Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
SALEH RAJAB TAMBWE, JOB LUSINDE NA SAMWEL SITTA
Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Balozi Saleh Tambwe ambae tukifahamiana kwa miaka mingi na yeye akimjua babu yangu katika kundi la wazee wa Kimanyema waliopigania uhuru wa Tanganyka kutokea Tabora, Western Province.
Katika kundi hili alikuwapo Rajab Tambwe, Abdallah na Maulidi Kivuruga, Bilali Rehani Wiakela, Issa Kibira kwa kuwataja wachache.
Kiasi cha kama miaka mitatu hivi nilikutana na Balozi Tambwe Makaburi ya Kisutu akiwa ameongozana na Balozi Job Lusinde na Spika Samwel Sitta.
Balozi Tambwe akanitambulisha kwao na tukawa na mazungumzo ya hapa na pale.
Nakumbuka nilimwambia Mh. Samwel Sitta kuwa mimi namfahamu toka utoto wangu Tabora nilipokuwa nikienda likizo kwa babu yangu Baba Popo.
Jina hili ni maarufu tukawa tumefahamiana.
Lakini nikamtajia kitu ambacho naamini hakukitegemea kutoka kwangu nilipomwambia kuwa akiwa mwanafunzi alipata kushinda mashindano ya kuandika insha ya Kiingereza na zawadi yake ilikuwa safari ya Marekani.
Alifurahi sana kwa mimi kumtambua hivyo.
Balozi Job Lusinde nilimwambia kuwa nimemtaja katika kitabu cha Abdul Sykes wakati akiwa mwalimu Alliance Secondary School, Dodoma, Central Province.
Kulikuwa na mgogoro wa kuunda tawi la TANU pale mjini na viongozi wa harakati hizi alikua Omari Suleiman aliyekuwa fundi cherahani na Haruna Taratibu Fundi Mwashi, Public Works Department (PWD).
Job Lusinde na wasomi wengine wa Makerere waliokuwa walimu pale Alliance walijiweka mbali na harakati hizi kwa kuhofia kupoteza kazi zao.
Lakini mimi sikumpeleka huko nilitosheka na kumfahamisha kuwa nimemtaja katika kitabu changu.
Job Lusinde alinijia kama mtu mkimya na mpole jinsi alivyokuwa anazungumza na mimi.
Nilikuwa na nakala ya kitabu hicho katika mkoba wangu nikaufungua nikamkabidhi.
Alinishukuru na nikawaomba niwapige picha ya pamoja wakanikubalia nikawapiga na tukaagana.
Job Lusinde alinijia kama mtu mkimya na mpole jinsi alivyokuwa anazungumza na mimi.
Haukupita muda mrefu Spika Samuel Sitta akafariki, kisha Balozi Job Lusinde na leo Balozi Saleh Rajab Tambwe ametangulia kwa Mola wake.
Tunamuomba Allah amfanyie wepesi Balozi Tambwe katika safari yake hii.
Angalia picha: SALEH RAJAB TAMBWE, JOB LUSINDE NA SAMWEL SITTA
Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Balozi Saleh Tambwe ambae tukifahamiana kwa miaka mingi na yeye akimjua babu yangu katika kundi la wazee wa Kimanyema waliopigania uhuru wa Tanganyka kutokea Tabora, Western Province.
Katika kundi hili alikuwapo Rajab Tambwe, Abdallah na Maulidi Kivuruga, Bilali Rehani Wiakela, Issa Kibira kwa kuwataja wachache.
Kiasi cha kama miaka mitatu hivi nilikutana na Balozi Tambwe Makaburi ya Kisutu akiwa ameongozana na Balozi Job Lusinde na Spika Samwel Sitta.
Balozi Tambwe akanitambulisha kwao na tukawa na mazungumzo ya hapa na pale.
Nakumbuka nilimwambia Mh. Samwel Sitta kuwa mimi namfahamu toka utoto wangu Tabora nilipokuwa nikienda likizo kwa babu yangu Baba Popo.
Jina hili ni maarufu tukawa tumefahamiana.
Lakini nikamtajia kitu ambacho naamini hakukitegemea kutoka kwangu nilipomwambia kuwa akiwa mwanafunzi alipata kushinda mashindano ya kuandika insha ya Kiingereza na zawadi yake ilikuwa safari ya Marekani.
Alifurahi sana kwa mimi kumtambua hivyo.
Balozi Job Lusinde nilimwambia kuwa nimemtaja katika kitabu cha Abdul Sykes wakati akiwa mwalimu Alliance Secondary School, Dodoma, Central Province.
Kulikuwa na mgogoro wa kuunda tawi la TANU pale mjini na viongozi wa harakati hizi alikua Omari Suleiman aliyekuwa fundi cherahani na Haruna Taratibu Fundi Mwashi, Public Works Department (PWD).
Job Lusinde na wasomi wengine wa Makerere waliokuwa walimu pale Alliance walijiweka mbali na harakati hizi kwa kuhofia kupoteza kazi zao.
Lakini mimi sikumpeleka huko nilitosheka na kumfahamisha kuwa nimemtaja katika kitabu changu.
Job Lusinde alinijia kama mtu mkimya na mpole jinsi alivyokuwa anazungumza na mimi.
Nilikuwa na nakala ya kitabu hicho katika mkoba wangu nikaufungua nikamkabidhi.
Alinishukuru na nikawaomba niwapige picha ya pamoja wakanikubalia nikawapiga na tukaagana.
Job Lusinde alinijia kama mtu mkimya na mpole jinsi alivyokuwa anazungumza na mimi.
Haukupita muda mrefu Spika Samuel Sitta akafariki, kisha Balozi Job Lusinde na leo Balozi Saleh Rajab Tambwe ametangulia kwa Mola wake.
Tunamuomba Allah amfanyie wepesi Balozi Tambwe katika safari yake hii.
Amin.
Angalia picha: SALEH RAJAB TAMBWE, JOB LUSINDE NA SAMWEL SITTA