Nimeshindwa kuishi kwa makosa yangu mwenyewe

Nimeshindwa kuishi kwa makosa yangu mwenyewe

0713417189

Senior Member
Joined
May 12, 2021
Posts
115
Reaction score
201
NIMESHINDWA KUISHI KWA MAKOSA YANGU MWENYEWE.
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304 ( WHATSAAP )

SEHEMU YA KWANZA.
NYAKATO KWA SAA NANE SOKONI.
"Karibu dagaa safi kabisa. Nguo unapata kwa shilingi elfu moja tu, ni sawa na bure. Kula madagele ya leo leo ukichelewa hupati kitu"
Hizo zilikuwa ni sauti za wafanya biashara mbali mbali wakinadi bidhaa zao. Katika soko maarufu mjini Musoma. Naam, wanapaita Nyakato, mtaa huo ukiachilia mbali soko hilo. Ni maarufu sana kwa uuzaji wa pombe za kienyeji hasa gongo.

Wakazi wake ni wengi sana. Pamechangamka. Watu kutoka kijijiji jirani cha bisumwa wamekuwa wakinyonga baiskeli zao kufata mahitaji muhimu. Kwa yeyote aliyewahi kuishi manispaa ya Musoma mkoani Mara, anaujua vyema umaarufu wa mtaa huo. Hasa miaka ya nyuma kuna kundi la vijana waliokuwa wakipora mali za watu. Walitumia eneo hilo kama maficho yao.

Vumbi jekundu, tope wakati wa mvua havikuweza kukwepeka. Katika medani za siasa hawakuwa nyuma. Nyakati za uchaguzi chama tawala kilikuwa kikikutana na upinzani mkali. Kutoka katika chama cha CHADEMA. ofisi za Chadema zilikuwa huko nyakato.

. Chezea Nyakato wewe, ni uswahilini penye kila burudani uliyohitaji. Makazi mengi yalikuwa ni duni. Na kabila lililokuwa na watu wengi hapo ni wakwaya na hata wajita pia.

Kelele za watu kuibiwa nyakati za usiku. Hapo ndipo palikuwa nyumbani kwake. Nani atoke pindi asikiapo yowe. Waliogopa, waliishi hivyo mpaka pale serikali ya mtaa ilipoamua kulivalia njuga. Vikao vya kila mara vikatokomeza kwa kiasi fulani tabia hiyo. Lakini katika suala la vijana kubwia pombe za kienyeji asubuhi, lilishindikana. Walipokamata wauza gongo kwa wingi. Vijana hao wakaamia kwenye pombe kali za kupima. Mtanange ukazidi kupamba moto.

_____________________________________
PAULINA alikuwa ni binti wa mzee maarufu sana hapo nyakato. Katika maeneo ya magamaga. Ni binti wa mzee Makunja Maregesi. Ukiuliza hata mtoto wa miaka mitano akupeleke katika mji huo, basi ondoa shaka umefika bila ya kupotea. Ucheshi, hekima na hata busara zilichagiza kufahamika kwake.. Lakini pia alikuwa ni fundi baiskeli wa miaka mingi sana. Uaminifu wake ukamuongezea wateja wengi. Na kufanya familia yake iweze kupata mahitaji ya kila siku. Kwa kile kidogo kilichokuwa kikipatikana. Ule upara wake kichwani ukamuongeza jina la utani kwamba mzee kipara. Hakuwa na hiana akalipokea kwa mikono miwili.

Nyumbani kwake alifanikiwa kufuga mbuzi wawili, ambao waliongezeka mpaka kufika watano. Kadiri siku zilivyozidi kwenda uzee ulimtafuna. Na hapo ndipo akajilaumu kwa kuchelewa kuoa na kupata watoto. Nguvu za kugongelea vyuma vya baiskeli, hatimaye zilianza kupungua. Ugonjwa wa kibofu cha mkojo ukawa pigo kwake. Na kudhoofisha kabisa utafutaji wake. Maisha yakazidi kuwa magumu. Mkewe ambaye hakuwa na umri mkubwa. Akayavaa majukumu na kuanza kuuza dagaa wa bichi katika soko hilo la Nyakato.

Kupanda kwa bei ya nyama. Na samaki aina ya sato na sangara kuadimika. Ilikuwa ni furaha kwa wauza dagaa. Kwani familia nyingi za Musoma ziliweza kumudu kununua dagaa kuliko nyama. Mkewe Mzee Makunja, akamshukuru Mungu. Kwani pesa aliiona na kuanza kuweka akiba, ambayo ikawa inamsaidia mumewe katika matitabu. Lakini kauli ya madaktari kwamba Makunja anatakiwa apelekwe hospitali ya Bugando Jijini Mwanza. Kwaajili ya upasuaji mkubwa. Ilimuumiza sana Mama huyo. Pesa aliyokuwa nayo isingefua dafu.
______________________
PAULINA alikuwa ni mtoto wa pili na wa mwisho wa Mzee Makunja. Kakake hakuwa na muda mwingi Duniani. Alifariki akiwa na miaka ishirini tu. Aliitwa Machumu. Alibahatika kumaliza kidato cha nne katika shule ya sekondari Mshikamano. Iliyopo hapo hapo manispaa ya Musoma Mjini. Matokeo yalikuwa mabaya kwake. Alipata daraja sifuri kabisa. Hakujutia hata kidogo, kwani kwa mwezi alihudhuria shuleni mara tano au kumi. Wazazi waliongea na kumkanya lakini hakuskia. Majuto ni mjukuu, msemo huo kwake haukuwa na maana kabisa.

