Elections 2010 Nimepiga kura, wewe je?

Huyo Ami si alikuwa CUF amehamia lini CCM?????
 

Rais JK usinichekeshe mie na mzazi wangu (ambaye ni kada wa zamani wa CCM), mke wangu na wadogo zangu na watu wanne mtaani kwetu tushaajiri rais mpya wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Sie ndio waajiri wakuu bwana JK na wewe subirini matokeo naenda kulala narudi baadae kwenda kulinda kura yangu pale kituoni hakuna kulala hapa leo.
 
Paragrafu yangu ya mwanzo nilitaka nimwambie kikwete
ACHANA NA MAFISADI
Ndugu raisi mafisadi nusura wakukoseshe kura katika kampeni za uraisi.Kwa hivyo............
 
Huyo Ami si alikuwa CUF amehamia lini CCM?????

Mimi ndugu yangu wala sijawahi kuwa na chama.Nimepiga kura kwa kufuata ushauri wa askofu Kakobe,Gamanywa na Sheikh Mkuu.Sikuchagua chama bali nimechagua wagombea kulingana na sera na kampeni zao.Ndio maana vyama vyote vitatu vimepata kura yangu.
 
Mama yangu Mzazi amekwenda kumpa kura yake Rais wetu mtarajiwa Dr. W Slaa. Kwa miaka yote amekuwa anaipigia CCM ila mwaka huu anasema mtazamo wake kwa kiti cha Uraisi umebadirika. Lakini anampigia CCM-kiti cha ubunge kwani bado anaimani na muwakirishi mpya katika nafasi hiyo hali kadhalika katika kiti cha udiwani. Namuunga mkono kwa uchambuzi wake na uhamuzi wake wa busara. Sisi tulio nje ya nchi tunafurahia kuona progress na muamko wa namna hii. N.B familia ya watu kumi wote wanampigia Dr. Slaa..MUNGU IBARIKI TANZANIA!!
 


Na mimi nimepiga kura na tayari nimesha mfukuzisha kazi jamaa wa MIPASHO na mama wa PATACHIMBIKA hapa Gonja SAME MASHARIKI. Inatia raha sana kwani vijana wamejitokeza kwa wingi ile mbaya kuanzia maeneo ya Ndungu, Gonja Mpirani, Gonja Maore. Vijana wameamua kumkoma nyani. Mipasho, patachimbika wote chaliiiiii, Napata msosi kidogo halafu twaoenda zetu kulinda kura zetu. Usiku wa leo, lazima mama apelekwe Mirembe. PEOPLEEEEE'S POWERRRRRRRRRRRRRRRRRRRR............!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…