Kila wakati nasisitiza umuhimu wa kusali vizuri kabla ya kulala na mara baada ya kuamka. Kamwe usilale kabla ya kusali na kujiweka chini ya ulinzi wa Mungu wewe, familia yako na mali zako! Kamwe!Ni juzi kati nilikuwepo Gesti Fulani na Dar na kabla ya kulala nilihesabu hela nilikuwa na 50000/=.
Nilipopatwa na usingizi mzito niliota mtu Fulani anakuja ananiambia nimpe hela zangu na nikampa yeye akanipa kitu kingine sikikumbuki.
Sasa nilivyoamka asubuhi natafuta Ile 50000/= sikuiona Tena Kila sehemu niliyosachi.
Sahivi naogopa hata kutoa hela benki nikakaa nazo.Jana pia Nimeota Nampa mtu hela kama makubaliano Fulani.
Spiritualist wa Jamii Forums NAOMBA mnitafsirie.