Machumu kabla ya umauti kumfika. Aliamua kuwa boda boda wa pikipiki. Alikuwa anapaki hapo kwa saa nane katika soko la Nyakato. Pesa ya kula na hata kuwapelekea wazazi wake Furu, madegere, na unga havikumpiga chenga. Akaanza kuwa anawapiga vijembe wale waliosoma mpaka vyuo vikuu na wapo tu mtaani. wakitegemea wazazi wao kwa kila kitu.

______________________
ITAENDELEA........
received_949343179602948.jpg
 
NIMESHINDWA KUISHI KWA MAKOSA YANGU MWENYEWE.
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304 ( WHATSAAP )

SEHEMU YA KWANZA.
NYAKATO KWA SAA NANE SOKONI.
"Karibu dagaa safi kabisa. Nguo unapata kwa shilingi elfu moja tu, ni sawa na bure. Kula madagele ya leo leo ukichelewa hupati kitu"
Hizo zilikuwa ni sauti za wafanya biashara mbali mbali wakinadi bidhaa zao. Katika soko maarufu mjini Musoma. Naam, wanapaita Nyakato, mtaa huo ukiachilia mbali soko hilo. Ni maarufu sana kwa uuzaji wa pombe za kienyeji hasa gongo.

Wakazi wake ni wengi sana. Pamechangamka. Watu kutoka kijijiji jirani cha bisumwa wamekuwa wakinyonga baiskeli zao kufata mahitaji muhimu. Kwa yeyote aliyewahi kuishi manispaa ya Musoma mkoani Mara, anaujua vyema umaarufu wa mtaa huo. Hasa miaka ya nyuma kuna kundi la vijana waliokuwa wakipora mali za watu. Walitumia eneo hilo kama maficho yao.

Vumbi jekundu, tope wakati wa mvua havikuweza kukwepeka. Katika medani za siasa hawakuwa nyuma. Nyakati za uchaguzi chama tawala kilikuwa kikikutana na upinzani mkali. Kutoka katika chama cha CHADEMA. ofisi za Chadema zilikuwa huko nyakato.

. Chezea Nyakato wewe, ni uswahilini penye kila burudani uliyohitaji. Makazi mengi yalikuwa ni duni. Na kabila lililokuwa na watu wengi hapo ni wakwaya na hata wajita pia.

Kelele za watu kuibiwa nyakati za usiku. Hapo ndipo palikuwa nyumbani kwake. Nani atoke pindi asikiapo yowe. Waliogopa, waliishi hivyo mpaka pale serikali ya mtaa ilipoamua kulivalia njuga. Vikao vya kila mara vikatokomeza kwa kiasi fulani tabia hiyo. Lakini katika suala la vijana kubwia pombe za kienyeji asubuhi, lilishindikana. Walipokamata wauza gongo kwa wingi. Vijana hao wakaamia kwenye pombe kali za kupima. Mtanange ukazidi kupamba moto.

_____________________________________
PAULINA alikuwa ni binti wa mzee maarufu sana hapo nyakato. Katika maeneo ya magamaga. Ni binti wa mzee Makunja Maregesi. Ukiuliza hata mtoto wa miaka mitano akupeleke katika mji huo, basi ondoa shaka umefika bila ya kupotea. Ucheshi, hekima na hata busara zilichagiza kufahamika kwake.. Lakini pia alikuwa ni fundi baiskeli wa miaka mingi sana. Uaminifu wake ukamuongezea wateja wengi. Na kufanya familia yake iweze kupata mahitaji ya kila siku. Kwa kile kidogo kilichokuwa kikipatikana. Ule upara wake kichwani ukamuongeza jina la utani kwamba mzee kipara. Hakuwa na hiana akalipokea kwa mikono miwili.

Nyumbani kwake alifanikiwa kufuga mbuzi wawili, ambao waliongezeka mpaka kufika watano. Kadiri siku zilivyozidi kwenda uzee ulimtafuna. Na hapo ndipo akajilaumu kwa kuchelewa kuoa na kupata watoto. Nguvu za kugongelea vyuma vya baiskeli, hatimaye zilianza kupungua. Ugonjwa wa kibofu cha mkojo ukawa pigo kwake. Na kudhoofisha kabisa utafutaji wake. Maisha yakazidi kuwa magumu. Mkewe ambaye hakuwa na umri mkubwa. Akayavaa majukumu na kuanza kuuza dagaa wa bichi katika soko hilo la Nyakato.

