Nimeshangaa kuona mtoto wa miaka 2.5 anaumwa kisukari.

Nimeshangaa kuona mtoto wa miaka 2.5 anaumwa kisukari.

Slave

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2010
Posts
5,313
Reaction score
2,646
Hellow jf dr's mtoto wa dada yangu kapatwa na huu ugonjwa wa kisukari ki-ukweli kabisa sikuwa kusikia kuhusu huu ugonjwa kuwapata watoto wadogo.hapa napata hofu kwa kuwa niliwahi kusikia huo ugonjwa hauna tiba.(sina uhakika) wana jf ninachoomba ni uelewa wenu 1. nini chanzo cha kisukari 2.ipi tiba yake
 
poleni sana. hiyo inajulikana kama juvenile diabetes type 1. inaweza kusababishwa na vitu viwili:
1.Autoimmune- ndio sababu kuu, virusi vinastua mwili kutengeneza sumu ya kinga, ambayo mwisho zinaharibu betta cells ambazo ziko kwenye pancreas na kusababisha insulin isitengenezwe kwa usahihi. inashukiwa kuwa ni Coxsackie B4 virus ama Cytomegalovirus
2.mara chache inatokea shambulizi makali kwenye pancrease (sijui ndo yaitwa kongosho?),ama kwa sababu zozote za kiugonjwa pancrease kuondolewa kwa operesheni

kuna uwezekano wa kuipata kwa 6/100 endapo ndugu yako wa tumbo moja anayo( so ni muhimu kuwaangalia kwa ukaribu hao nduguze manake type 1 diabetes ina-attack ghafla sana hivyo ni hatari). Akizingatia ushauri wa wataalamu haina madhara makubwa sana na atakua salama,inshaallah.
 
Hii ya mtoto wa miaka 2.5 ndiyo kali zaidi, bali kupata kufahamu zaidi kuhusu kisukari fuatisha anuani hii(mi si mtaalamu sana katika ku-link):kisukari | maajabu ya maji good luck

mkuu hiyo ndiyo hali halisi.amini usiamini. Pia kuhusu ku link sidhani kama kuna utaalamu zaidi ya hivyo ulivyofanya. Pia nimeanza kufunguka na sasa naanza kutambua umhimu wa maji.
 
safi sana mkuu kama umeanza ku-shine kuhusu maji, nakusihi uingie mara kadhaa katika blog hiyo na utajifunza mengi yatakayokusitaajabisha, king'asti kafafanuwa vizuri zaidi ila kwa huyo wa miaka miwili msitumie tiba ya maji bila kupata mwongozo wa kutosha kwanza.
 
safi sana mkuu kama umeanza ku-shine kuhusu maji, nakusihi uingie mara kadhaa katika blog hiyo na utajifunza mengi yatakayokusitaajabisha, king'asti kafafanuwa vizuri zaidi ila kwa huyo wa miaka miwili msitumie tiba ya maji bila kupata mwongozo wa kutosha kwanza.

kwa ufupi mtoto huyu alipatwa na homa kali hali iliyo wapelekea wazazi wake kumpeleka hosptl,kutokana na umbali kati yao na hosptl,mtoto alifika akiwa hoi taabani,baada ya kufungia mashine ya kupumlia na drip alipimwa na kuonekana na maralia pamoja na hiyo kisukari.na baada ya matibabu ya kama wiki moja mtoto alipata nafuu kiasi cha kushindwa kumtofautisha na mzima.binafsi niliona mtoto kapona kabisa.ila jana nilipatwa na mshtuko baada ya doctor kumwandikia uhamisho kwenda katika hosptal ya rufaa bugando.hili ndilo lililopelekea mimi kupatwa na hofu.
 
Hellow jf dr's mtoto wa dada yangu kapatwa na huu ugonjwa wa kisukari ki-ukweli kabisa sikuwa kusikia kuhusu huu ugonjwa kuwapata watoto wadogo.hapa napata hofu kwa kuwa niliwahi kusikia huo ugonjwa hauna tiba.(sina uhakika) wana jf ninachoomba ni uelewa wenu 1. nini chanzo cha kisukari 2.ipi tiba yake
Pepo hilo sio sukari ya kweli
 
Pepo hilo sio sukari ya kweli

mh! Fafanua ili nijaribu kupima uwezekano wa kuwepo kwa pepo.huwa siamini sana kama hayo mapepo yapo.ila naamini msemo wa lisemwalo lipo nakama halipo linakuja.
 
