Nimepata Dv 1 ya 14 na Kazi yangu ya Houseboy inanilipa...

Nimepata Dv 1 ya 14 na Kazi yangu ya Houseboy inanilipa...

yutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2013
Posts
1,668
Reaction score
1,017
Habari zenu wakubwa na wadogo, siku ya trh 22,2 ilikuwa ni siku ya furaha kwangu baada ya kupata matokeo yangu ya kidato cha nne na kufaulu vizuri. Nilipowajulisha walezi wangu kuhusu hayo matokeo waliniwekea kikao na kuniamuru niende haraka huko Makete (Lupila).

Baada ya kufanya mtihani mwaka jana nikaona nitafute temp work ndipo nilipofanikiwa kukutana na hawa wazungu nilipowaeleza shida yangu wakaniambia wao hawana nafasi ya kazi labda kama nitaweza kuwasaidia kufanya shughuri ndogo ndogo za nyumbani kama kuchota maji kupiga deki na kuwapikia chakula kutokana ugumu wa maisha hapo kijijini bila kinyongo ilinilazimu kufanya hivyo kwa ujira wa laki moja kwa mwezi na nilifanyanao kwa mwezi mmoja wakawa wanahamia Dar kwani project yao ilikuwa imeisha na kuja hapa Dar kusubilia majukum mengine ya kupangiwa na shilika lao,

Kwa jinsi nilivyofanya nao kazi walitokea kunipenda sana na wakaniomba niendelee kukaa nao na hapa sikuwa na yoyote zaidi kula na kulala labda nijitolee mimi mwenyewe kuwasaidia wabongo wenzangu niliowakuta kwani sikubweteka hata kama nilikuwa napata posho kila wiki na kwasababu. Hapa Dar sio mwenyeji kwahiyo siwezi fanya biashara yoyote na isitoshe hapa nyumbani ni geti kali (Masaki) unatoka kwa maandishi unarudi na kusaini.

Nikaona hicho kidogo nikipatacho ni bora nitume nyumbani wanilimie mashamba kinachosalia kiwasaidie hapo nyumba lakini cha kushangaza toka nianze kuwasaidia hivyo vijisenti na wanandugu kunikalia kikao wamesema uwezo wa kuendelea kunisomesha haupo na sasa wanataka kula matunda yangu na nisiendelee kusoma kwani nikifika chuo kikuu ajira hamna. Na mara kaka yao amewachia mzigo mkubwa wa kunitunza mimi na wadogo zangu ilihali watoto wao wameishia kuuza ulanzi.

My take ni kwamba wafadhili wangu wako tayari kunisaidia na kuna uwezekano wa kumalizia project yao Ghana ya miezi 6 warudi finla
 
Unaweza kujisikia salama sana katika bwawa ulilopo, lakini kama hujajitosa nje ya hapo, kamwe huwezi kujua kwamba kuna kitu kama bahari. Kuendelea kushikilia jambo ambalo ni zuri kwa sasa inaweza kuwa sababu ni kwa nini hauna kitu kizuri zaidi
 
Wamedai tutaenda ghana baada ya project yao kuisha miezi 6 tutaenda nao finland kila kitu itakuwa juu yao na kwa kuanzia fungu likitoka watanipa mil 5 kwa ajili ya wazazi walezi nyumbani sasa nimebaki njia panda sijui niende majuu au nikomae hapa hapa bongo na mil 5 itanisaidia mpaka nimalize form six na naona nikijiongeza kwenye biashara na masomo si ntapotea ushauri wenu tafadhali
 
Wamedai tutaenda ghana baada ya project yao kuisha miezi 6 tutaenda nao finland kila kitu itakuwa juu yao na kwa kuanzia fungu likitoka watanipa mil 5 kwa ajili ya wazazi walezi nyumbani sasa nimebaki njia panda sijui niende majuu au nikomae hapa hapa bongo na mil 5 itanisaidia mpaka nimalize form six na naona nikijiongeza kwenye biashara na masomo si ntapotea ushauri wenu tafadhali

Rudi shule mdogo wangu
 
Unaweza kujisikia salama sana katika bwawa ulilopo, lakini kama hujajitosa nje ya hapo, kamwe huwezi kujua kwamba kuna kitu kama bahari. Kuendelea kushikilia jambo ambalo ni zuri kwa sasa inaweza kuwa sababu ni kwa nini hauna kitu kizuri zaidi

Mbona bado umeniweka njia panda tango poli nahitaji msaada niende na hao wazungu au nibaki?
 
Nenda shule wewe what if iyo safari ikafa na shule ukawa umechelewa think twice.
 
Shule haina mwisho dogo na shule ni popote kama uwezo wa akili uko vizuri!
Nenda mbele kwanza dogo, ili kwa sasa amua unataka kuwa nani kitaaluma.
sawa LUCKY BOY?
 
Kama wazungu hao wanakupenda kwa dhati watakushauri uendelee na shule.

Hata kama wanaosoma wengi hawapati ajira kama uambiwavyo na wengine, lakini shule si kwa ajili ya ajira rasmi tu - bali kukupanua mawazo ili uje kupambana na maisha vizuri zaidi.
 
Me nahisi ao wazungu Kama utawaeleza basi watakusaidia but usione unapata laki moja ukaona nyingi huku nje haikutoshi ata kidogo
 
Hata mi ishanitokea nilipomaliza form four bt mi niliamua kwenda shule wao wakarud USA.Ada wamenilipia kuanzia 4m4 mpaka sasa nipo chuo kikuu nalipiwa,Na BOOM navuta.
 
Ila wee dogo mbona unaonekana una akili kuliko elimu uliyonayo!!!!!

Hali uliyonayo kweli ni mtihani,ila ukitulia na kutumia akili ulizonazo utapata jibu.

Ni kweli ajira nazo ni changamoto ya ukweli,usije ukajutia baadaye.
 
Elimu haina mwisho,dogo nenda mbele ishu ikibuma utarud bongo kupga msuri cha msingi credt za kupga hata private candidates unazo...shikilia kama kupe au mbu anavonyonya dam hizo chance kwa weupe n adimu!
 
Mdogo wangu umepata bahati ambayo unatakiwa kuitumia kwa umakini,kiasi ambacho usije kujutia mbele ya safari.Cha msingi waeleze ukweli hao wazungu umefaulu vizuri masomo yako na utapangiwa kuendelea kidato cha 5 kwa shule za BONGO,Na walezi waliokuwa wanakusomesha wamekataa kukulipia masomo ya kidato cha tano na sita hata ngazi ya chuo.Kwa vile hawa ndugu zetu ni waelewa watakuelewa na kukusaidia kwa moyo mmoja.Pili utakapopata huo msaada usibweteke A-Level,soma kwa bidii na kujituma huku ukimtanguliza MUNGU,usijjingize kabisa ktk starehe,HAKIKISHA MALENGO YA KWENDA CHUO KIKUU YANAFANIKIWA.Tatu.Hao wazungu jitahidi usipotezane nao endelea kuwa in touch nao.Jitahidi kuwa mwema kwao,Hakika mdogo wangu utafika mbali kimaisha.ALL THE BEST
 
kaweke heshima nenda mbele kale upepo bongo shombo
 
Back
Top Bottom