Kupanda kwa bei ya nyama. Na samaki aina ya sato na sangara kuadimika. Ilikuwa ni furaha kwa wauza dagaa. Kwani familia nyingi za Musoma ziliweza kumudu kununua dagaa kuliko nyama. Mkewe Mzee Makunja, akamshukuru Mungu. Kwani pesa aliiona na kuanza kuweka akiba, ambayo ikawa inamsaidia mumewe katika matitabu. Lakini kauli ya madaktari kwamba Makunja anatakiwa apelekwe hospitali ya Bugando Jijini Mwanza. Kwaajili ya upasuaji mkubwa. Ilimuumiza sana Mama huyo. Pesa aliyokuwa nayo isingefua dafu.
______________________
PAULINA alikuwa ni mtoto wa pili na wa mwisho wa Mzee Makunja. Kakake hakuwa na muda mwingi Duniani. Alifariki akiwa na miaka ishirini tu. Aliitwa Machumu. Alibahatika kumaliza kidato cha nne katika shule ya sekondari Mshikamano. Iliyopo hapo hapo manispaa ya Musoma Mjini. Matokeo yalikuwa mabaya kwake. Alipata daraja sifuri kabisa. Hakujutia hata kidogo, kwani kwa mwezi alihudhuria shuleni mara tano au kumi. Wazazi waliongea na kumkanya lakini hakuskia. Majuto ni mjukuu, msemo huo kwake haukuwa na maana kabisa.

Machumu kabla ya umauti kumfika. Aliamua kuwa boda boda wa pikipiki. Alikuwa anapaki hapo kwa saa nane katika soko la Nyakato. Pesa ya kula na hata kuwapelekea wazazi wake Furu, madegere, na unga havikumpiga chenga. Akaanza kuwa anawapiga vijembe wale waliosoma mpaka vyuo vikuu na wapo tu mtaani. wakitegemea wazazi wao kwa kila kitu.

______________________
ITAENDELEA........View attachment 3084551
Nimerejea....
 
NIMESHINDWA KUISHI KWA MAKOSA YANGU MWENYEWE.....02
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304 ( WHATSAAP )




SEHEMU YA PILI.....

Ilipoishia sehemu ya kwanza...

Machumu kabla ya umauti kumfika. Aliamua kuwa boda boda wa pikipiki. Alikuwa anapaki hapo kwa saa nane katika soko la Nyakato. Pesa ya kula na hata kuwapelekea wazazi wake Furu, madegere, na unga havikumpiga chenga. Akaanza kuwa anawapiga vijembe wale waliosoma mpaka vyuo vikuu na wapo tu mtaani. wakitegemea wazazi wao kwa kila kitu.


ENDELEA NAYO....

PAULINA rangi yake ilikuwa ni nyeusi, lakini weusi wa kung'aa. Wembamba na urefu wake, vikamfanya apachikwe jina la missi. Kichwa chake kipana na kirefu, kikapendezeshwa na macho makubwa mazuri. Ukiskia macho kumchuzi ndo hayo sasa. Chini yake ilikaa vyema ile pua ndefu mithili ya msomali au Mnyarwanda. Mdomo ulikuwa ni mdogo, wenye lipsi zilizolingana vyema kabisa. Juu ya huo mdomo alikuwa na kidoti cheusi. Kilichoongeza muonekano mzuri wa uso wake. Naam, waliomuita mrembo wa kabila la Wakwaya hawakukosea. Pamoja na udogo wake, lakini Kazi ya Mungu ilionekana kwa uzuri kabisa, kwamba aliumbwa akaumbika.

WINGU LA UMAUTI lilizidi kutanda katika anga ya maisha ya Mzee Makunja. Alilia na mola wake. Akatamka mipango ambayo bado hajaitimiza. Akiomba walau apate hata miaka mitatu mbele. Ni kama aliiona kesho yake iliyofika tamati. Unyonge, kilio havikuacha kumsakama ni kama vilikuwa vikimuwinda. Mkewe na mwanaye jukumu la kumtia moyo mzee huyo, walilivaa kikamilifu.

FURAHA ikitoweka katika familia ni kama mkuki uliokitwa kidondani. Maumivu yake hayavumiliki. PAULINA kuna nyakati macho yake yalijawa na machozi. Alikumbuka mengi ambayo Babaye alimsihi hayafanyie kazi. Akajiona anadeni kubwa yapaswa kulilipa angali mzee akiwa hai.
___________________

"Hey..! we mwanafunzi mambo?"
Ilikuwa ni sauti kutoka kwa boda boda mmoja. Akiwa ameegesha pikipiki yake, kando ya shule ya sekondari Bweri Makatani.

Kimyaaaaaaa....