poleni sana. hiyo inajulikana kama juvenile diabetes type 1. inaweza kusababishwa na vitu viwili:
1.Autoimmune- ndio sababu kuu, virusi vinastua mwili kutengeneza sumu ya kinga, ambayo mwisho zinaharibu betta cells ambazo ziko kwenye pancreas na kusababisha insulin isitengenezwe kwa usahihi. inashukiwa kuwa ni Coxsackie B4 virus ama Cytomegalovirus
2.mara chache inatokea shambulizi makali kwenye pancrease (sijui ndo yaitwa kongosho?),ama kwa sababu zozote za kiugonjwa pancrease kuondolewa kwa operesheni

kuna uwezekano wa kuipata kwa 6/100 endapo ndugu yako wa tumbo moja anayo( so ni muhimu kuwaangalia kwa ukaribu hao nduguze manake type 1 diabetes ina-attack ghafla sana hivyo ni hatari). Akizingatia ushauri wa wataalamu haina madhara makubwa sana na atakua salama,inshaallah.
kin`gast umetoa maelezo ambayo yapo ki-taaluma zaid nami pia sasa nimeweza kupata pa kuanzia.
 
mh! Fafanua ili nijaribu kupima uwezekano wa kuwepo kwa pepo.huwa siamini sana kama hayo mapepo yapo.ila naamini msemo wa lisemwalo lipo nakama halipo linakuja.

Sukari kwa mtoto/mtu wa chini ya miaka 30 siyo jambo la kawaida.
 
Sukari kwa mtoto/mtu wa chini ya miaka 30 siyo jambo la kawaida.

majimoto.unanitisha mkuu. Embu fafanua kidogo tu.najua wewe unayo elimu kubwa ya kuyaelewa haya mapepo na tabia zake. Nakumbuka mengi sana watu wengi walijifunza/wanajifunza kupitia ile post ya biashara ya uchawi tanzania.wengi wamechukua tahadhari nakumbuka vizuri kuna sehemu uliandika dalili za mtu mwenye majini/mapepo, ulifafanua vizuri sana. mchangiaji. Pia ktk hili mkuu,naomba ufafanue japo kwa ufupi.
 
Hatari sana, watoto wengine wanazaliwa na matazizo kibao mpaka unaogopa
We acha tu... Kuna wakati almost tunakufuru kwa kuona watoto wanavo teseka yani. But we know Mungu hakuumba ugonjwa so tunasali sana in faith and hope...
 
We acha tu... Kuna wakati almost tunakufuru kwa kuona watoto wanavo teseka yani. But we know Mungu hakuumba ugonjwa so tunasali sana in faith and hope...
unaweza kukufuru kweli hasa katika mambo yenye utata kama haya
 
Tatizo lolote kwenye pancrease linasababisha ugonjwa wa sukari, rudia tena maelekezo yangu. Ama google juvenile diabetes utaona.

Sukari kwa mtoto/mtu wa chini ya miaka 30 siyo jambo la kawaida.
 
Mbona ni jambo la kawaida.. Kisukari ni ugonjwa wa kurithi so probably amerithi kutoka kwa mmoja wazazi wake.
 
unaweza kukufuru kweli hasa katika mambo yenye utata kama haya
Kua na imani tu kaka yangu. Sali sana na fanya chochote kilicho katika uwezo wako kumsaidia huyo mtoto....
 
mh! Fafanua ili nijaribu kupima uwezekano wa kuwepo kwa pepo.huwa siamini sana kama hayo mapepo yapo.ila naamini msemo wa lisemwalo lipo nakama halipo linakuja.
hutakiwi kuamini mapepo ila kukubali kuwa yapo na kukubali sio kuyasapoti, vitabu vya mungu vinasema shetani yupo sasa kama wewe hutaki iko siku utasema huamini kama mungu yupo, shauri lako bana
 
hutakiwi kuamini mapepo ila kukubali kuwa yapo na kukubali sio kuyasapoti, vitabu vya mungu vinasema shetani yupo sasa kama wewe hutaki iko siku utasema huamini kama mungu yupo, shauri lako bana

unajua mshangao nilio nao una maana kubwa.?hawa wazazi wa huyo mtoto wote ni watumishi katika kanisa.pia hapo juu kuna mchangiaji kasema huo ugonjwa ni wakurithi. Nimejaribu kufanya utafiti wa haraka haraka nikaona kwa upande wa mume hawajawahi kupata huo ugonjwa.hata upande wa mwanamke ambao ndiyo upande wetu pia hatujawahi kuuguza/kuugua kisukari.
 
Mpaka sasa hari ya mtoto inaonekana nzuri kwa kumtazama,ila kwa taarifa za daktari inaonyesha sukari haitulii,inakuwa inapanda na kushuka.mpaka leo tunaelekea wiki ya pili tangu mtoto alazwe hosptl.
 
Back
Top Bottom