Nimeshtushwa Polisi kutishia uhai wa watoto kwa silaha za kivita

Nimeshtushwa Polisi kutishia uhai wa watoto kwa silaha za kivita

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925
SAM_4268.JPG
1.jpg



Hii ni dalili kwamba Tanzania hatuna sheria ya kutetea haki za watoto. Maandamano ya hawa watoto au wanafunzi hayakuwa uvujaji wa amani au sheria, bali kuisaidia serikali kufungua zaidi na kuona madai ya walimu yafikiwe mwafaka ili wasiendelee kukosa vipindi madarasani sababu ya mgomo wa walimu.

Askari polisi kutumia silaha za kivita kutishia uhai wa wanafunzi ni jambo hatari kabisa kwa malezi ya watoto hawa, la ajabu, na lisilo la kistaarbu kabisa, na kabisa kisaikolojia ni kuwaharibu hawa watoto. Athari za matukio ya polisi kutishia watoto kwa silaha kali za kivita ni kubwa katika maisha yao, na hapo ndipo busara inapokosekana kwa serikali na jeshi la polisi nchini ni kielelezo tosha.


SAM_4271.JPG


Tanzania hatuna wanasaikolojia wanaoweza kuwasaidia hawa watoto kuongea nao wakaelewa na pengine wakachukua mawazo ya watoto hawa na kuyafanyia kazi, na badala ya watoto hawa kuwatisha wanafunzi uhai wao ka mitutu ya bunguki na mabomu ya machozi, je walikuwa na silaha gani kama si mikono mitupu kudai haki yao ya kupata elimu jambo ambalo linaeleweka kwa kila mmoja? Wizara ya jamii na watoto kazi yao nini , na wanafanya nini kutetea hawa watoto?

Wanafunzi%2Bwa%2Bshule%2Bya%2BMSINGI%2BIpembe%252C%2BNyerere%252C%2BUnyankindi%2Bna%2BSingidani%2Bktk%2BManispaa%2BSingida%2Bwakiwa%2Bkatika%2Buwanja%2Bwa%2Bmbele%252C%2Bjengo.jpg


Hawa watoto ni haki yao kudai muda unaopotezwa na walimu wanapodai haki zao wakati wanakosa masomo madarasani. Binafsi sioni kosa la watoto kama maandamano yao yalikuwa ya amani, na kama waliziba njia ni bora kutumia njia za kisaikolojia kuwatuliza wanafunzi kuliko tishio la silaha za kivita.

Serikali iko tayari kusikiliza kilio cha wanasiasa wabunge kuwaongezea mishahara na malupulupu, lakini wanaosota maisha yao yote kuandaa hili taifa la kesho wamewapiga danadana siku nyingi na leo wanapochukua hatua serikali inaamua kumalizia hasira kwa hawa malaika wasio na makosa, waadhiriwa na mgomo wa walimu.

Je, serikali inapotumia jeshi la polisi kutishia watoto hawa ambao ni waadhirika wa kukosa masomo bila ridhaa yao kwa uzembe wa serikali yenyewe, je inajengwa taswira gani katika maisha, malezi na future ya watoto hawa?

:nono:Hili ndilo tatizo la vyombo vya dola vinapotumika zaidi kisiasa.:nono:​
 
hiyo ndo tanzania kila kitu kinawezekana ndugu.
 
Candid Scope, something is very wrong somewhere! I wish leaders could know what it is before too late.

Ile picha ya mtoto akipanda karandinga pasipo uoga inaongea mengi sana. I hope watawala wanasoma kinachoendelea - wasipuuzie na kudharau
 
Hata Ufalme wa Mfalme Jean Bedel Bokassa uliangushwa kwa kunyanyasa watoto wa shule.

Endeleeni kuwafunza protest ni nini hawa watoto ili waujue kiuhalisi udhalimu wenu mapema kabisa.
 
Candid Scope, something is very wrong somewhere! I wish leaders could know what it is before too late.

Kuwatishia uhai watoto hawa kwa bunduki ni kitu ambacho hakiingii akilini mwangu, siwezi kuelewa seikalini kuna matatizo gani. Hakuna chombo cho chote cha serikali kijamii kukemea tukio hilo, maana yake imehalalishwa, I don't understand at all, can't be acceptable
 
Dah...nakumbuka mimi wakati nipo darasa la saba hata ningeulizwa mgomo ni nini nisingeweza kujibu lakini leo hii hata mtoto wa darasa la kwanza anaujua mgomo na kale ka wimbo ka "tunaka haki yetu".
 