"Kwahiyo hauniskii, waleta dharau?"

Dereva boda huyo alizidi kufoka. Akawa anaiwasha pikipiki yake, kumfata mwanafunzi huyo kwa nyuma.

"Kaka niache, mbona wanisumbua!"

Alilalamika PAULINA, akavuka barabara na kuelekea upande wa pili. Lakini boda huyo alimfata pia.

"Kaka niache nisome!"

"Kuna msomi hapo! au mwakalia uma... ya ...tu "

"Unajifanya msoooomi, mse***** wewe!"

Kijana huyo alitukana. Kitendo hicho kilimuumiza sana PAULINA. Alivyofika nyumbani alimueleza Mamaye kila kitu.

"Pole sana mwanangu. Simama imara, tambua nini unachokifanya shuleni. Soma kwa bidii uje uwe daktari. Uweze kumtibu babako, kama atakuwa bado u hai. Elimu ni mkombozi mpya anayepatikana kwa kuvuja jasho jingi, hasa kwa ninyi watoto wa kike. Maisha tunayoishi ni kama kuzimu hatuna nuru wala tabasamu. Shida ndizo zimepamba sura ya kitabu cha tamthiliya ya maisha yetu"

Maneno hayo yalitoka kinywani mwa Mamaye PAULINA.

"Sawa Mama, nimekuelewa!"

Lilikuwa ni jibu la unyenyekevu kutoka kwa Paulina. Baada ya hapo alienda kuoga, kisha akarejea na kuchukua chakula alichokuwa amehifadhiwa.

"Mwanangu PAULINA, nimesikia karibia mnafanya mtihani wa kidato cha nne?"

Alizungumza kwa sauti kavu babake.

"Ni kweli baba, jumatatu tunaanza mtihani, niombee sana." alijibu PAULINA.

"Nakuombea saana mwanangu, huenda wewe ndo ukaja niamsha hapa kitandani. Ikiwa ni kwa kupata pesa za upasuaji mkubwa. Au hata kupata kazi nzuri. Itakayokuwa msaada kwa familia"

Ni kama mzee alipaliwa akaanza kukohoa mfululizo. Paulina akakimbia ulipo mtungi wa maji, akachota maji na kumpelekea.

"Kunywa maji baba" alisema Paulina, sura yake ikiwa imepoa, na kupoteza tabasamu.

"Uzee na haya maradhi vinaniumiza sana mwanangu!"

Alilalamika Mzee Makunja, baada ya kumaliza kunywa yale maji aliyoletewa na bintiye.

"Sasa haya maisha ntayaishi mpaka lini? Kila kukicha nuru ya mafanikio inazido kufifia."

Alizungumza pekee mkewe Mzee Makunja. Ni kama hali ya maisha ilimnyima usingizi. Usowe ukalipoteza tabasamu. Nguvu ya kuiacha familia na kwenda mbali kutafuta maisha, ikachukua nafasi kubwa moyoni mwake. Lakini kila akimtazama PAULINA, nguvu za kuondoka zinayeyuka.

"Familia yangu, niombeeni maisha mema, uko nendako. Maumivu yapitayo katika mwili wangu hayavumiliki tena!"

Sauti ya uchungu na simanzi, kutoka kinywani mwa Mzee Makunja akimwambia mkewe na mwanaye pia. Hawakua na la kujibu zaidi ya kuyaachia machozi yawabubujike, mpaka yatakapokoma.
_________________ ITAENDELEA _________________
JamiiForums1700149874.jpg
 
NIMESHINDWA KUISHI KWA MAKOSA YANGU MWENYEWE.....03
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304 ( WHATSAAP )



SEHEMU YA TATU.....

Ilipoishia sehemu ya pili...

Alizungumza pekee mkewe Mzee Makunja. Ni kama hali ya maisha ilimnyima usingizi. Usowe ukalipoteza tabasamu. Nguvu ya kuiacha familia na kwenda mbali kutafuta maisha, ikachukua nafasi kubwa moyoni mwake. Lakini kila akimtazama PAULINA, nguvu za kuondoka zinayeyuka.

"Familia yangu, niombeeni maisha mema, uko nendako. Maumivu yapitayo katika mwili wangu hayavumiliki tena!"

Sauti ya uchungu na simanzi, kutoka kinywani mwa Mzee Makunja akimwambia mkewe na mwanaye pia. Hawakua na la kujibu zaidi ya kuyaachia machozi yawabubujike, mpaka yatakapokoma.

ENDELEA NAYO.............


MATOKEO YA KIDATO CHA NNE, yalitangazwa rasmi. Purukushani za wazazi wenye simu janja, walipambana kutafuta matokeo ya watoto wao. Lakini wale kapuku, walisogea kwenye vibanda vya huduma za intaneti. Na kuomba wasaidiwe, tena kwa kulipia kiasi fulani cha pesa.

"Taja namba yako!"

