aliambukizwa miaka minne iliyopita. Pia akasema yeye kwa sasa mwanaume yeyote atakayemtongoza anakubali kulala naye. Anasema aliambukizwa kwa makusudi hivyo naye lazima alipize kisasi.

Huyu binti alitokea huko kanda ya ziwa na alikuja Dar kusoma kuanzia certificate na sasa yupo mwaka wa tatu degree. Anatoka familia masikini hivyo alipofika Dar maisha yakawa magumu akajirahisisha kwa wanaume.

Ndugu zangu kuweni makini sana maana yupo anatembea kila kiwanja kuusambaza. Jina lake linaanzia na G na linaishia na A.

Nimepima vipimo viwili kwa mpigo niko poa. Picha hapa chini.

Screenshot_20230520-114120.jpg
 
Ila we mwamba una msimamo, mimi ningekuwa nimeshaambukizwa tayari. Yaani demi nimchezee, amelainika halafu, nimeshadindisha, halafu naanza kuleta issue za maabara? Huo msimamo sina aiseee na nina bahati sijakutana na demi aliye +.
Muongo huyu, kaka kama hajala Kwa Nini apaniki?? Eti alimshika tu
20220615_214454.jpg
 
Hivi dettol si anti bacterial? Ama inaua na virus?

Anyway, huyo anapaswa kuwajibishwa kwa kosa la kuambukiza Ugonjwa kimakusudi.

Nakushauri umripoti katika kituo cha afya kitengo cha CTC, watajua namna ya kumuwajibisha.

Wewe umepona, je ni wangapi wataugua? Wengi. Inaweza isikupate wewe, ila makusudi yake ikampata baba yako au nduguyo wa karibu na mwishowe zigo litakuangukia pia kwa namna moja ama nyingine.
 
Back
Top Bottom