Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Hivi ni Kabila au ni hulka za watu tu?
Naamini kuna waha swaaafi kabisa n'a kuna wasio kuwa waha n'a ni washirikina mbayaaaa..
Mkuu ogopa sana jamii zenye asiri ya machafuko. The only way used to protect themselves was through witchcraft. So baada ya kupata sehemu iliyosettle hayo mambo hawakuyaacha na sasa wamegeuza malengo ya zamani😌
 
Mkuu ogopa sana jamii zenye asiri ya machafuko. The only way used to protect themselves was through witchcraft. So baada ya kupata sehemu iliyosettle hayo mambo hawakuyaacha na sasa wamegeuza malengo ya zamani[emoji18]
Kama nimekuelewa vileee
 
Dogo, kama yamekukuta kweli, ni stori ya mwezio au umetunga! Kama kweli ni wewe basi una safari ndefu sana ya maisha. Unachikulia poa masuala serious, unaona ni kitu kidogo tu, unajiona uko sawa, huonekani kujutia wala kukubali kuwa una makosa na kuwa hayo waliyokufanyia walikuonea!

Ulitakiwa uende kwa hofu na unyenyekevu mkubwa ili mambo yasiwe makubwa. Kumbuka wewe nawe ni mzazi, unapaswa kujifunza na kujiandaa kwa ajili ya nyakati zijazo. Uyafanyayo sasa huenda utakutana nayo baadaye, jifunze kitu, jifunze ku-handle haya mambo kwa hofu na unyenyekevu, huenda hayo uliyofanya na kuyafanya dhidi ya mkweo, naye ujanani alikuwa na akili kama zako na sasa wewe unatumika kumkumbusha aliyomfanyia mwenzake.

Vv
 
Tulienda na gari tukaiacha mjini, kutoka mjini kwenda huko Kijijini tulikodi boda boda kwani njia ni mbaya mno!
Mlienda na gari yenu private? Kwanini usingewabeba wazee wa heshima (akiwemo baba yako?) Angalau baba mkwe wako asingekuwa na hasira na wewe, mlienda wepesi mno ndo maana, wazee huwa wanaongeza uzito wa ugeni. Bro wako tu asingetosha
 
Nasikitika kwamba unanihukumu kwa hisia zako tu, ukisema nilitakiwa kwenda kwa "unyenyekevu mkubwa" una maanisha nini? Kwamba nilienda pasipokuwa mnyenyekevu?

Brother kwa akili ya kawaida tu, unawezaje kwenda ukweni, tena kwa mara ya kwanza na usiwe mnyenyekevu? Au unyenyekevu unaomaanisha ni wa aina gani?

Halafu ni mtu katili pekee anayeweza kufikiria kuwa safari ya Dar mpaka Kigoma, nikiambatana na kaka yangu mkubwa (mbadala wa baba yangu kwani mzee alishafariki) ni mzaha, lakini kwa yeyote aliye timamu kabisa alipaswa kuiona hiyo dhamira yetu,na angalau kutupokea kama binadamu (hata kama kuna makosa tuliyowahi kuyafanya, mimi n'a mtoto wake)

Lakini kutu-harass na kutufedhehesha mbele za watu,na kutaja pesa anazojua kabisa kuwa hatuwezi kuzilipa ni ukatili mno!
 
Mlienda na gari yenu private? Kwanini usingewabeba wazee wa heshima (akiwemo baba yako?) Angalau baba mkwe wako asingekuwa na hasira na wewe, mlienda wepesi mno ndo maana, wazee huwa wanaongeza uzito wa ugeni. Bro wako tu asingetosha
Huyu kaka yangu ana zaidi ya miaka 50, lakini ndiye baba yetu kwani baba mzazi alishafariki miaka mingi tu!

That is why,nilinunua zawadi za yule mzee kichwani nikiamini atakuwa baba yetu (Mimi na mke wangu) lakini alinivunja moyo sanaaa!
 