"Naongea na wewe binti, unaweza nini? ninawatu wengi wa kuwahudumia!"

Aliyekuwa akikurupushwa ni Paulina. Akataja namba yake kwa upesi kabisa. Akaambiwa asogee karibu atazame matokeo yake. Akapewa na kipande cha karatasi kama atapenda kuyanakiri.

"Wuiiiiiiiiiiiiiiiiiii..."

Alipiga yowe, kana kwamba kang'atwa na mdudu. Au kapokea taarifa mbaya za msiba. Lakini haikuwa hivyo, hakuamini kile alichokiona. Alikuwa amepata daraja la mwisho kabisa, yaani sifuri. Alijikaza taratibu akazipiga hatua kuelekea nje. Ghafla akaitwa kwamba hajalipa pesa. Akatoa shilingi elfu moja akalipa. Uso wake ulifunikwa na machozi. Alilia pasi ya kutoa sauti kwa kuogopa umati wa watu. Uchungu ulimzidia akaamua kukaa pembezoni mwa duka moja, na kuanza kulia kwa sauti. Awamu hii hakuhofia tena macho ya watu wanaomtazama.

"Baba u mgonjwa kitandani, akipokea matokea haya si kama nimempa kibali cha kuiaga dunia." Alilalamika Paulina binti wa watu.

"Pole binti simama uende nyumbani!"

Kimyaaaaaa..

"Kwani nyumbani wapi?"

"Nyakato karibia na soko la kwa saa nane"

Alijibu Paulina, baada dada huyo mwenye duka, kujaribu kumtuliza..

Kinyonge, alisimama kichwa chini mikono nyuma, Alisimama. Na kuelekea barabara ya Mkendo, akakatisha Uhuru na kuibukia mtaa wa karume, karibia na hotel ya AFRILUX. Akasimama kidogo na kushangaa vijana waliokuwa wamekusanyika hapo wakibishana, kuhusu wanawake warembo Tanzania.

Alitikisa kichwa, akaendelea na safari yake mpaka akafika Mwigobero, lengo alitaka akaione feri maana tangu imeanza kuvusha watu kuwapeleka mpaka kinesi hakuwahi kuiona. Alikuta mazingira ya kivukoni yamebadilika sana.

Aliamua kufanya hivyo, walau mawazo ya kufeli mtihani yapungue. Haikuwa kweli. Ni kama alifufua upya ahadi za wazazi wake ambazo msingi mkubwa wa kuzitimiza ilikuwa ni yeye kufaulu kidato cha nne, na kusonga mbele.

SAA KUMI NA MOJA NA NUSU ZA JIONI,
Paulina aliona ni muda sahihi wa kuanza kurejea nyumbani. Akiwa njiani alijaribu kuumba maneno, ni kwa jinsi gani atamfikishia matokeo haya mamake. Kila neno alilotaka kulitumia mwisho wa siku anaona halifai. Kiukweli alikuwa na kibarua kizito sana.

Alipita katika vichochoro mbalimbali. Akaibukia barabara ya mtaa wa Shabani, akachepuka tena mkono wa kushoto akaingia makongoro akaanyosha. Kabla hajaingia Nyerere road, alistukia akimiminiwa mvua ya matusi.

"We mwanaharumu nini, hauoni gari? unavuka tu kama barabara ya mjomba ako hii!"

Alifoka kijana aliyekuwa ameketi nyuma, kwenye lori lililokuwa limebeba mawe. Hakuna kati yao aliyebahatika kujua ni kipi kinachomuumiza binti huyo.

Alitembea barabara nzima akiwa amejiinamia. Kitendo hicho kilipoteza ule umakini wake wa siku zote, pindi awapo barabarani..
Hatimaye PAULINA, alifika nyumbani. Aliingia kwa kunyata kama mgeni. Aligundua mamake bado hajafika. Alishukuru Mungu. Akazivuta pumzi zake kwa fujo na kuzitoa taratibu. Aliingia ndani akamsalimu babake, alivyoitikia tu salamu, alirudi haraka nje. Hakutaka maongezi marefu akihisi ataulizwa habari za matokeo.

Alielekea jikoni akachukua dagaa, na kuanza kutengeneza. Mapigo ya moyo pia yalimuenda kasi, na tumbo la hofu lilimuunguruma.

"Afadhali umejiongeza, leo nimechelewa kumaliza biashara"

"Nilijua tu, ikanibidi nianze kuandaa mboga" alijibu Paulina.

"Sasa naona umekua binti yangu, ngoja nimuone mzee kisha nikajimwagie maji" alitamatisha Mama Paulina.

Ilikuwa ni saa mbili na nusu za usiku. Walimaliza kula chakula. Juma hili walau Mzee Makunja afya iliimarika, aliweza kuzungumza na kusimama pia. Lilikuwa ni jambo la kupendeza kwa familia yake.

