Nimependa Machawa Wote Kuitwa "Wabeba Usaha"

Nimependa Machawa Wote Kuitwa "Wabeba Usaha"

the power

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2012
Posts
407
Reaction score
799
Usaha ni uchafu, usaha unanuka, usaha unaumiza na kuleta maradhi mengi, usaha unasambaa mwilini pindi husipotibiwa na kibaya usaha unaweza kukuua na kukumaliza kabisa. Dawa ya kwanza ya usaha ni kuutoa, kuukamua (Curratage and Dilatation) ndipo unaendelea na antiobitics, kutumia antibiotics penye usaha wa kutosha hakuwezi kuuondoa usaha tena ni kama kutengeneza bomu linalochimba ndani kwa ndani siku likilipuka ni shimo, kukatwa mguu, kukatwa mkono au kiungo chote au kifo.

Ili uwe chawa mzuri lazima ukubali kunuka tena vibaya sana, lazima uweze kuumiza wengine bila kujali, lazima chawa uwe tayari kuua (character assassination) wengine kwa faida ya boss. Suala la aibu liweke kando, suala la personality weka mbali, suala la heshima lisiwe suala lako kabisa. Eti binadamu inabidi utumie akili na common sense, ili uweze kuwa chawa kindakindaki nakwambia hakuna cha kutumia akili na common sense, tena the opposite is true, matendo yako lazima yawe ni ya kujitoa akili na common sense.

1718267248722.png


Ili uwe chawa husijali elimu yako , uchawa hauna kiwango cha elimu, hasiye na elimu, primary school leaver, degree, graduates wa masters, PhD hata professors tunaona wanafanya matendo ya uchawa. Yalabi!

Ebu fikilia chawa anasema" umenitoa jalalani" wakati alikuwa mkuu wa kitengo cha sheria chuo kikuu. Fikilia chawa anasema "Ukioondoa manabii Yesu na mtume Muhamadi Mama Samia ndiye anafuata" . Chawa mwingine akajitoa akili kabisa na kusema "huyu boss ningekuwa mwanamke ningemruhusu anioe bure" na "niko tayari kumfanyia chochote atakachoniambia" Toba Yalabi chochote, are you serious?

Kibaya zaidi chawa wengine wanafikia hatua ya kujitoa akili, kujifanya mabwege na punguani kabisa eti chawa anasema "Napenda kuanza kwa kutoa shukurani zangu za dhati kwa Mh Mwendazake- Mungu" Kweli kabisa binadamu unamuita Mungu tena kwenye public na husiniambia was a typo, hayo ni matamshi , na husiniambie kuchapia, muunganiko wa neno Mungu hapo haliwezi kuchapika kibaya mzungumzaji ni mtaalamu mzuri na mahili wa public speaking na ni mzuri wa lugha ya kiswahili. Kwa hiyo this was an intentional act, purposefully done , with prior meditation before selection of word "Mungu" kama kielezi cha sifa cha Boss wake.

As if maneno hayatoshi, ili uwe chawa kamili lazima uonyeshe heshima na adabu ya hali ya juu, heshima ya the highest level of highness, king of the Kings, the majesty; heshima ya utumwa tena mbele ya kadamnasi na mbele ya Boss (sasa atakuonaje ulivyojidhalilisha kwake), ni lazima ifanyike kwa vitendo huku ukiwa mkavu na macho pevu, mfano lazima huiname na kuchuchumaa, umfunge kiatu boss hata kama kamba zimefungwa, fungua kamba na kufunga tena mbele ya Kamera" hiyo ndiyo heshima ya utumwa unayotakiwa kufanya. Chawa mwingine alifikia hatua ya kulamba miguu tena huku akirekodiwa akisema na kutenda "Kwa heshima zote, ngoja nikulambe miguu bosi wangu naweza ambulia chochote"

1718267400704.png


Hakika machawa ni wabeba usaha, ni lazima ukubali kubeba usaha, kuadhirika, kusononeshwa, kunuka kinyesi ili utoboe na kuqualify kama chawa. Najiuliza hivi kizazi chetu cha vijana wako tayari kuwa wabeba usaha, kwa maana ndiko tunakoelekea huko, baada ya machawa wachache kujidisplay kwamba wameyaweza , wamefanikiwa kimaisha kupitia uchawa ingawa wachache tunajua wamepita wapi nyakati za kiza mpaka wakapata kidogo hicho, na uchawa wanaodisplay ni cover up tu.

Cha kujiuliza na cha kuumiza ni kuhusu haya matendo yao, je hawa jamaa wanatengeneza precedence gani kwa watoto wao wa kiume na kike? haswa wa kiume kwani mwanaume lazima uwe ngangali na uwe mtu wa misimamo ya kiume, simaanishi wanawake wawe machawa. Kwanza nashangaa machawa wengi kuwa wanaume. ni Taswira ipi wanaitengeneza kwa jamii yao. Jamani Ifike mahali turudi kwenye maadili yetu ya mila na desturi.

Nashangaa kwa nini machawa hawakemewi tena wanafanya uchawa wao hadharani na uchawa umekuwa fashion sasa, kwani principal mojawapo ya chawa lazima matendo yako ya kipuuzi yawe recorded na yafanyike hadharani. Ni ukweli husipingika ukishakuwa na taifa la machawa, taifa hilo linaelekea kuhangamia.
 
Ni zaidi ya usaha na ushuzi kimsingi ni wafu tu kwa jina lingine, damn unawezaje kumfanaisha mwanamke anayeblidi kila mwezi na mitume wa mwenyezi Mungu? tumefikishwa mahala pabaya sana na siisiiemu.
 
Uchawa iishakuwa ajira ila ubaya ni kwamba unajidhalilisha

Umasikini siyo dhambi ila siyo jambo jema
 
Fisiemu ndio wameleta madhira yote haya. Kusifia sifia kiumbe chawa amezaliwa sshv unakutana na libaba lizima lina mke na watoto lichawa. Kama limwijaku au libabalevo
 
Ni zaidi ya usaha na ushuzi kimsingi ni wafu tu kwa jina lingine, damn unawezaje kumfanaisha mwanamke anayeblidi kila mwezi na mitume wa mwenyezi Mungu? tumefikishwa mahala pabaya sana na siisiiemu.
Do wewe jamaa umeua kabisa, do.......nilifikiri mimi ndio nina hasira,ila wewe mwenzangu hasira zako zimezidi
 
Soon Machawa watapitisha azimio kuwe na Kitivo cha Uchawa Pale Chuokikuu,Yaani unaondoka na degree yako ya Uchawa safiiiii kabisa kutoka UDSm,Mwalimu ni Kabudi na Mukandara(Watarudi kushika chaki). Yote imeonekana uchawa unalipa sana kwa nyakati hizi
 
Soon Machawa watapitisha azimio kuwe na Kitivo cha Uchawa Pale Chuokikuu,Yaani unaondoka na degree yako ya Uchawa safiiiii kabisa kutoka UDSm,Mwalimu ni Kabudi na Mukandara(Watarudi kushika chaki). Yote imeonekana uchawa unalipa sana kwa nyakati hizi
Ahhaaaaa kuna jamaa alipendekeza suala kama hilo eti secural education imeshindwa kuaccomodate need ya market.
 
Back
Top Bottom