Nimepata Mtaji wa TZS 20Mil, nataka mawazo mbadala ya Biashara

joniee

Member
Joined
Mar 13, 2013
Posts
35
Reaction score
14
Hivi karibuni nimepata mtaji wa takribani Mil 20. Nimekuwa nikipanga kuanza biashara ya electronics kama vilivyotajwa hapa chini, changamoto inayoniogopesha ni mamlaka za serikari kuhusu vibali na ushuru na ubora wa wazo lenyewe. Naombeni ushauri nini nizingatie, nini niongeze kwenye list au kipi nibadili
  1. Simu zenye thamani ndogo
  2. Earphones/Head phnones
  3. Phone covers
  4. Screen protectors
  5. Wireless speakers
  6. Batteries
  7. .......
 
Hamna kazi ngumu kama kupanga mipango huku hela unayo mkononi.

Wasiliana na kampuni za vinywaji kisha waombe muongozo wa namna ya kua wakala wao kwa kufungua depot yako mwenyewe.

Nahisi kwa 20M utaanza na simu chache kidogo. Na pia ununuaji wa simu kwa waTz unajulikana ni slow sana.
 
Hili nalo wazo zuri, ngoja nifatilie PEPSI kumekaaje nina mtu namfahamu
 
Tatizo linaanzia hapo. Hujui biashara unayotaka kuifanya na unataka ushauri toka kwetu. Hilo ni kosa kubwa. Ushauri wangu ni kwamba
1. fanya utafiti wa biashara ambayo nafsi yako inapenda ufanye
2. jaribu kuwasiliana na watu ambao hivi sasa wanaifanya biashara hiyo na
changamoto zake
3. Tafuta eneo zuri na salama kwa biashara yako
4. Tengeneza ka business plan kako ili uwe na dira
5. Hakikisha unakata leseni ili usije bughuthiwa
6. Weka rekodi ya mapato na matumizi kwa kuhifadhi risiti ya gharama zozote zile ambazo utazitumia kwenye biashara [hata risiti ya taxi]
7. Wekeza siyo zaidi ya 50% ya mtaji ili uwe na buffer
8. Tafuta mtu au jifunze basic book keeping skills ili iwe rahisi kwa TRA kukufanyia tathmini.
 
Twende pole pole mkuu, hizo 20M za mtaji umezipataje? Kama ni kwa biashara endelea kuikuza hiyo hiyo biashara iliyokupatia hizo pesa badala ya kuanzisha biashara nyingine. Otherwise unambie chanzo cha mtaji wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…