"Mwanangu vipi matokeo, nilisubiri tumalize kula kwanza!"
_______________ ITAENDELEA ___________________

KAMA UNA CHANNEL YAKO YOU TUBE, UNAHITAJI SIMULIZI KWAAJILI YA KUSIMULIA .

BASI NIONE, BEI NI POA SAAAANA.

MAWASILIANO

0757 238 304 ( WhasAPP )

0713 417 189 ( piga simu au tuma sms )
 
NIMESHINDWA KUISHI KWA MAKOSA YANGU MWENYEWE.....04
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304 ( WHATSAAP )

SEHEMU YA NNE.....

Ilipoishia sehemu ya tatu...

Ilikuwa ni saa mbili na nusu za usiku. Walimaliza kula chakula. Juma hili walau Mzee Makunja afya iliimarika, aliweza kuzungumza na kusimama pia. Lilikuwa ni jambo la kupendeza kwa familia yake.
"Mwanangu vipi matokeo, nilisubiri tumalize kula kwanza!"


ENDELEA NAYO.....

"Mwanangu vipi matokeo, nilisubiri tumalize kula kwanza!"

Paulina hakujibu kitu...

"Nazungumza na wewe, kwani unawaza nini?"

Paulina hakutia neno lolote lile. Akatoa kipande cha karatasi na kumkabidhi.

"Doh! mwanangu umefanya nini hiki?"

"Nisamehe Mama, nisamehee!"

Alijibu huku machozi yakianza kumchuruzika.

"Mwanangu hatukukubaliana hivi, umeamua kuniumiza. Utakuwa vipi dakatari, umuuguze babayo kwa matokeo haya?"

Si Mama wala mtoto waliangusha kilio kizito. Huku kila mtu akizungumza maneno ambayo mwenziye hakuweza kuyasikia sababu ya sauti za vilio kutawala.

"Mwanangu nitamwambia nini babako! alikutegemea sana!"

Alilalamika Mama mtu.

Mama ni Mama, hakuna kama yeye. Pamoja na maumivu ya mwanaye kufeli, bado aliamua amtulize na kumpa moyo. Aliona ni jinsi gani binti yake ameumizwa. Alimkumbatia na kumbusu katika paji la uso kama ishara ya upendo.

"Nenda kalale mwanangu, babako nitamueleza, nikielekea chumbani kupumzika!"

"Nitashukuru sana Mama"

Paulina alielekea chumbani kwake kwaajili ya kupumzika. Hakika siku hii ilikuwa ngumu sana katika maisha yake. Machozi aliyomwaga katu hatokuja kuyasahau. Mama Paulina akiwa chumbani na mzee alimueleza taratibu na kwa utulivu matokeo ya binti yake. Mzee hakuwa na neno na hakutaka kuzungumza kitu. Machungu na maumivu yalifichika ndani ya moyo wake.

BAADA YA MWAKA MMOJA KUPITA
PAULINA alizidi kukua na kuzoea mazingira ya nyumbani. Alikuwa akienda sokoni na kumsaidia Mamake. Umaarufu wa jina lake uliongezeka hapo Nyakato kwenye soko la saa nane. Vijana wengi walimzunguka na kumsumbua. Waliamini kwa sasa PAU si mwanafunzi tena. Walipenda kufupisha jina hilo na kumuita PAU.

Viazi vitamu, bamia, nyanya chungu, na hata madegele. Vyote vilipatikana katika meza yao. Japo faida yake haikuwa kubwa sana. Kufeli shule si kufeli maisha. Kauli hiyo bado Paulina alipingana nayo vikali. Japo ilitoka vinywani kwa wale rafiki zake waliosoma shule moja.

Wanaume wengi walifika nyumbani kwa Mzee Makunja, kwa lengo la kupeleka posa. Paulina alikataa akidai kwamba muda bado. Anasubiri mchumba mwema kutoka kwa Bwana. Mzee hakutaka kumlazimisha akiogopa lawama hapo mbeleni. Kulingana na umri wake ameshuhudia ndoa nyingi sana, zikivunjika mapema.

"Mwanangu kila mchumba anayekuja nyumbani unamkataa. Mtoto wa kike kuna umri ukifika utahangaika sana kupata mchumba. Na hapo ndipo utapolazimisha kujikabidhi kwa mtu asiye sahihi kwako. Usinifikirie vibaya kwamba nakupangia, hapana binti yangu nakukumbusha tu, kwasababu nimeliona jua kabla yako. Na nimeshuhudia vitu vingi sana"

Alizungumza Mamake Paulina, akiwa anazifuta nyanya vumbi, na kuzipanga sehemu yake. Wakati Paulina alikuwa pembeni akipanga bamia.

Walizungumza kwa sauti ya chini kabisa, kuepuka mazungumzo yao kuwanufaisha watu wengine.

"Hapana Mama, siyo kwamba nakataa makusudi. Kuna kijana yupo tayari na kaishaonesha nia ya kunichumbia!"

"Unasema?" alistuka Mama.

