Nimeshangazwa na Ushuru wa serikali wa kulipia mabango ambayo yapo kwenye biashara yako, mfano juu ya paa la sehemu yako ya biashara!

Nimeshangazwa na Ushuru wa serikali wa kulipia mabango ambayo yapo kwenye biashara yako, mfano juu ya paa la sehemu yako ya biashara!

TensorFlow

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2020
Posts
993
Reaction score
1,286
Wakuu,

Watu kutoka manispaa za Kinondoni na Temeke wamekuwa na hekaheka za kwenda kwenye sehemu za wafanyabiashara, maarufu kama fremu na kupima mabango ambayo yapo kwenye sehemu za biashara, na kudai yalipiwe. Hizo ni sheria za manispaa.

Najiuliza sana, kuwa bango lengo lake ni kuelekeza wateja kuwa kuna huduma fulani sehemu, wakishapata huduma hiyo, mwenye biashara analipa kodi na maushuru kibao serikalini, chahce tu ni kodi ya TRA, service levy - halmashauri husika, leseni, withholding tax, kodi ya pango, tozo kibao, usafi, nk.!

Sasa hapa inategemea na aina ya biashara, zingine zina msururu wa kodi na ushuru na vibali mpaka unajuta!

Huu ubunifu ni wa serikali yetu, mtu binafsi au ni nini hiki?

Kama bango lipo eneo la serikali, mfano yale makubwa barabarani kulipia sikatai, lakini bango lipo exactly sehemu yako ya biashara na tayari unalipa kodi na maushuru ya kufa mtu!

Mbona tunaua biashara kwa makusudi?

Tujadili.

tf.
 
Serikali hii ni kizungumkuti tu.
Matumizi makubwa na ya anasa.
Mfanyabishara wa kipato cha kawaida anaumizwa na msururu wa Kodi,Ushuru,tozo na gharama zingine ambazo hazima maelezo.
Hapo hapo kila siku Raisi na Waziri wa fedha wanazunguka duniani kutrmbeza bakuli tu na cha kushangaza hizo pesa za misaada na mikopo hazieleweki zinafanya nini na hata kinachofanyika nacho hakieleweki yaani hakiendani na misaada na mikopo waliyoomba. Hapo hapo unakuta kuna Bajaji 18,000 zimeandikwa SSH 2025 na thamani ya zile Bajaji zaidi ya 54 Billion
Hiyo hela ya hizo bajaj ingetolewa kama mikopo kwa Vijana na Wakina Mama si ingeleta tabasamu na unafuu wa maisha kwenye familia za Masikini wengi?
Serikali ifikie hatua hili suala la Makodi, Maushuru na Matozo iliangalie kwa makini sana. Maana Watanzania tunaumia mnoo as if tunatawaliwa na Mkoloni na hata huyo Mkoloni alikuwa anazingatia mahitaji muhimu ua kibinadamu
 
Wakuu,

Watu kutoka manispaa za Kinondoni na Temeke wamekuwa na hekaheka za kwenda kwenye sehemu za wafanyabiashara, maarufu kama fremu na kupima mabango ambayo yapo kwenye sehemu za biashara, na kuadai yalipiwe. Hizo ni sheria za manispaa.

Najiuliza sana, kuwa bango lengo lake ni kuelekeza wateja kuwa kuna huduma fulani sehemu, wakishapata huduma hiyo, mwenye biashara analipa kodi na maushuru kibao serikalini, chahce tu ni kodi ya TRA, service levy - halmashauri husika, leseni, withholding tax, kodi ya pango, tozo kibao, usafi, nk.!

Sasa hapa inategemea na aina ya biashara, zingine zina msururu wa kodi na ushuru na vibali mpaka unajuta!

Huu ubunifu ni wa serikali yetu, mtu binafsi au ni nini hiki?

Kama bango lipo eneo la serikali, mfano yale makubwa barabarani kulipia sikatai, lakini bango lipo exactly sehemu yako ya biashara na tayari unalipa kodi na maushuru ya kufa mtu!

