Nimepeleka mgonjwa usiku Zahanati ya Kitunda, Daktari anasema hawafanyi vipimo siku za Wikiendi Usiku

Nimepeleka mgonjwa usiku Zahanati ya Kitunda, Daktari anasema hawafanyi vipimo siku za Wikiendi Usiku

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
WhatsApp Image 2024-11-24 at 09.14.49_1ea6b7eb.jpg
Usiku wa kuamkia leo Novemba 24, 2024 nilifika kwenye Kituo cha Afya ambacho ni Zahanati ipo Kitunda (Dar es Salaam), palepale Kitunda Mwisho ambapo Dadalada zinageuka.

Nilipofika hapo wameandika huduma zao zinatolewa kwa saa 24, nilimpeleka Mtoto wangu ambayo alikuwa anachemka sana, nikaamini nitapata huduma ya haraka.

Nilikuwakuta wahudumu wapo wakiwemo wale wa manesi wa mapokezi n ahata daktari pia, lakini kilichonishangaza ni kuwa waliniambia hakuna huduma ya vipimo.

Sasa nikajiuliza wao wanafanya nini muda huo kama wako hapo Saa 24 na hawana huduma ya vipimo, inamaana mgonjwa anapofika wanampaje huduma kama hawana hata mchakato wa upimaji.

Nilipohoji hivyo nikajibiwa kuwa wikiendi hasa husiku huwa hawana huduma ya kufanya vipimo, nikahoji hivyo wao wanafanya nini hapo au wanawatibu vipi wagonjwa muda wa usiku? Sikupata jibu.

Natoa wito kwa Serikali hasa Wizara ya Afya kuangalia hivi vituo vyao vidogo, kama wanatambua ni sehemu ya kupata huduma ya kwanza kabla ya kwenda hospitali kubwa, siku tatu za wikiendi kwa maana Ijumaa, Jumamosi na Jumapili usiku hakuna huduma ya vipimo, hilo ni tatizo tena tatizo kubwa.

Vituo vidogo vipewe uwezo wa kuwa na vipimo hadi usiku au kama ni uzembe wa hicho kituo hatua zichukuliwe, kwani watu wengi wanaweza kupata madhara makubwa kwa kuwa tu kituo cha karibu kama hicho hakina huduma ya upimaji.
WhatsApp Image 2024-11-24 at 09.14.49_a6f4abd5.jpg
 
Usiku wa kuamkia leo Novemba 24, 2024 nilifika kwenye Kituo cha Afya ambacho ni Zahanati ipo Kitunda, palepale Kitunda Mwisho ambapo Dadalada zinageuka.

Nilipofika hapo wameandika huduma zao zinatolewa kwa saa 24, nilimpeleka Mtoto wangu ambayo alikuwa anachemka sana, nikaamini nitapata huduma ya haraka.

Nilikuwakuta wahudumu wapo wakiwemo wale wa manesi wa mapokezi n ahata daktari pia, lakini kilichonishangaza ni kuwa waliniambia hakuna huduma ya vipimo.

Sasa nikajiuliza wao wanafanya nini muda huo kama wako hapo Saa 24 na hawana huduma ya vipimo, inamaana mgonjwa anapofika wanampaje huduma kama hawana hata mchakato wa upimaji.

Nilipohoji hivyo nikajibiwa kuwa wikiendi hasa husiku huwa hawana huduma ya kufanya vipimo, nikahoji hivyo wao wanafanya nini hapo au wanawatibu vipi wagonjwa muda wa usiku? Sikupata jibu.

Natoa wito kwa Serikali hasa Wizara ya Afya kuangalia hivi vituo vyao vidogo, kama wanatambua ni sehemu ya kupata huduma ya kwanza kabla ya kwenda hospitali kubwa, siku tatu za wikiendi kwa maana Ijumaa, Jumamosi na Jumapili usiku hakuna huduma ya vipimo, hilo ni tatizo tena tatizo kubwa.

Vituo vidogo vipewe uwezo wa kuwa na vipimo hadi usiku au kama ni uzembe wa hicho kituo hatua zichukuliwe, kwani watu wengi wanaweza kupata madhara makubwa kwa kuwa tu kituo cha karibu kama hicho hakina huduma ya upimaji.
Mama ana tosha.......
 
Ccm mbele kwa mbele, kutaka huduma ya kitabibu usiku ni kiherehere, usiku ni muda wa mapenzi.
 
Aliweka baadhi ya sehemu za kutokea afya kuwa chini ya tamisemi alihribu sana ,,huduma zinazotolewa under tamisemi ni mbovu mnooo Bora uende Kwa mganga
 
Machawa kazi yao kusifia utawala tu na kuuabudu, vitu vya msingi hawawezi kuhoji mpaka raia wa kawaida waviibue ! Sad !
 
Usiku wa kuamkia leo Novemba 24, 2024 nilifika kwenye Kituo cha Afya ambacho ni Zahanati ipo Kitunda (Dar es Salaam), palepale Kitunda Mwisho ambapo Dadalada zinageuka.

Nilipofika hapo wameandika huduma zao zinatolewa kwa saa 24, nilimpeleka Mtoto wangu ambayo alikuwa anachemka sana, nikaamini nitapata huduma ya haraka.

Nilikuwakuta wahudumu wapo wakiwemo wale wa manesi wa mapokezi n ahata daktari pia, lakini kilichonishangaza ni kuwa waliniambia hakuna huduma ya vipimo.

Sasa nikajiuliza wao wanafanya nini muda huo kama wako hapo Saa 24 na hawana huduma ya vipimo, inamaana mgonjwa anapofika wanampaje huduma kama hawana hata mchakato wa upimaji.

Nilipohoji hivyo nikajibiwa kuwa wikiendi hasa husiku huwa hawana huduma ya kufanya vipimo, nikahoji hivyo wao wanafanya nini hapo au wanawatibu vipi wagonjwa muda wa usiku? Sikupata jibu.

Natoa wito kwa Serikali hasa Wizara ya Afya kuangalia hivi vituo vyao vidogo, kama wanatambua ni sehemu ya kupata huduma ya kwanza kabla ya kwenda hospitali kubwa, siku tatu za wikiendi kwa maana Ijumaa, Jumamosi na Jumapili usiku hakuna huduma ya vipimo, hilo ni tatizo tena tatizo kubwa.

Vituo vidogo vipewe uwezo wa kuwa na vipimo hadi usiku au kama ni uzembe wa hicho kituo hatua zichukuliwe, kwani watu wengi wanaweza kupata madhara makubwa kwa kuwa tu kituo cha karibu kama hicho hakina huduma ya upimaji.
Kama haiwezekani kupatiwa vipimo usiku basi waweke tangazo hapo nje,tunatoa huduma msaa 24 ila wikiend kuanzia usku hakuna huduma ya vipimo tunatibu tu kwa kuhisi...
 
Nilisoma/ kusikia pahala..kwa mujibu wa Mwongozo wa utoaji huduma..Zahanati hutoa huduma asubuhi hadi saa Tisa..jumatatu hasi Ijumaa.
 
Back
Top Bottom