"Ni kweli yupo!" alisisitiza Paulina.

"Mwanangu huwajui wanaume vizuri. Atakulaghai kwa maneno matamu, kwamba yuko tayari kukuoa. Tena wengine wanapeleka mpaka posa. Wapate uhalali wa kukutumia kikamilifu. Kua makini mwanangu!"

Aliongea kwa sauti ya jazba kidogo, japo ilikuwa ni ya kunong'ona. Maana anawajua wakwaya wakisikia neno, hawana jambo dogo.

"Sawa Mama nimekuelewa, nitazidisha umakini katika suala hili"

Baada ya jibu hilo kutoka kwa Paulina, waliendelea na shughuli ya kupanga bidhaa katika meza yao.
JUMAMOSI saa nne kamili za asubuh. Ugeni uliingia nyumbani kwa Mzee Makunja. Haukua wa kustukiza kwasababu tayari Paulina alikwisha wadokeza kwamba yule mchumba wake ataleta posa. Ikamlazimu mzee huyo kujikaza na kuketi kwaajili ya mazungumzo. Mambo yalienda vizuri binti akakubali na wazazi wakapokea kishika uchumba.

Mipango ya harusi iliendelea kupangwa, kwa upande wa mwanamke wao walikusudia kufanya sherehe ndogo kabisa. Kutokana na hali ya kiuchumi kuwa ngumu.

Manyama Makubi, ndiye mchumba wa binti Paulina. Ni kijana mrefu na mweusi. Upangiliaji wake mzuri wa mavazi, ulimuongezea utanashati. Ukute ndo sababu iliyomteka Paulina. Maana wazee wetu walisema mapenzi upofu. Kupenda sana ni ugonjwa usiotibika.

NYEGINA ndicho kijiji alichozaliwa Manyama na hapo ameweka makazi yake rasmi. Ni kijiji maarufu sana, hasa kwa Wakristo wa jimbo la Musoma Mjini. Wamissionari kipindi wakieneza Ukristo waliweza kuweka makazi yao hapo.

Na walitoa mchango mkubwa sana kudumisha MAHUSIANO mazuri na Serikali: Mapadre wa shirika la Maryknoll walikuwa marafiki wakubwa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mfano: Pd. William Collins ndiye aliyeshuhudia Ndoa ya Mwl. Nyerere na Maria Gabriel tarehe 24.01.1953. Kadhalika, mapadri Collins na Albert Nevins na John Considine ndio walitoa NAULI ya Mwl. Nyerere kutoka Ulaya kwenda Amerika kutetea Uhuru wa Tanganyika mbele ya Umoja wa Mataifa – March, 1955.


___________________ ITAENDELEA _____'_________


KAMA UNA CHANNEL YAKO YOU TUBE, UNAHITAJI SIMULIZI KWAAJILI YA KUSIMULIA .

BASI NIONE, BEI NI POA SAAAANA.

MAWASILIANO

0757 238 304 ( WhasAPP )

0713 417 189 ( piga simu au tuma sms )



JamiiForums1700149874.jpg
 
NIMESHINDWA KUISHI KWA MAKOSA YANGU MWENYEWE.....05
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304 ( WHATSAAP )

SEHEMU YA TANO.....



Ilipoishia sehemu ya nne...


NYEGINA ndicho kijiji alichozaliwa Manyama na hapo ameweka makazi yake rasmi. Ni kijiji maarufu sana, hasa kwa Wakristo wa jimbo la Musoma Mjini. Wamissionari kipindi wakieneza Ukristo waliweza kuweka makazi yao hapo. Na walitoa mchango mkubwa sana kudumisha MAHUSIANO mazuri na Serikali: Mapadre wa shirika la Maryknoll walikuwa marafiki wakubwa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mfano: Pd. William Collins ndiye aliyeshuhudia Ndoa ya Mwl. Nyerere na Maria Gabriel tarehe 24.01.1953. Kadhalika, mapadri Collins na Albert Nevins na John Considine ndio walitoa NAULI ya Mwl. Nyerere kutoka Ulaya kwenda Amerika kutetea Uhuru wa Tanganyika mbele ya Umoja wa Mataifa – March, 1955.


ENDELEA NAYO............


MANYAMA alikuwa ni mfanyabiashara wa samaki alizunguka vijiji vingi kutafuta samaki. Alianzia Bugoji, Bugwema, Bukima, Bukumi, Bulinga, Busambara, Bwasi, Etaro, Ifulifu, Kiriba, Makojo, Mugango, Murangi, Musanja, Suguti na kumalizia Tegeruka.

Biashara hiyo ilimuingizia kiasi kikubwa cha pesa. Alikuwa akimiliki pikipiki mbili, ng'ombe mmoja. na mbuzi watano. Kwa maisha ya mtanzania hawezi lala bila kula huyo, labda aamue mwenyewe.


UKUMBI WA CCM MUSOMA MJINI.

