Nimenyimwa hati ya eneo ninalolimiliki

Moseley

Senior Member
Joined
Jul 10, 2010
Posts
187
Reaction score
98
Habari wana JF?

Kama kichwa cha habari kinavojieleza.

Kwa ufupi ni kwamba, naombeni msaada wa kisheria juu ya jinsi ya kupata hati ya eneo la zaidi ya hekari 18 ninalolimiliki kiasilia.


Nimekua katika harakati za kuyapatia hati maeneo ambayo ninayamiliki miaka nenda rudi. Maeneo hayo nimekua nikiyatumia kwa kilimo toka miaka ya zamani.

Kipindi cha nyuma babu yangu alikua anamiliki hilo eneo ambalo alimpatia baba angu sehemu ya eneo hilo ambalo kwa sasa ndo ninalolimiliki.

Mabwana ardhi wananambia sitaweza kupata hati ya maeneo hayo yenye zaidi ya hekari 18.

Naomba msaada wa kisheria, nifanyeje ili nipate hati ya miliki ya maeneo hayo?

Ni muda sasa nafatilia ila naambiwa sitaweza kupata kwa sababu eneo hilo lipo kwenye mpango mji. Sasa, eneo likiwa kwenye mpango mji maanake miliki asilia naikosa? Na kwa nn niikose haki yangu wakati maeneo hayo nayamiliki kihalali na hayana mgogoro wa aina yoyote ile?
 
Hujasema ni Eneo hilo shamba lako lipo
Maelezo yaliyofuata unadai kuwa kutakuwepo na mipango Miji
Ni kwamba kwa Ardhi yoyote hapa TZ ipo chini ya Rais na Hati miliki zimegawiwa katika Umiliki wa miaka 33, miaka 66, na miaka 99 kuanzia utakapoomba.
Km utakuwa Mjini au Jirani na Mji tambua kwamba Mji unapanuka kila siku hivyo kukuta wewe mwenye Ekari 18 haitachukua miaka 5
Kwa vile hiyo ardhi ni ya kulima tu na ndivyo mnavyoitumia litakapofikia hatua ya kupanuliwa kwa Mji wataangali Hati Miliki yako km ipo wataisubiri iishe na hawatakupa ingine kwa hiyo sehemu hiyo wanaweza kukuruhusu uwauzie wananchi wajenge nyumba au Serikali iichukue kujenga Mji, Hospital Vyuo nk
Nakushauri uombe Hatimiliki ya Kijiji kwa ajili ya Kilimo na wakupimie km upo Kijijini lakini km upo Mjini naona wapo wataalam humu JF watakufafanulia ni vipi upate Hati miliki ya miaka 99 Ujenge Chuo? au
 

Eneo halipo mbali na mjini. Nataka kupata hati ya kumiliki eneo hilo. Kwa sababu liko karibu na mji, niko tayari kuuza sehemu ya eneo hilo.

Kwa maana hiyo, nataka eneo lipimwe na nipate hati ya kumiliki. Kuliko hivi sasa, eneo halijapimwa na sina document yoyote kuthibitisha kuwa eneo hilo ni langu zaidi ya miliki ya kiasili.
 
Nakupa SIRI nenda kalikopee mkopo wa muda mrefu Bank yoyote ni lazima watakwambia wapelekee Hati miliki sasa hapo Nenda Hatimiliki Wizara ya Ardhi waambie nataka kukopa na Dhamana ni Shamba ekari 18
ardhi yote sasa ipo katika Google (GPS) ukiitafuta kwenye Google Earth utaiona na watakuandikia na kukuchorea kwa vile ni mkopo watakusaidia kukugharamikia
Hujasema liko wapi huenda hapo kuna Wawekezaji (au EPZ) watakusaidia
Bado wataalamu wataingia kukusaidia km si kwa mikopo ufanyeje
 
Sijakuelewa, hawajakupatia hiyo hati; wametoa sababu zipi za kutokukupatia hati hiyo?
 

Kama eneo liko kwenye development plann wizara haiwezi kufanya hicho unachomweleza cha kufanya aende local authority kwa mfano km kiwanja kipo kigamboni aende manispaa ya temeke apeleke maombi ya kupatiwa eneo hapo mradi utakapokua implemented lakini inategema kama map inasemaje cz kuna uwezekano kwenye ramani eneo lake likawa ni shule, soko, au hospitali hapo huwezi patiwa katika ardhi yako wataangalia eneo lingine la makazi ambapo utapatiwa sizable plot kulingana na mgawanyo wa viwanja vya makazi na mara nyingi vinakua vimepimwa kwa gharama yako mwenyewe around laki 3..
 
Tafuta kampuni ya wapimaji ardhi binafsi wakupe ushauri nini cha kufanya ili uweze kumiliki eneo km shamba au viwanja tena ufanye mapema watu wa mansipaa sio wema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…