Mbona tunaua biashara kwa makusudi?

Tujadili.

tf.
Watakusikia saaaasa? Vichwani wameweka maji akili wameziweka tumboni
 
Tatizo ni kuwa na watu wasiokuwa wabunifu na wwshamba ambao badala hata ya kujisomea zaidi na kuangalia nchi zinazoendelea zinaingiza namna gani mapato yao miji?
Lazima kuangalia wapi pa kuzipata na zinasaidiaje
Hizo hela zinaishia kwa watu wachache na sio ubunifu kabisa
Kuna mabango barabarani ya Rais yapo kila sehemu hayo nani analipia kuwepo hapo na ni sh ngapi
Ubunifu ni akili ambayo wengi hawana
 
Ukweli mchungu ni kwamba. Kwa Tanzania yetu hii mfanyabiashara akiwa mwaminifu kwa kulipa kodi kama inavyotakiwa basi miezi 6 haitoisha atakuwa ashafunga biashara.


Namfahamu mfanyabiashara mmoja (aliyefilisika) ambaye niliwahi kufanya naye mahojiano. Alilalamikia mifumo kandamizi ya kikodi ambayo ipo ikiwemo hilo la kodi ya mabango na tena kuna kupigwa faini pia.


Tanzania ili uweze ku sustain kwenye biashara yako basi unalazimika kukwepa kodi kama ukoma.
Ikiwa mtu analipa kodi nyingi namna hiyo. Iweje hata bango lake pia nje tu ya biashara yake alilipie?
Tanzania ukiwa mfanyabiashara unanyonywa ili ufunge biashara hasa biashara ndogondogo na za kati.

NB:
Sijasema watu wasilipe kodi ila angalia wewe mwenyewe. Ukiweza kukwepa “BIG UP” ukiwalipa SHAURI YAKO.
 
Tatizo ni kuwa na watu wasiokuwa wabunifu na wwshamba ambao badala hata ya kujisomea zaidi na kuangalia nchi zinazoendelea zinaingiza namna gani mapato yao miji?
Lazima kuangalia wapi pa kuzipata na zinasaidiaje
Hizo hela zinaishia kwa watu wachache na sio ubunifu kabisa
Kuna mabango barabarani ya Rais yapo kila sehemu hayo nani analipia kuwepo hapo na ni sh ngapi
Ubunifu ni akili ambayo wengi hawana
Mkuu ungesema tu Hawana akili ukisema wamekosa ubunifu unakuwa unawapendelea kiana
 
Wakuu,

Watu kutoka manispaa za Kinondoni na Temeke wamekuwa na hekaheka za kwenda kwenye sehemu za wafanyabiashara, maarufu kama fremu na kupima mabango ambayo yapo kwenye sehemu za biashara, na kuadai yalipiwe. Hizo ni sheria za manispaa.

Najiuliza sana, kuwa bango lengo lake ni kuelekeza wateja kuwa kuna huduma fulani sehemu, wakishapata huduma hiyo, mwenye biashara analipa kodi na maushuru kibao serikalini, chahce tu ni kodi ya TRA, service levy - halmashauri husika, leseni, withholding tax, kodi ya pango, tozo kibao, usafi, nk.!

Sasa hapa inategemea na aina ya biashara, zingine zina msururu wa kodi na ushuru na vibali mpaka unajuta!

Huu ubunifu ni wa serikali yetu, mtu binafsi au ni nini hiki?

Kama bango lipo eneo la serikali, mfano yale makubwa barabarani kulipia sikatai, lakini bango lipo exactly sehemu yako ya biashara na tayari unalipa kodi na maushuru ya kufa mtu!

Mbona tunaua biashara kwa makusudi?

Tujadili.

tf.
Tanzania ukisema ulipe kila kitu yani uwe mwaminifu haki biashara utaifunga. Yani mazingira ya kufanya biashara tanzania si rafiki. hili la mabango likiwa ni mojawapo.
 
Back
Top Bottom