Zilisikika ndelemo na vifijo. Nyimbo za kijita zilipigwa kwa wingi. Wakwaya walifunga vibwebwe na kulisakata rumba. Alikuwa ni DJ maarufu aliyefahamika kama CLEO THE DJ. Ndugu wa maharusi kutoka Nyegina na Bisumwa walikuwa ndani ya nyumba. Kushuhudia vijana wao wakiaga ukapela. Wanaungana kuwa mwili mmoja. Pilau nyama na ndizi za kukaanga, watu walivishambulia kwa wingi. Mzee Makunja alishuhudia harusi ya binti yake angali akiwa bado anaumwa.

Manyama alikabidhiwa mkewe. Furaha ndani ya moyo wake haikuwa na kipimo. Ni kama alikuwa akiogelea kwenye bahari ya malavidavi. Alijuta kuchelewa kuoa. Akajifariji muda muafaka ulikuwa bado haujafika.

"Mwanangu nakusihi sana, muheshimu mumeo. Ukipata shida yeyote ile, wa kwanza kumueleza awe yeye kisha sisi. Nenda ukayaanze maisha mapya. Nenda ukawapende ndugu wa mumeo. Nenda ukauoneshe ulimwengu jinsi tulivyokulea katika maadili. Nenda ukamfanye mumeo ajihisi mwenye tabasamu na furaha muda wote."

Ilikuwa ni sauti ya chini kabisa, Mama Paulina akimnong'oneza bintiye wakiwa nje ya ukumbi. Na hapo harusi ilikuwa imefika tamati.

MIEZI MITATU na majuma mawili yalikuwa yamekatika baada ya harusi. Maisha yaliendelea, kila aliyepewa pumzi. Alizidi kuzipambania ndoto zake. Waliokata tamaa nao walizidi kuulaumu ulimwengu kwa kuwatunuku maisha hayo ya dhiki.

"Baby! wataka chakula gani leo?"
Sauti nzuri na nyororo, kutoka kinywani mwa Paulina iliuliza.

"We tena mpenzi wangu! chochote utachopika kwangu kitamu"

Alijibu Manyama, akiwa anamtazama mkewe kwa bashasha. Jinsi wanavyozungumza kwa mahaba. Ni kama unatazama tamthiliya za kikorea au kituruki. La asha..! hawa ni vijana wa musoma.

"Usiniambie! basi ntapika ugali na samaki wa kuchoma?"

"Kama umeota vile. Tengeneza na kachumbali kabisa, usisahau ndimu na pilipili"

Alidakia Manyama, akasimama na kwenda kumkumbatia mkewe. Dah! Kweli ndoa changa ina raha yake. Kama umekua ukisimuliwa juu ya penzi la dhati. Basi ukifika kwa wapendanao hawa utalishuhidia kwa macho.

"Aaahiiiiiiiiiiiiiiiiii"

Alipiga kelele Paulina kwamba kaungua, alipokuwa anachoma samaki. Lakini mlio huo alioutoa mmmmh. So kwamba kaungua, ilikuwa ni sauti ya mitego. Chezea watoto wa kike wewe utalala mlango wazi.

Chakula kiliiva wakaanza kula. Huku wakipiga stori za hapa na pale. Wakatumia wasaha huo. Kila mtu akawa simuliza mikasa mbali mbali ya maisha yake. Mbali na hayo waligeuka njiwa, maana sio kwa kulishana huko.

Maneno matamu pia yaliporomoshwa kutoka vinywani mwao. Yaliweza kusindikiza vyema chakula hicho.

KITANDANI ndipo walielekea kwaajili ya kupumzisha miili yao. Kila mtu aliomba dua zake akisisitiza Mwenyezi amuepushe na kifo cha ghafla. Baada ya hapo Paulina alijisogeza karibu kabisa na mumewe.

Akapokelewa vyema na kupakatwa ndani ya kifua kizuri. Binti wa watu alishindwa kujizuia, mwili mzima ulilegea kama mgonjwa aliyeshikwa na homa kali. Maneno hayakusikika vizuri. Ni kwamba homa ya mapenzi ilimzidia.

Angefanya nini binti wa watu. Kama sio kusubiri huduma kutoka kwa daktari wake aliyemchagua. Chumba kilitulia tuli. Hata wale mbu wasumbufu walikaa kimya. Ni kama waliisubiri dabi hiyo ya kariakoo. Si Paulina wala Manyama aliyesikika akizungumza, kilichokuwa kikiendelea hapo ni siri ya chumba hicho.


_____________ iTAENDELEA _________________
KAMA UNA CHANNEL YAKO YOU TUBE, UNAHITAJI SIMULIZI KWAAJILI YA KUSIMULIA .

BASI NIONE, BEI NI POA SAAAANA.

MAWASILIANO

0757 238 304 ( WhasAPP )

0713 417 189 ( piga simu au tuma sms )




JamiiForums1700149874.jpg
 
Back
Top Bottom