Huyu kaka yangu ana zaidi ya miaka 50, lakini ndiye baba yetu kwani baba mzazi alishafariki miaka mingi tu!

That is why,nilinunua zawadi za yule mzee kichwani nikiamini atakuwa baba yetu (Mimi na mke wangu) lakini alinivunja moyo sanaaa!
Pole sana mwamba. Emu jipe muda kila kitu kitakuwa sawa tu hakuna mzazi asiyependa binti yake aolewe.
 
Pole sana mwamba. Emu jipe muda kila kitu kitakuwa sawa tu hakuna mzazi asiyependa binti yake aolewe.
Ninaweza kuendelea na maisha na mke wangu, lakini yule mzee sijui kama nitampa value niliyokuwa nampa awali, na kwa vyovyote vile mke wangu hawezi kukubali baba yake asithaminiwe na mimi mumewe, inaweza kuwa shida baadaye, that is why nafikiria kumuacha tu, nihesabu kwamba nimekataliwa kwao n'a mimi siwezi kulazimisha!
 
Na hapa ndipo penye mkwamo, nakosa namna yoyote ya kufanya isipokuwa kumuacha kabisa mtoto wao, japo ni kweli nampenda ila sina namna!
Mkuu si Kila anayeishi na mke anayempenda anamahusiano mazuri na wazazi hapana wewe jikite kuwasamehe hujui makuzi ya Mzee hivyo inahitaji utulivu wa Hali ya juu na endelea kuwa na mawasiliano na mshenga kujua kama utulivu mmemrejea mzee
 
Sidhani kama unampenda kweli unampenda huyo dada, upendo una gharama, kama kweli unampenda gharama haziwezi kuzuia nia yako ya kufunga naye ndoa, mtu ni raslimali nambari moja. Au huyo dada yeye hachangii kwente uchumi wako? Kama hana mchango, mnapanga iwe hivyo maisha yenu? Yakobo [kama unasoma Biblia], kwa upendo wake kwa Raheli, alikuwa tayari kumtumikia mkewe kwa miaka 7 zaidi.

Vv
 
Kwa hiyo ulilipa pungufu ya asilimia 10 ya mahari?

Ajabu sisi tumeenda na Milioni moja mzee anakataa na kudai anataka 4 Milioni,hakika sitampelekea hiyo pesa hata kwa fimbo
Sijawapa tena fedha na baada ya kukabidhiwa Binti na Mimba nikapachika biashara ya Mahari ikaishia hapo.

Jambo zuri nilikuja kuambiwa kuwa kwao ni marufuku Mahari kulipwa yote (Wanasema ukilipa mahari yote ni sawa umemnunua binti yao) Hivyo nimejikausha na wao hawajaulizia tena.
 
Pole sana Mzee wangu,hapo Kuna mambo yakujifunza,pia jitahid uwe makini haswa kwenye swala la kimaamuzi maana Kuna mitego wamekupa bila wewe kujua" umeondoka na mwanamke ni ishara ya utayari wako kutoa mahali ambayo wametaka, pia kitendo Cha mwanamke kukulilia na kukushika miguu huyo Kuna jambo la hatari ambalo alishapewa kama onyo na huyo Mzee, pia jitahid sana kutoa mahali japo taratibu ingawaje wamefanya kama kukuadhibu kurudisha garama zao za masomo na kuwadharaulisha Hilo inategemea na Mila zao, pili usipotoa mahali ukiacha mambo ya kishirikina na ikatokea bahati mbaya mwanamke amepatwa na tatizo kubwa (kifo) huyo Mzee anaweza akakuzilia/ kususa na akagomesha wasizike mpaka alipwe mahali! Sasa binafsi naona ni mtego ndiomana walikuwa radhi kuacha uondokenae hvyo kwenye maamuzi jitahid ushirikishe wazee wako na wenyeji wa kiha ili iwe salama kwako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…