Nimepoteza imani katika dini ingawa bado ninahofu kuwa napotea

Nimepoteza imani katika dini ingawa bado ninahofu kuwa napotea

Maleven

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2019
Posts
689
Reaction score
3,373
Yani kwa sasa mtu akisema anaenda kwenye nyumba ya ibada namuona kama “old school” mtu anaeishi maisha ya kusadikika,

Bado naamini kuna Mungu ila Mungu huyo hahitaji ibada wala hana habari na sisi, hakuna moto wala pepo.

Dini zote naona ni kama vikundi vinavyojinasibisha tu lakini hakuna ukweli na ni habari za kutunga.

Naamini katika kutenda mema na kushi na watu vizuri lakini siamini kama kuna adhabu au zawadi huko mbinguni,

Naona kua sisi ni kama wanyama na viumbe wengine, ukifa lako limeisha na hakuna habari inayoendelea.

Kwa upande fulan bado ninahofu na natamani imani yangu irudi, nimekua nikijikaza kushirikiana na wanajamii mambo ya dini ila ukweli nafsi haitaki.

Niko njia panda katika hili.
 
Kuwa na amani ndugu.
Dini zilindwa na binadamu, wakaunda character asiyeonekana wakamuita mungu.

Wakaandika vitisho kutisha watu na ahadi kemkem za Kupatikana baada ya kufa..

Hata Mungu akiwepo, binadamu hana lolote ajualo kuhusu mungu.

So ishi kwa upendo na amani itakutawala tu.
 
"Nimepoteza imani katika dini ingawa bado ninahofu kua napotea"

Ni sawa na demu unayemtongoza akuambie anakupenda ila kama kaka yake
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Huko nilitoka zamani sana nimezaliwa katika uislamu na nimesoma dini vizuri.
Sikuishia hapo nikaanza kuisoma vizuri sana imani ya upande wapili
Wakristo.
Aisee ukristo ni mama mkuu wa
UONGO NA UTAPELI.
UISLAMU,BUDHA NA HINDU HAO NIWATOTO3 MAPACHA.
WAZAZI WAO WAPO JUU👆👆
HAPO.
FANYA MEDITATION SANA HAPO NDIO KUNAUKWELI THABITI KUHUSU DINI HIZI.
ILA SIO KAWAIDA KUNIELEWA NINGUMU SAAAAAAANAAA...
ILA WANAO NIELEWA WAMEELEWA.
 
Kwa upande fulan bado ninahofu na natamani imani yangu irudi, nimekua nikijikaza kushirikiana na wanajamii mambo ya dini ila ukweli nafsi haitaki.

Niko njia panda katika hili.
Hii ndo nature ya subconscious mind, kushikilia kwa nguvu zote kile ilichoaminishwa.
 
hii hali naipitia iv sasa ukizingatia mazingira niliyopo nimezungukwa na walokole aisee najiona nikiwa atheists mdogo mdogo
 
Ni kweli unapotea!. Nafikiri changamoto kubwa uliyonayo ni kuhusiana kwako na Mungu ki jamii au kifamilia zaidi na sio kibinafsi, kwahiyo hauna ushuhuda wowote wa roho ama mwilini mwako kukuonesha kwamba Mungu yupo, ila ukweli Yupo, na anakupenda sana, ingawa zipo roho za kukudanga zinakuambia tofauti,Kama neno linavyosema:
'1 Timothy 4:1
Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani'
Imani chanzo chake ni kusikia, jitahidi kutamani kusikiliza maneno ya Mungu ili imani yako ijengeke
 
Back
Top Bottom