Nimepima UKIMWI naambiwa majibu yana utata nirudi baada ya mwezi vipi kuna usalama kweli?

Mhh! Sasa hiyo 'saikolojiko tocha' mtu unakua nayo mwezi mzima wanaifikiria? Mi naona heri upime na kwengine upate uhakika maana huo mwezi wa kusubiria utakua mgumu kwako sababu kucha utakuwa unawaza

Mambo grece mzima ww
 
hivyo vipimo umepima hospitali au,..
 
Huwa inatokea. Majibu yanakuwa yamecheza. Ilishamtokea rafiki yangu wa karibu alipoenda kupima muhimbili.
Ila aliporudia kipimo alikuwa negative.
 
Kajaribu kupima sehemu nyingine. BTW ukimwi sio kifo ikitokea umeukwaa tafuta washauri na wataalamu wakushauri utatumia dozi utaishi kama kawa. Kifo anapanga mungu unaweza kuwa na ngoma ukaishi na asiyenangoma akafa kwa ajali.
 
Mkuu utata huo unatokana na kimoja kuonesha unao na kingine kuonesha hauna!

Sasa kimoja kikionyesha unao tafsiri yake ni nn? Au wewe ni nan mpaka kimoja kionyeshe hauna?

Joking realax!
:closed_2:
 
pole mwakwetu mbona siku hizi huwaga wanawaambiaga ukweli hapohapo
sasa wewe wanakuambia urudi tena baadaye kulikoni?
ndugu yangu nenda hospt ingine kapime ukiona mambo yamevurugika anza dozi
Nifahamishen huo utata unakuwaje?
 
maelezo yako yamekaa poa sana(joti syle)
 
Kuna sera inayowaongoza wapimaji (watoa huduma) nchi nzima, kwamba wanaanza na aina fulani ya kipimo na majibu yake yataamua kama waendelee na aina ya pili au la; maana yangu ni kwamba ukienda kupima mahali pengine provided protocol ya upimaji inafanana, utapata majibu hayohayo. Ushauri wangu vuta subira hadi huo muda ulioambiwa kurudia kupima tena.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
By nestor83 :
Kupima VVU tunatumia vipimo vya aina mbili.
Ya kwanza ni Determine na ya pili ni Unigold.
Determine tunatumia kudetect uwepo wa vvu
na ili kujihakikishia tunatumia na unigold as
a confirmatory test. Ili kuonesha kwamba
umeathirika vipimo vyote viwili lazima vitoe
mistari miwili. Inapotokea kipimo kimoja yaani
Determine ikatoa mistari miwili na unigold
ikatoa mstari mmoja hayo ndio tunayosema
majibu tata. Na kwa kawaida inatakiwa urudie
kupima baada ya siku kumi na nne na sio
mwezi.

MAELEZOZO YA NESTOR NI SAHIHI KABISA INAWEZEKANA KABISA UTAKAPOENDA UKAAMBIWA UMEATHIRIKA AU LA. LAKINI KAMA UPO DAR UNAWEZA KWENDA AGHA KHAN HOSPITAL WANA KIPIMO KINGINE KINACHOITWA ELISA TEST HISHO KINA DETECT NGOMA HATA YA SIKU MOJA KAMA UPO MBALI NENDA BAADA YA SIKU KUMI NA NNE UNIGOLD NA DETERMINE YATAAONYESHO POA. LABDA NIELEZE NI NN KINAFANYA MAJIBU YAWE TATA INAWEZEKA KAMA SIO HIV BAS UTAKUA UNAUMWA UGONJWA MWINGINE AMBAO UNAPUNGUZA KINGA ZA MWILI HIVO UMEAMSHA ANT GEN ZAKO MWILINI NA HIVO KIPIMO HIKI KUDETECT MAANA VIPIMO HIVI HUPIMA ANTIGEN ZINAZOPAMBANA NA HIV. NAZAN TUMEELEWANA NAKARIBISHA MASWALI PALE AMBAPO HAPAJAELEWEKA.
 
Majibu yenye utata ndio majibu gani hayo?

Tafuta kituo chochote cha ANGAZA kapime huko, utapokea majibu yako muda mfupi tu na ya uhakika.

Inaonekana wengi hamjawahi kupima ukimwi,
wacha nitoe somo,
Ukienda kupimwa wakati wa ushahuri nasaa unaambiwa kawaida kuna majibu matatu, Postive, Postive/negative na negative.

Hili Postive/negative naamini ndili lilo mkuta ndugu yetu hapo na kawaida ili kuconfirm inabidi aje baada ya miezi mitatu maana kama ana virus basi atakuwa tayari kashakuwa Postive.
 

Hicho unachokieleza inawezekana kikawa na ukweli isipokuwa kisayansi huwa hakuna JIBU LENYE UTATA...

Unaweza ukawa na jibu la mwanzo lenye kuhitaji CONFIRMATION baadaye lakini si JIBU LENYE UTATA...

Kutokuona vizuri HIV huo sio UTATA
 
Ndugu watu8. Majibu yenye utata ni majibu yasiyotoa picha halisi ya kile unachokipima na yapo kwa sababu ifuatayo. Katika kipimo cha HIV kilichopo kinapima antigen-antibody reaction na sio HIV pekee inayostimulate hii reaction na ndio maana kama mtu alikuwa ana ugonjwa mwingine uliosababisha reaction hii basi tutapata majibu yenye utata nikimaanisha kipimo kimoja kikaonesha positive na kingine kikaonesha negative kwasababu kitadetect uwepo wa antibodies za aina tofauti. Na ndio maana tunawapa siku 14 ili infection nyingine iwe imekwisha ndipo tunarudia kupima tena.
 

Samahani naomba niendeleze swali.
1.Nifahamishe ni upi muda sahihi wa window period? Ni miezi 3 au 6 maelezo tafadhal
 
Kuna watu wanapenda kuwakatisha wenzao tamaa, mtu majibu yake tatabado unampa maneno kama RIP, unao na mengine ya ovyo. Kama hujui unasoma halafu unapita vile
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…