Nimeshaanza kukata tamaa na Tanzania tunayofikirishwa. Je, wewe?

Nimeshaanza kukata tamaa na Tanzania tunayofikirishwa. Je, wewe?

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
1,958
Reaction score
3,890
Kwa kweli hali tunavyofikirishwa na majilabu ya Chama tawala kuwa wataiboresha Tanzania kuwa ya aina yake! Nashangaa sana tunaaminishwa tupo kimaendelea tupo uchumi wa kati na jana juzi tunaanza kuaminishwa kuendea uchumi nambari moja, nikazidi kushangaa na kuwachwa kwenye mataa.

Nina wasi na uchumi huu unaotajwatajwa na tunaoaminishwa kama unatuhusu sisi wanyonge, nimeona ile kauli ya Mnyonge myongeni lakini mpeni haki yake umegeuka na kuwa mnyonge msimnyonge lakini musimpe haki yake.

Rais Suluhu kuingia tu ameingia na gear ya kupandia mlima na ya kushukia mlima baada ya mkaguzi kuweza kupumua na Rais nae kupata pa kuchungulia au pa kuanzia kwa kusema anahitaji ukaguzi wa mahesabu kuanzia January na pia kuwasimamisha kazi wakuu wa bandari, Tunaweza sema yajayo yanafurahisha?

Mashaka ni kuwa sasa Rais ametafuta Mpango, kwa kuwa ni mapema huwezi juwa ni mpango gani? Ni wa yuleyule aliyeondoka na sasa mpango umepandishwa grade na ahadi ni za kufuata nyayo. Mitandaoni kwa wananchi wenye uchumi unaowaruhusu kuingia huko malalamiko yameanza kuwa raisi ameokota bokorewa au lulu?
 
Mashaka mengi husababisha msononeko wa moyo.

Na msononeko huko husababisha hata uchawi wa kimaendeleo.
 
Kwa mpango pale mimi sioni nuru yoyote ni kama kuzima afadhali iliyoanza kuonekana kupitia Mama, hata ukisikiliza speech yake aliyoitoa unaona ni kurudi kulekule tulipotoka.
 
Umakamu wa urais ni cheo ambacho hakikupi wigo wa kufanya maamuzi.

Kazi yako itakua kutabasamu, kuhudhuria warsha za chama kujaribu kumshauri rais na kutumaini mtamaliza ngwe yenu salama.

Kama unahisi uwepo wa makamu wa rais fulani utaleta impact ya kiutendaji kwa zaidi ya asilimia 2 nahisi haupo sahihi.

Uwaziri Mkuu huu sasa ndiyo bakora katika maamuzi.
 
Ukipata sehemu ya kupiga, piga (kweri kweri ) nchi ina resources za kumtosheleza kila mwenye akili kidogo tu,sasa kama wewe hata hizo kidogo huna basi tena pengine umeubwa ili uwe mtumwa tu.
 
Back
Top Bottom