Dah...nakumbuka mimi wakati nipo darasa la saba hata ningeulizwa mgomo ni nini nisingeweza kujibu lakini leo hii hata mtoto wa darasa la kwanza anaujua mgomo na kale ka wimbo ka "tunaka haki yetu".

Mchelea mwana mwisho hulia, kama hatua stahiki zingechukuliwa toka awali na kutolimbikiza madai hayo, leo isingekuwa tatizo kugombana na walimu na kusababisha vitisho vya uhai wa wanafunzi kitu ambacho ni aibu sana tunayojitwika ukilinganisha na mataifa yanayojali haki za mtoto.
 
Tatizo ni mazoea ya kufilikili kwamba kila maandano ni vurugu na kushindwa kutambua jinsi ya kukabili maandamano kulingana na nature yake wao wanachojua ni kila maandano ni vurugu.Kweli inasikisha sana kuona askali wetu wanakimbilia mitutu ya bunduki kwa watoto wadogo hapa ni mwanzo wa kuwafundisha ujasili wa kivita kabla ya umri wao na hii tutegemee watoto wasiojali maslai ya nchi hapo baadae.Tufikilie njia za kisakologia katika jambo linalo husu watoto wetu.
 
Kuwatishia uhai watoto hawa kwa bunduki ni kitu ambacho hakiingii akilini mwangu, siwezi kuelewa seikalini kuna matatizo gani. Hakuna chombo cho chote cha serikali kijamii kukemea tukio hilo, maana yake imehalalishwa, I don't understand at all, can't be acceptable

Nimepoteza imani na mambo mengi sana yanayoendelea. Yaashiria tumeamua kukosa umakini kwa makusudi kabisa. I don't understand....
 
Huyu Kikwete sasa naona anakaribia kaburi ,Kifo ndicho kilichobaki nchi imesaini na imeridha mkataba wa kimataifa wa 1990 wa ulinzi wa watoto, sheria ya watoto ya mwaka 2010 Kikwete kasaini ataamrishaje Polisi na mitutu ya bunduki wawakamate watoto na kuwatia kwenye karandiga huu ni uozo uliopitiliza huyu kweli ni Raisi wa nchi ya mmaamuma you cant just swallow this nosense
 
Ile picha ya mtoto akipanda karandinga pasipo uoga inaongea mengi sana. I hope watawala wanasoma kinachoendelea - wasipuuzie na kudharau

I dont understand...ninashindwa kuelewa tunaelekea wapi. Tunataka kutengeneza Taifa la watu wakorofi korofi? Kwa faida ya nani?
 
​wacha watoto wazoee mitutu siku wakiingia mtaani kijani na njano mna hali mbaya
Ile picha ya mtoto akipanda karandinga pasipo uoga inaongea mengi sana. I hope watawala wanasoma kinachoendelea - wasipuuzie na kudharau
 
Kuwatishia uhai watoto hawa kwa bunduki ni kitu ambacho hakiingii akilini mwangu, siwezi kuelewa seikalini kuna matatizo gani. Hakuna chombo cho chote cha serikali kijamii kukemea tukio hilo, maana yake imehalalishwa, I don't understand at all, can't be acceptable

Candid Scope, tatizo kubwa tulilo nalo sisi Wabongo ni kufikiri kuwa tuna serikali. Hiki tulicho nacho ni genge la mafisadi (kleptocractic regime). Kwa hivyo, kusema huwezi "kuelewa serikalini kuna matatizo gani" ni bahati mbaya kufikiri hivyo -Bongo hakuna serikali!
 
Ile picha ya mtoto akipanda karandinga pasipo uoga inaongea mengi sana. I hope watawala wanasoma kinachoendelea - wasipuuzie na kudharau
unawajua hao watawala kweli?mambo mazito kama hayo hawayaoni.wanachukulia poa ,mabweg.e yale hayana jipya
 
ukiona mpaka watoto wa miaka saba wanaandamana na kubebwa na polisi kama majambazi ujue tumefika mwisho tunahitaji maombi sana....
 
Inasikitisha kwakweli. Mlolongo wa matukio ya kipuuzi huku kukiwa hakuna sauti zenye mwangwi wa kutosha kuyakemea imefanya mambo kama haya kuonekana ya kawaida. TUKO WAPI WATANZANIA? TUKO WAPI WAZAZI? Hali tusiwasimamie watoto hawa na madai yao hadi waonekane ni watukutu tu waliotumwa na si wenye kilio cha kweli
 
Back
Top Bottom