Nimeshikwa pabaya - wakuu naomba msaada tutani!


Kwa upande mwingine ukiamini kuwa ni kweli, ndiyo maana wengine tunaona kuwa huyu jamaa ni hovyo kabisa, limbukeni wa mapenzi...ni kiazi kweli kweli!
 
kama unataka ushauri wangu kisha uumbayuwayu ni hivi,
tafuta kamera swaaafi kisha fanya mpango wa kuwanasa ktk mikao mibovu ya hasara kisha tandika foto kadhaa kwa siku tofauti tofauti then mtumie mbwiga mwenye mke ili afure zaidi. wewe usiongee neno just tuma picha maana huwa zinaongea kuliko maneno.
 
Huyo jamaa yako kama hataki kuelewa, na wewe mchimbe mkwara aache kukutishia maisha

...No no, no!
Hiyo itamaanisha kuna kaukweli amemind 'kupigwa kibuti!.'
Asubirie tu 'siku ya kilio,' kumkumbushia rafiki yake; "nilikwambia hukuniamini!"
 

...ebana wee,..yanini unamshawishi huyu jamaa 'hobby' ya ukozimeni bana?

Yaliyompata yeshamtosha. Keshasema yupo ughaibuni, na winter ndio ishaanza sasa,
Unataka apate pneumonia bure kwa kunyatia na kuchungulia vidirishani mwa watu?

Atakuja sutwa bure mwenzenu. Jamaa mshamsikia, anaweza pata picha na still akasema
ni photoshop sijui nini!...
 
Thanks for the knowledge!:smow:
 
Na hili ndilo mshikaji (rafiki yangu) analong'ang'ania kuwa kama nilijua kwanini sikutangulia kumwambia. Ukweli ni kwamba sikutaka kukurupuka katika kumtaarifu jamaa hasa ukizingatia najua kuwa anamppenda sana mkewe.
Ulikuwa sawa pia kwani wakati mwingine si vizuri kukurupuka,never regret
 

Duuh, samahani sana kaka kama hukunipata vizuri pengine sikuwa clear. Lakini kilichopo ni kwamba huyu shemeji yangu ametumia "defensive mechanism", yaani kutangulia kuripoti kuwa nimemtongoza ili in case mimi nikimripoti yeye kuwa ana-cheat, nionekane muongo, na kwa hilo amefanikiwa. Nashukuru wachangiaji wengi walinielewa hivyo. Hata hivyo nashukuru kwa mchango wako.

Halafu siyo kwamba niligharamia safari yake yote ya kuja hapa isipokuwa katika pilikapilika za kumsaidia niliingia gharama fulani, naona mkuu hiyo umeikolezea sana.
 
hapo kazi ipo, kama jamaa anaweza pata vekeshen ya kuja huko, japo ya muda mfupi tu! aje na afikie kwako na bila kumtaarifu mkewe angalau ajionee mwenyewe kinachoendelea, indekusaidia zaidi, pole sana mkuu.
 
Bora uyo mama ana megwa a uyo jamaa ,kuliko angekaa Bongo angemegwa na mapredejee na kukamata ngoma ingawa ngoma iko kote.
Hivi kwa nini unapoteza muda na kujistress na huyo mlupo? kama amemegwa huko ulaya inawezekana alisha kua ana megwa hata huko TZ nadhani ni vizuri wamesha tengana bila kujijua ,sababu wanaishi nchi tofauti ni vizuri utumie njia za busara kumfahamisha huyo rafiki yako ( haswa ukiwa na ushahidi wa uhakika ) kama mkewe amewekwa kinyumba na jamaa huko mamtoni. Hapo huyo rafiki yako ataamua kubeba mlupo au kuachana naye.
 
Pole sana mkuu kwa yaliyokukuta.
Nakushauri kama kama inawezekana jaribu kuongea na rafiki yako tena kwa upya kuhusu ishu hiyo.Usimchukie coz hata ungekuwa wewe lazima ungepata mshtuko fulani though sio lazima kwamba unge-react kama yeye,ila lazima hiyo kitu ingekustua!Jaribu kadri uwezavyo kumueleza kuwa kama anaweza aje huko ulipo pasipo mke wake kujua ili aje ajionee mwenyewe yanayoendelea na kwamba wife kashahama hostel kabisa.
Na alifanya hivyo kama njia ya kujilinda tu ili pindi ukimweleza asikuamini kwa lolote.Stick on that uone rafiki yako atachukua hatua gani.All in all just try to ease yourself ili hii ishu isije kukuletea BP bure ndugu yangu....asipokuelewa achana naye.
 
Dem kakuwahi huyo.inabidi upate hard evidence za kujikinga au vipi ukirudi bongo jamaa akupige kisu cha KANYUNGU !!!!
 
hapo kazi ipo, kama jamaa anaweza pata vekeshen ya kuja huko, japo ya muda mfupi tu! aje na afikie kwako na bila kumtaarifu mkewe angalau ajionee mwenyewe kinachoendelea, indekusaidia zaidi, pole sana mkuu.

...enyi watu hamkubali ukweli 'sikio la kufa halisikii dawa!' ???
keshasema hataki kuambiwa upuuzi huo kuhusu mkewe!
Mpaka amuue Deodat ndio mtaamini huyu bwana 'kazidiwa?'
 

Usirudi Bongo.

Kwanza huku njaa tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…