Nimeomba mkopo wa Tsh 1,500,000/= kutoka taasisi moja hapa nchini ambao riba yake ni 17%. Nimeweka dhamna kiwanja. Hivyo basi, nimeingiziwa huo mkopo ambao inatakiwa niulipe kwa muda wa miezi 6 ambapo kila mwezi inatakiwa nilope 300000. Lakini baada ya kuingiziwa pesa hiyo, nimeambiwa ni-deposit kwanza amana ya Tsh 202,500/= ambayo nitakuja kuichukua mwishoni baada ya kumaliza kurejesha huo mkopo. Kwa maana hiyo, kiasi nilichopata ni Tsh 1,300,000/=
Sasa jamani, naomba mnisaidie kukokotoa hapa. Je, huu mkopo una riba ya asilimia 17 kweli? Naomba msaada wenu